Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 20.11
Bible en Swahili de l’est


Séjour d’Abraham à Guérar

1 Ibrahimu akaondoka huko kwenda nchi ya kusini, akakaa kati ya Kadeshi na Shuri, naye akatembea katika Gerari.
Genèse 26.6 Genèse 18.1 Genèse 26.1 Genèse 16.7 Genèse 16.1
2 Ibrahimu akamnena Sara mkewe, Huyu ni ndugu yangu. Basi Abimeleki mfalme wa Gerari akapeleka watu akamtwaa Sara.
Genèse 26.7 Genèse 12.15 Genèse 12.11-12.13 Genèse 26.1 Ecclésiaste 7.20
3 Lakini Mungu akamjia Abimeleki katika ndoto ya usiku, akamwambia, Umekuwa mfu wewe kwa sababu ya mwanamke huyu uliyemtwaa, maana ni mkewe mtu.
Genèse 20.7 Job 33.15 Psaumes 105.14 Matthieu 1.20 Matthieu 27.19
4 Basi Abimeleki alikuwa hakumkaribia, akasema, Ee Bwana, Je! Utaua hata taifa lenye haki?
Genèse 18.23-18.25 1 Chroniques 21.17 Genèse 19.24 Genèse 20.17-20.18 2 Samuel 4.11
5 Je! Hakuniambia mwenyewe, Huyu ni ndugu yangu? Na mwanamke mwenyewe naye alisema, Huyu ni ndugu yangu. Kwa ukamilifu wa moyo wangu, na kwa kuwa safi mikono yangu, nimefanya hivi.
1 Rois 9.4 Psaumes 7.8 Psaumes 25.21 Psaumes 78.72 Job 33.9
6 Mungu akamwambia katika ndoto, Nami nimejua ya kwamba kwa ukamilifu wa moyo wako umefanya hivi, ndipo nami nikakuzuia usinitendee dhambi, kwa hiyo sikukuacha umguse.
1 Samuel 25.34 1 Samuel 25.26 Genèse 39.9 Genèse 31.7 Psaumes 51.4
7 Basi sasa umrudishe mwanamke kwa mtu huyo, maana yeye ni nabii, naye atakuombea, upate kuishi. Bali usipomrudisha, fahamu ya kwamba kwa hakika utakufa wewe na watu wote ulio nao.
Job 42.8 1 Samuel 7.5 2 Samuel 24.17 2 Rois 5.11 Nombres 16.32-16.33
8 Abimeleki akaamka asubuhi na mapema, akawaita watumwa wake wote, akawaambia maneno hayo yote masikioni mwao, nao watu hao wakaogopa sana.
9 Kisha Abimeleki akamwita Ibrahimu, akamwambia, Umetutenda nini? Nimekukosa nini, hata ukaleta juu yangu na juu ya ufalme wangu dhambi kuu? Umenitenda matendo yasiyotendeka.
Genèse 12.18 Genèse 39.9 Genèse 34.7 Genèse 26.10 1 Samuel 26.18-26.19
10 Abimeleki akamwambia Ibrahimu, Umeona nini hata ukatenda jambo hili?
11 Ibrahimu akasema, Kwa sababu naliona, Yakini hapana hofu ya Mungu mahali hapa, nao wataniua kwa ajili ya mke wangu.
Genèse 26.7 Genèse 12.12 Proverbes 16.6 Genèse 42.18 Néhémie 5.15
12 Naye kweli ni ndugu yangu, binti wa baba yangu ila siye mwana wa mama yangu, ndipo akawa mke wangu.
Genèse 11.29 Genèse 12.13 1 Thessaloniciens 5.22
13 Ikawa hapo Mungu aliponisafirisha kutoka nyumba ya baba yangu, nikamwambia, Hii ndiyo fadhili yako, utakayonifanyia. Kila mahali tuingiapo, useme, Huyu ni ndugu yangu.
Genèse 12.1 Genèse 12.9 Genèse 12.11-12.20 Actes 5.9 Psaumes 64.5
14 Basi Abimeleki akatwaa kondoo, na ng’ombe, na watumwa, na wajakazi, akampa Ibrahimu, akamrudishia Sara mkewe.
Genèse 12.16 Genèse 20.7 Genèse 20.2 Genèse 20.11 Genèse 12.19-12.20
15 Abimeleki akasema, Nchi yangu iko mbele yako, kaa upendapo.
Genèse 13.9 Genèse 34.10 Genèse 47.6
16 Naye akamwambia Sara, Tazama! Nimempa ndugu yako fedha elfu, itakuwa kifunika macho kwako mbele ya wote walio pamoja nawe, nawe utakuwa na haki mbele ya watu wote.
Genèse 20.5 Proverbes 27.5 Genèse 24.65 1 Chroniques 21.3-21.6 Proverbes 25.12
17 Ibrahimu akamwomba Mungu, Mungu akamponya Abimeleki, na mkewe, na wajakazi wake, nao wakazaa wana.
Jacques 5.16 Philippiens 4.6 1 Thessaloniciens 5.25 Genèse 29.31 Proverbes 15.29
18 Maana Bwana alikuwa ameyafunga matumbo ya watu wa nyumbani mwa Abimeleki, wasizae, kwa ajili ya Sara mkewe Ibrahimu.
Genèse 12.17 1 Samuel 1.6 Genèse 16.2 Genèse 20.7 Genèse 30.2

Cette Bible est dans le domaine public.