Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Apocalypse 16.8
Bible en Swahili de l’est


Sept coupes

Les sept coupes versées

1 Nikasikia sauti kuu kutoka hekaluni, ikiwaambia wale malaika saba, Enendeni, mkavimimine vile vitasa saba vya ghadhabu ya Mungu juu ya nchi.
Apocalypse 15.1 Apocalypse 16.17 Sophonie 3.8 Jérémie 10.25 Apocalypse 16.2-16.12
2 Akaenda huyo wa kwanza, akakimimina kitasa chake juu ya nchi; pakawa na jipu baya, bovu, juu ya wale watu wenye chapa ya huyo mnyama, na wale wenye kuisujudia sanamu yake.
Apocalypse 8.7 Apocalypse 16.11 Apocalypse 13.15-13.18 Deutéronome 7.15 Exode 9.8-9.11
3 Na huyo wa pili akakimimina kitasa chake juu ya bahari, ikawa damu kama damu ya mfu, na vitu vyote vyenye roho ya uhai katika bahari vikafa.
Exode 7.17-7.21 Apocalypse 8.8-8.9 Apocalypse 11.6 Apocalypse 10.2 Apocalypse 13.1
4 Na huyo wa tatu akakimimina kitasa chake juu ya mito na chemchemi za maji; zikawa damu.
Apocalypse 8.10-8.11 Exode 7.17-7.20 Apocalypse 14.7 Apocalypse 16.5 Esaïe 50.2
5 Nami nikamsikia malaika wa maji akisema, Wewe u mwenye haki, uliyeko na uliyekuwako, Mtakatifu, kwa kuwa umehukumu hivi;
Apocalypse 11.17 Apocalypse 1.4 Apocalypse 4.8 Apocalypse 15.3-15.4 Apocalypse 1.8
6 kwa kuwa walimwaga damu ya watakatifu na ya manabii, nawe umewapa damu wainywe; nao wamestahili.
Esaïe 49.26 Apocalypse 11.18 Apocalypse 6.10-6.11 Apocalypse 18.24 Luc 11.49-11.50
7 Nikaisikia hiyo madhabahu ikisema, Naam, Bwana Mungu Mwenyezi, ni za kweli, na za haki, hukumu zako.
Apocalypse 19.2 Apocalypse 6.9 Apocalypse 14.18 Apocalypse 15.3-15.4 Ezéchiel 10.7
8 Na huyo wa nne akakimimina kitasa chake juu ya jua, nalo likapewa kuwaunguza wanadamu kwa moto.
Apocalypse 14.18 Apocalypse 8.12 Apocalypse 6.12 Actes 2.20 Esaïe 24.23
9 Wanadamu wakaunguzwa maunguzo makubwa, nao wakalitukana jina la Mungu aliye na mamlaka juu ya mapigo hayo; wala hawakutubu wala kumpa utukufu.
Apocalypse 11.13 Apocalypse 16.21 Apocalypse 2.21 Daniel 5.22-5.23 Apocalypse 16.10-16.11
10 Na huyo wa tano akakimimina kitasa chake juu ya kiti cha enzi cha yule mnyama; ufalme wake ukatiwa giza; wakatafuna ndimi zao kwa sababu ya maumivu,
Apocalypse 9.2 Esaïe 8.21-8.22 Apocalypse 11.10 Matthieu 8.12 Matthieu 22.13
11 wakamtukana Mungu wa mbingu kwa sababu ya maumivu yao, na kwa sababu ya majipu yao; wala hawakuyatubia matendo yao.
Apocalypse 16.9 Apocalypse 16.2 Apocalypse 11.13 Apocalypse 16.21 Apocalypse 2.21
12 Na huyo wa sita akakimimina kitasa chake juu ya mto ule mkubwa Frati; maji yake yakakauka, ili njia itengenezwe kwa wafalme watokao katika maawio ya jua.
Apocalypse 9.14 Esaïe 11.15 Esaïe 41.25 Jérémie 51.36 Esaïe 44.27
13 Nikaona roho tatu za uchafu zilizofanana na vyura, zikitoka katika kinywa cha yule joka, na katika kinywa cha yule mnyama, na katika kinywa cha yule nabii wa uongo.
Apocalypse 19.20 Apocalypse 20.10 1 Timothée 4.1-4.3 Apocalypse 13.1-13.7 Apocalypse 12.3-12.4
14 Hizo ndizo roho za mashetani, zifanyazo ishara, zitokazo na kuwaendea wafalme wa ulimwengu wote kuwakusanya kwa vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi.
1 Timothée 4.1 Apocalypse 12.9 Apocalypse 17.14 Apocalypse 20.8 Apocalypse 19.19-19.20
15 (Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake.)
Matthieu 24.42-24.43 Apocalypse 3.18 Apocalypse 3.3-3.4 1 Thessaloniciens 5.2-5.3 Osée 2.3
16 Wakawakusanya hata mahali paitwapo kwa Kiebrania, Har-Magedoni.
Zacharie 12.11 Apocalypse 9.11 Juges 5.19 2 Rois 23.29-23.30 Apocalypse 17.14
17 Na huyo wa saba akakimimina kitasa chake juu ya anga. Sauti kuu ikatoka katika hekalu, katika kile kiti cha enzi, ikisema, Imekwisha kuwa.
Apocalypse 21.6 Ephésiens 2.2 Jean 19.30 Apocalypse 14.15 Daniel 12.7-12.13
18 Pakawa na umeme na sauti na radi; na palikuwa na tetemeko la nchi kubwa, ambalo tangu wanadamu kuwako juu ya nchi hapakuwa namna ile, jinsi lilivyokuwa kubwa tetemeko hilo.
Apocalypse 4.5 Daniel 12.1 Apocalypse 11.13 Apocalypse 6.12 Apocalypse 11.19
19 Na mji ule mkuu ukagawanyikana mafungu matatu, na miji ya mataifa ikaanguka; na Babeli ule mkuu ukakumbukwa mbele za Mungu, kupewa kikombe cha mvinyo ya ghadhabu ya hasira yake.
Apocalypse 18.5 Apocalypse 17.18 Apocalypse 18.21 Apocalypse 18.10 Esaïe 49.26
20 Kila kisiwa kikakimbia, wala milima haikuonekana tena.
Apocalypse 6.14 Apocalypse 20.11 Esaïe 2.14-2.17 Jérémie 4.23-4.25
21 Na mvua ya mawe kubwa sana, ya mawe mazito kama talanta, ikashuka kutoka mbinguni juu ya wanadamu. Wanadamu wakamtukana Mungu kwa sababu ya lile pigo la mvua ya mawe; kwa maana pigo lake ni kubwa mno.
Apocalypse 11.19 Apocalypse 16.11 Apocalypse 16.9 Apocalypse 8.7 Josué 10.11

Cette Bible est dans le domaine public.