Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Apocalypse 14.9
Bible en Swahili de l’est


L’Agneau et les rachetés

1 Kisha nikaona, na tazama, huyo Mwana-Kondoo amesimama juu ya mlima Sayuni, na watu mia na arobaini na nne elfu pamoja naye, wenye jina lake na jina la Baba yake limeandikwa katika vipaji vya nyuso zao.
Apocalypse 3.12 Psaumes 2.6 Apocalypse 7.3-7.17 Joël 2.32 Hébreux 12.22-12.24
2 Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni, kama sauti ya maji mengi, na kama sauti ya radi kuu. Na hiyo sauti niliyoisikia ilikuwa kama sauti ya wapiga vinubi, wakivipiga vinubi vyao;
Apocalypse 5.8 Apocalypse 1.15 Apocalypse 11.15 Apocalypse 15.2 Psaumes 33.2
3 na kuimba wimbo mpya mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele ya wale wenye uhai wanne, na wale wazee; wala hapana mtu aliyeweza kujifunza wimbo ule, ila wale mia na arobaini na nne elfu, walionunuliwa katika nchi.
Apocalypse 5.9 Apocalypse 2.17 Apocalypse 14.1 Esaïe 42.10 Psaumes 149.1
4 Hawa ndio wasiotiwa unajisi pamoja na wanawake, kwa maana ni bikira. Hawa ndio wamfuatao Mwana-Kondoo kila aendako. Hawa wamenunuliwa katika wanadamu, malimbuko kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo.
2 Corinthiens 11.2 Jacques 1.18 Apocalypse 3.4 Apocalypse 5.9 Jean 12.26
5 Na katika vinywa vyao haukuonekana uongo. Maana hawana mawaa.
Psaumes 32.2 Sophonie 3.13 Jude 1.24 Ephésiens 5.27 Jean 1.47

Les trois anges proclamant le jugement

6 Kisha nikaona malaika mwingine, akiruka katikati ya mbingu, mwenye Injili ya milele, awahubiri hao wakaao juu ya nchi, na kila taifa na kabila na lugha na jamaa,
Apocalypse 8.13 Apocalypse 3.10 Apocalypse 13.7 Matthieu 10.27 Apocalypse 10.11
7 akasema kwa sauti kuu, Mcheni Mungu, na kumtukuza, kwa maana saa ya hukumu yake imekuja. Msujudieni yeye aliyezifanya mbingu na nchi na bahari na chemchemi za maji.
Apocalypse 15.4 Apocalypse 4.11 Néhémie 9.6 Apocalypse 11.18 Exode 20.11
8 Kisha mwingine, malaika wa pili, akafuata, akisema, Umeanguka, umeanguka Babeli, mji ule ulio mkubwa, maana ndio uliowanywesha mataifa yote mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake.
Esaïe 21.9 Apocalypse 18.2-18.3 Jérémie 51.7-51.8 Apocalypse 16.19 Apocalypse 11.8
9 Na mwingine, malaika wa tatu, akawafuata, akisema kwa sauti kuu, Mtu awaye yote akimsujudu huyo mnyama na sanamu yake, na kuipokea chapa katika kipaji cha uso wake, au katika mkono wake,
Apocalypse 14.11 Apocalypse 14.6-14.8 Apocalypse 13.11-13.17 Jérémie 44.4 Apocalypse 13.3-13.6
10 yeye naye atakunywa katika mvinyo ya ghadhabu ya Mungu iliyotengenezwa, pasipo kuchanganywa na maji, katika kikombe cha hasira yake; naye atateswa kwa moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu, na mbele za Mwana-Kondoo.
Esaïe 51.17 Apocalypse 20.10 Apocalypse 19.20 Apocalypse 16.19 Psaumes 11.6
11 Na moshi wa maumivu yao hupanda juu hata milele na milele, wala hawana raha mchana wala usiku, hao wamsujuduo huyo mnyama na sanamu yake, na kila aipokeaye chapa ya jina lake.
Esaïe 34.10 Apocalypse 19.3 Apocalypse 18.18 Matthieu 25.41 Apocalypse 20.10
12 Hapa ndipo penye subira ya watakatifu, hao wazishikao amri za Mungu, na imani ya Yesu.
Apocalypse 13.10 Apocalypse 12.17 Apocalypse 3.8 2 Timothée 4.7 Apocalypse 3.10
13 Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao.
1 Corinthiens 15.18 Apocalypse 20.6 1 Thessaloniciens 4.16 Hébreux 4.9-4.11 Apocalypse 6.11

La moisson et la vendange

14 Kisha nikaona, na tazama, wingu jeupe, na juu ya wingu hilo ameketi mmoja, mfano wa Mwanadamu, mwenye taji ya dhahabu juu ya kichwa chake, na katika mkono wake mundu mkali.
Apocalypse 1.13 Daniel 7.13 Apocalypse 6.2 Matthieu 17.5 Psaumes 21.3
15 Na malaika mwingine akatoka katika hekalu, akimlilia kwa sauti kuu yeye aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu, Tia mundu wako, ukavune; kwa kuwa saa ya kuvuna imekuja; kwa kuwa mavuno ya nchi yamekomaa.
Joël 3.13 Apocalypse 14.18 Jérémie 51.33 Matthieu 13.39 Marc 4.29
16 Na yeye aliyeketi juu ya wingu akautupa mundu wake juu ya nchi, nchi ikavunwa.
Matthieu 16.27 Apocalypse 16.1-16.21 Apocalypse 14.14 Jean 5.22-5.23 Apocalypse 14.19
17 Kisha malaika mwingine akatoka katika lile hekalu lililoko mbinguni, yeye naye ana mundu mkali.
Apocalypse 14.14-14.15 Apocalypse 16.1 Apocalypse 14.18 Apocalypse 15.5-15.6
18 Na malaika mwingine akatoka katika ile madhabahu, yule mwenye mamlaka juu ya moto; naye akamlilia kwa sauti kuu yule mwenye mundu ule mkali, akisema, Tia mundu wako mkali, ukachume vichala vya mzabibu wa nchi, maana zabibu zake zimeiva sana.
Joël 3.13 Apocalypse 16.8 Apocalypse 6.9-6.10 Apocalypse 14.15-14.16
19 Malaika yule akautupa mundu wake hata nchi, akauchuma mzabibu wa nchi, akazitupa zabibu katika shinikizo hilo kubwa la ghadhabu ya Mungu.
Deutéronome 32.32-32.33 Apocalypse 19.15-19.21
20 Shinikizo lile likakanyagwa nje ya mji, damu ikatoka katika shinikizo mpaka kwenye hatamu za farasi, kama mwendo wa maili mia mbili.
Apocalypse 11.8 Lamentations 1.15 Esaïe 63.1-63.3 Esaïe 66.24 Esaïe 34.5-34.7

Cette Bible est dans le domaine public.