Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Samuel 13.13
Bible en Swahili de l’est


Règne de Saül

Guerre contre les Philistins

1 Sauli alikuwa na umri wa miaka kadha wa kadha hapo alipoanza kutawala;naye akatawala miaka kadha wa kadha juu ya Israeli.
Michée 6.6 Exode 12.5
2 Naye Sauli alijichagulia watu elfu tatu wa Israeli; ambao katika hao, elfu mbili walikuwa pamoja na Sauli katika Mikmashi, na katika mlima wa Betheli na elfu moja pamoja na Yonathani katika Gibea ya Benyamini; nao wale watu waliosalia akawaruhusu waende kila mtu hemani kwake.
1 Samuel 10.26 1 Samuel 14.31 1 Samuel 13.5 1 Samuel 13.23 Josué 18.28
3 Yonathani akaipiga hiyo ngome ya Wafilisti, iliyokuwako huko Gibea, nao Wafilisti wakapata habari. Naye Sauli akapiga tarumbeta katika nchi yote, huku akisema, Na wasikie Waebrania.
1 Samuel 10.5 Juges 3.27 Juges 6.34 1 Samuel 13.16 2 Samuel 20.1
4 Waisraeli wote wakasikia habari ya kwamba Sauli ameipiga hiyo ngome ya Wafilisti, na ya kwamba Waisraeli wamepata kuwa makuruhi kwa Wafilisti. Basi hao watu wakakusanyika pamoja kumfuata Sauli huko Gilgali.
Genèse 34.30 Exode 5.21 1 Samuel 11.14-11.15 Genèse 46.34 Zacharie 11.8
5 Nao Wafilisti wakakusanyana ili wapigane na Waisraeli, magari thelathini elfu, na wapanda farasi sita elfu, na watu kama mchanga ulio ufuoni mwa bahari kwa wingi wao; wakapanda juu, wakapiga kambi yao katika Mikmashi, upande wa mashariki wa Beth-aveni.
Josué 11.4 1 Samuel 14.23 Josué 18.12 Genèse 22.17 Jérémie 15.8
6 Hata Waisraeli walipoona ya kuwa wa katika dhiki, (maana watu walifadhaishwa), ndipo hao watu wakajificha katika mapango, na katika vichaka, na katika miamba, na katika mashimo, na katika mabirika.
Juges 6.2 Hébreux 11.38 Josué 8.20 Philippiens 1.23 Juges 10.9
7 Hata baadhi ya Waebrania walivuka Yordani, wakaingia nchi ya Gadi na Gileadi; lakini Sauli alikuwa akaliko huko Gilgali, nao watu wote wakamfuata wakitetemeka.
Osée 11.10-11.11 Deutéronome 28.25 Deutéronome 3.12 Deutéronome 20.8 Nombres 32.1-32.5
8 Akangoja siku saba, kwa kadiri ya muhula uliowekwa na Samweli lakini Samweli hakuja Gilgali; na hao watu wakatawanyika mbali naye.
1 Samuel 10.8
9 Sauli akasema, Nileteeni hapa sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani. Akaitoa sadaka ya kuteketezwa.
1 Rois 3.4 Deutéronome 12.6 2 Samuel 24.25 Esaïe 66.3 Proverbes 21.3
10 Hata mara alipokwisha kuitoa hiyo sadaka ya kuteketezwa, kumbe! Samweli akatokea. Naye Sauli akatoka kwenda kumlaki na kumsalimu.
1 Samuel 15.13 Psaumes 129.8 Ruth 2.4
11 Samweli akasema, Umefanya nini? Naye Sauli akasema, Ni kwa sababu naliona ya kuwa watu wanatawanyika mbali nami, na wewe hukuja siku zile zilizonenwa; nao Wafilisti wamekusanyika pamoja huko Mikmashi;
1 Samuel 13.2 1 Samuel 13.23 1 Samuel 13.5 1 Samuel 13.16 Josué 7.19
12 basi nikasema, Wafilisti watanishukia sasa mpaka Gilgali, kabla sijaomba fadhili za Bwana; kwa hiyo nalijishurutisha, nikatoa sadaka ya kuteketezwa.
1 Rois 12.26-12.27 1 Samuel 21.7 Amos 8.5 Psaumes 66.3 2 Corinthiens 9.7
13 Naye Samweli akamwambia Sauli, Umefanya upumbavu; hukuishika amri ya Bwana, Mungu wako, aliyokuamuru; kwa maana Bwana angaliufanya ufalme wako kuwa imara juu ya Israeli milele.
2 Chroniques 16.9 1 Samuel 15.22 1 Samuel 15.11 1 Samuel 15.28 Psaumes 50.8-50.15
14 Lakini sasa ufalme wako hautadumu; Bwana amejitafutia mtu aupendezaye moyo wake, naye Bwana amemwamuru yeye kuwa mkuu juu ya watu wake, kwa sababu wewe hukulishika neno lile Bwana alilokuamuru.
Actes 13.22 1 Samuel 15.28 1 Samuel 2.30 Actes 7.46 2 Samuel 5.2
15 Basi Samweli akaondoka, akapanda kutoka Gilgali mpaka Gibea ya Benyamini. Naye Sauli akawahesabu watu waliokuwapo pamoja naye, wapata kama mia sita.
1 Samuel 13.2 1 Samuel 14.2 1 Samuel 13.6-13.7
16 Naye Sauli, na mwanawe Yonathani, na watu waliokuwapo pamoja nao, wakakaa huko Geba ya Benyamini; lakini Wafilisti wakatua katika Mikmashi.
1 Samuel 13.3
17 Nao watekaji wa nyara wakatoka katika marago ya hao Wafilisti, vikosi vitatu; kikosi kimoja kikageukia njia iendayo Ofra, mpaka nchi ya Shuali;
Josué 18.23 1 Samuel 14.15 1 Samuel 11.11 Josué 19.3
18 na kikosi kingine kikageukia njia iendayo Beth-horoni; na kikosi kingine kikageukia njia ya mpakani ielekeayo bonde la Seboimu upande wa nyika.
Néhémie 11.34 Josué 18.13-18.14 Josué 16.3 1 Chroniques 6.68 Osée 11.8
19 Basi, hakuonekana mhunzi ye yote katika nchi yote ya Israeli; kwa kuwa Wafilisti walisema, Waebrania wasije wakajifanyizia panga au mikuki;
2 Rois 24.14 Juges 5.8 Jérémie 24.1 Esaïe 54.16
20 lakini Waisraeli wote hushuka kwa Wafilisti, ili kunoa kila mtu jembe lake, na mundu wake, na shoka lake, na sululu yake;
21 ila walikuwa na tupa za kunolea sululu, na miundu, na mauma, na mashoka; na kwa kuinoa michokoo.
22 Hivyo ikawa, siku ya vita, haukuonekana mkononi mwa mtu ye yote, miongoni mwa watu waliokuwa pamoja na Sauli na Yonathani, upanga wala mkuki; isipokuwa Sauli mwenyewe na mwanawe Yonathani walikuwa navyo.
Juges 5.8 2 Corinthiens 4.7 Zacharie 4.6 1 Samuel 17.47 1 Corinthiens 1.27-1.29
23 Na jeshi la Wafilisti wakatoka hata mwanya wa Mikmashi.
Esaïe 10.28 1 Samuel 14.1 1 Samuel 14.4-14.5 1 Samuel 13.5 1 Samuel 13.2-13.3

Cette Bible est dans le domaine public.