Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 30.34
Bible en Swahili de l’est


1 Naye Raheli alipoona ya kuwa hamzalii Yakobo mwana, Raheli alimwonea ndugu yake wivu. Akamwambia Yakobo, Nipe wana; kama sivyo, nitakufa mimi.
Genèse 29.31 Genèse 37.11 1 Samuel 1.4-1.8 Job 3.1-3.3 Proverbes 14.30
2 Yakobo akamghadhibikia Raheli, akasema, Je! Mimi ni badala ya Mungu, aliyekuzuilia uzao wa mimba?
Genèse 16.2 1 Samuel 1.5 Psaumes 127.3 2 Rois 5.7 Genèse 25.21
3 Akasema, Yuko mjakazi wangu, Bilha, uingie kwake ili kwamba azae juu ya magoti yangu, nami nipate uzao kwa yeye.
Genèse 50.23 Job 3.12 Genèse 30.9 Ruth 4.11 Genèse 16.2-16.3
4 Basi akampa Bilha mjakazi wake kuwa mkewe. Yakobo akaingia kwake.
Genèse 16.3-16.4 Genèse 25.1 Genèse 33.2 Genèse 35.22 Genèse 22.24
5 Naye Bilha akapata mimba, akamzalia Yakobo mwana.
6 Raheli akasema, Mungu amenipa haki yangu, naye amesikia sauti yangu, akanipa mwana. Kwa hiyo akamwita jina lake Dani.
Lamentations 3.59 Psaumes 43.1 Psaumes 35.24 Genèse 49.16-49.17 Jérémie 13.24
7 Bilha, mjakazi wa Raheli, akapata mimba tena, akamzalia Yakobo mwana wa pili.
8 Raheli akasema, Kwa mashindano makuu nimeshindana na ndugu yangu, nikashinda. Akamwita jina lake Naftali.
Genèse 49.21 Matthieu 4.13 Exode 9.28 Deutéronome 33.23 1 Samuel 14.15
9 Lea alipoona ya kuwa ameacha kuzaa, alimtwaa Zilpa, mjakazi wake, akampa Yakobo kuwa mkewe.
Genèse 30.4 Genèse 29.35 Genèse 16.3 Genèse 30.17
10 Zilpa, mjakazi wa Lea, akamzalia Yakobo mwana.
11 Lea akasema, Bahati njema! Akamwita jina lake Gadi.
Genèse 49.19 Genèse 46.16 Genèse 35.26 Deutéronome 33.20-33.21 Esaïe 65.11
12 Zilpa, mjakazi wa Lea, akamzalia Yakobo mwana wa pili.
13 Lea akasema, Ni heri mimi, maana wanawake wataniita heri. Akamwita jina lake Asheri.
Luc 1.48 Genèse 49.20 Genèse 35.26 Proverbes 31.28 Cantique 6.9
14 Reubeni akaenda siku za mavuno ya ngano akaona tunguja kondeni, akazileta kwa Lea mamaye. Ndipo Raheli akamwambia Lea, Nipe mimi baadhi ya tunguja za mwanao.
Cantique 7.13 Genèse 25.30
15 Naye akamwambia, Je! Ni jambo dogo kuninyang’anya mume wangu; hata wataka kuzitwaa tunguja za mwanangu pia? Raheli akamwambia, Kwa hiyo atalala kwako usiku huu kwa tunguja za mwanao.
Nombres 16.13 Nombres 16.9-16.10 Esaïe 7.13 1 Corinthiens 4.3 Ezéchiel 16.47
16 Yakobo akaja kutoka kondeni jioni, Lea akatoka kumlaki, akasema, Lazima uje kwangu, kwa sababu nimekuajiri, kwa tunguja za mwanangu; akalala kwake usiku ule.
17 Mungu akamsikia Lea, naye akapata mimba, akamzalia Yakobo mwana wa tano.
Exode 3.7 1 Samuel 1.20 Luc 1.13 Genèse 30.6 Genèse 30.22
18 Lea akasema, Mungu amenipa ujira wangu, kwa sababu nimempa mume wangu mjakazi wangu. Akamwita jina lake Isakari.
Genèse 46.13 Genèse 49.14-49.15 Genèse 35.23 Deutéronome 33.18 1 Chroniques 12.32
19 Lea akapata mimba tena, akamzalia Yakobo mwana wa sita.
20 Lea akasema, Mungu amenipa mahari njema, sasa mume wangu atakaa nami, kwa kuwa nimemzalia wana sita. Akamwita jina lake Zabuloni.
Genèse 35.23 Genèse 49.13 Matthieu 4.13 Psaumes 68.27 Juges 5.14
21 Baadaye akazaa binti, akamwita jina lake Dina.
Genèse 46.15 Genèse 34.26 Genèse 34.1-34.3
22 Mungu akamkumbuka Raheli; Mungu akamsikia, akamfungua tumbo.
Genèse 29.31 1 Samuel 1.19-1.20 Genèse 8.1 Genèse 25.21 Psaumes 105.42
23 Akapata mimba, akazaa mwana, akasema, Mungu ameondoa aibu yangu.
Luc 1.25 Esaïe 4.1 1 Samuel 1.5-1.6 Genèse 29.31 Luc 1.21
24 Akamwita jina lake Yusufu, akisema, Bwana aniongeze mwana mwingine.
Genèse 35.24 Genèse 49.22-49.26 Genèse 37.2 Genèse 42.6 Genèse 39.1-39.23

Départ de Jacob pour Canaan

25 Ikawa Raheli alipomzaa Yusufu, Yakobo akamwambia Labani, Nipe ruhusa niende kwetu, na kwenye nchi yangu.
Genèse 24.54 Genèse 24.56 Genèse 18.33 Genèse 28.15 Genèse 24.6-24.7
26 Nipe wake zangu na watoto wangu, niliokutumikia, niende zangu, maana umejua utumishi wangu niliokutumikia.
Osée 12.12 Genèse 29.30 Genèse 31.6 Genèse 29.19-29.20 Genèse 30.29-30.30
27 Labani akamwambia, Iwapo nimeona fadhili machoni pako, kaa, maana nimetambua ya kwamba Bwana amenibariki kwa ajili yako.
Genèse 26.24 Esaïe 61.9 Ruth 2.13 Genèse 39.21-39.23 Actes 7.10
28 Akasema, Sema mshahara wako utakao, nami nitatoa.
Genèse 29.15 Genèse 29.19
29 Akamwambia, Umejua jinsi nilivyokutumikia, na jinsi wanyama wako walivyokuwa kwangu.
Genèse 31.6 Genèse 31.38-31.40 Matthieu 24.45 1 Pierre 2.18 Genèse 30.5
30 Maana mali yako ilikuwa haba kabla sijaja, nayo imezidi kuwa nyingi, Bwana akakubariki kila nilikokwenda. Basi sasa, nitaangalia lini mambo ya nyumba yangu mwenyewe?
1 Timothée 5.8 Deutéronome 11.10 2 Corinthiens 12.14
31 Akamwuliza, Nikupe nini? Yakobo akasema, Usinipe kitu; ukinifanyia neno hili, nitalisha wanyama wako tena na kuwalinda.
Psaumes 118.8 2 Samuel 21.4-21.6 Hébreux 13.5
32 Nitapita katika wanyama wako wote leo, na kutoa huko kila mnyama aliye na madoadoa na marakaraka, na kila mnyama mweusi katika hao kondoo, na aliye na marakaraka na madoadoa katika mbuzi; nao watakuwa mshahara wangu.
Genèse 31.8 Genèse 31.10 Genèse 30.35
33 Na haki yangu itanishuhudia katika siku zijazo, utakapokuja kwa habari ya mshahara wangu ulioko kwako. Kila asiye madoadoa au marakaraka katika mbuzi, au asiye mweusi katika kondoo, akionekana kwangu, itahesabiwa kuwa ameibiwa.
Exode 13.14 2 Samuel 22.21 Psaumes 37.6 1 Samuel 26.23 Esaïe 59.12
34 Labani akasema, Tazama, na iwe hivi kama usemavyo.
Nombres 22.29 Galates 5.12 1 Corinthiens 14.5 1 Corinthiens 7.7
35 Basi akatoa siku ile mbuzi waume walio na milia na madoadoa, na mbuzi wake walio na madoadoa na marakaraka, kila aliye na doa jeupe, na kondoo wote waliokuwa weusi, akawatia mikononi mwa wanawe.
Genèse 31.9
36 Akajitenga na Yakobo mwendo wa siku tatu; naye Yakobo akachunga wanyama wa Labani waliosalia.
37 Yakobo akatwaa fito za mlubna mbichi, na mlozi, na mwaramoni, akazibambua maganda, mistari myeupe ionekane ndani ya hizo fito.
Ezéchiel 31.8 Genèse 31.9-31.13
38 Akazisimamisha fito hizo alizozibambua katika mabirika ya kunyweshea maji, pale walipokuja wanyama wanywe; wakachukua mimba walipokuja kunywa.
39 Wanyama wakapata mimba mbele ya hizo fito, wakazaa wanyama walio na milia, na madoadoa, na marakaraka.
Genèse 31.38 Exode 12.35-12.36 Genèse 31.9-31.12 Genèse 31.40 Genèse 31.42
40 Na Yakobo akawatenga wana-kondoo, akazielekeza nyuso za makundi zielekee wale waliokuwa na milia, na kila aliyekuwa mweusi katika wanyama wa Labani. Akaweka kando wanyama wake mwenyewe, wala hakuwachanganya pamoja na wanyama wa Labani.
41 Ikawa kila walipopata mimba wanyama wenye nguvu, Yakobo akaziweka zile fito mbele ya macho ya hao wanyama katika mabirika ili kwamba wachukue mimba kati ya zile fito,
42 lakini wanyama walipodhoofika hakuziweka zile fito. Basi wale dhaifu walikuwa wa Labani, na wenye nguvu walikuwa wa Yakobo.
43 Kwa hiyo mtu huyo akazidi mno, akawa na wanyama wengi, na vijakazi, na watumwa, na ngamia, na punda.
Genèse 30.30 Genèse 26.13-26.14 Genèse 24.35 Genèse 13.2 Genèse 28.15

Cette Bible est dans le domaine public.