Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Josué 21.20
Bible en Swahili de l’est


Désignation des 48 villes des Lévites

1 Wakati huo hao vichwa vya nyumba za mababa ya Walawi wakamwendea Eleazari, kuhani, na Yoshua, mwana wa Nuni, na hao waliokuwa vichwa vya nyumba za mababa ya kabila za wana wa Israeli;
Josué 14.1 Josué 19.51 Josué 17.4 Nombres 34.17-34.29 Exode 6.14
2 wakanena nao hapo Shilo katika nchi ya Kanaani, wakisema, Yeye Bwana aliamuru kwa mkono wa Musa kwamba sisi tupewe miji tupate kukaa humo, pamoja na malisho yake kwa ajili ya wanyama wetu wa mifugo.
Josué 18.1 Nombres 35.2-35.8 1 Timothée 5.17-5.18 Ezéchiel 48.9-48.18 Matthieu 10.10
3 Basi wana wa Israeli wakawapa Walawi miji hii, pamoja na malisho yake, katika urithi wao, sawasawa na hiyo amri ya Bwana.
Deutéronome 33.8-33.10 Genèse 49.7 1 Chroniques 6.54-6.81
4 Kura ikatokea kwa ajili ya jamaa za Wakohathi; na wana wa Haruni kuhani, waliokuwa katika Walawi, walipata miji kumi na mitatu kwa kura katika kabila ya Yuda, na katika kabila ya Simeoni, na katika kabila ya Benyamini.
1 Chroniques 6.54-6.60 Josué 24.33 Josué 21.8-21.19
5 Kisha Wakohathi wengine waliosalia walipata kwa kura katika jamaa za kabila ya Efraimu, na katika kabila ya Dani, na katika hiyo nusu ya kabila ya Manase, miji kumi.
Josué 21.20-21.26 Nombres 3.27 Genèse 46.11 1 Chroniques 6.61 1 Chroniques 6.66-6.70
6 Tena wana wa Gershoni walipata kwa kura katika jamaa za kabila ya Isakari, na katika kabila ya Asheri, na katika kabila ya Naftali, na katika hiyo nusu ya kabila ya Manase huko Bashani, miji kumi na mitatu.
Josué 21.27-21.33 Nombres 3.21-3.22 Exode 6.16-6.17 1 Chroniques 6.71-6.76 1 Chroniques 6.62
7 Na wana wa Merari kwa kuandama jamaa zao walipata katika kabila ya Reubeni, na katika kabila ya Gadi, na katika kabila ya Zabuloni, miji kumi na miwili.
Josué 21.34-21.40 Nombres 3.20 1 Chroniques 6.63 Exode 6.19 1 Chroniques 6.77-6.81
8 Kisha wana wa Israeli waliwapa Walawi kwa kura miji hiyo pamoja na malisho yake, kama Bwana alivyoamuru kwa mkono wa Musa.
Josué 21.3 Nombres 35.3 Nombres 32.2 Proverbes 18.18 Proverbes 16.33
9 Kisha wakawapa katika kabila ya wana wa Yuda, na katika kabila ya wana wa Simeoni, miji hii iliyotajwa hapa kwa majina;
1 Chroniques 6.65 Josué 21.13-21.18
10 nayo ilikuwa kwa ajili ya wana wa Haruni, wa jamaa ya Wakohathi, waliokuwa wa wana wa Lawi; kwa kuwa kura ya kwanza ilikuwa ni yao.
Josué 21.4 Nombres 3.27 Exode 6.18 Nombres 4.2 Exode 6.20-6.26
11 Nao wakawapa Kiriath-arba, huyo Arba alikuwa baba yake Anaki, (ndio Hebroni), katika nchi ya vilima ya Yuda, pamoja na malisho yake yaliyouzunguka pande zote.
1 Chroniques 6.55 Luc 1.39 Josué 15.54 Juges 1.10 Genèse 35.27
12 Lakini mashamba ya mji, na vile vijiji vyake, wakampa Kalebu mwana wa Yefune kuwa milki yake.
Josué 14.13-14.15 1 Chroniques 6.55-6.57
13 Kisha wakawapa wana wa Haruni kuhani Hebroni pamoja na malisho yake, huo mji wa kukimbilia kwa ajili ya mwuaji, na Libna pamoja na malisho yake;
Josué 15.42 Josué 20.7 Josué 10.29 Josué 15.54 1 Chroniques 6.56-6.57
14 na Yatiri pamoja na malisho yake, na Eshtemoa pamoja na malisho yake;
Josué 15.50 Josué 15.48 1 Samuel 30.27-30.28
15 na Holoni pamoja na malisho yake, na Debiri pamoja na malisho yake;
Josué 15.51 Josué 15.49 Josué 12.13 1 Chroniques 6.58
16 na Aini pamoja na malisho yake, na Yuta pamoja na malisho yake, na Bethshemeshi pamoja na malisho yake; miji kenda katika kabila hizo mbili.
1 Chroniques 6.59 Josué 15.55 Josué 15.10 1 Samuel 6.12 Josué 15.42
17 Tena katika kabila ya Benyamini, Gibeoni pamoja na malisho yake, na Geba pamoja na malisho yake;
Josué 9.3 Josué 18.24-18.25 1 Chroniques 6.60
18 na Anathothi pamoja na malisho yake, na Almoni pamoja na malisho yake; miji minne.
Esaïe 10.30 Jérémie 1.1 1 Chroniques 6.60 1 Rois 2.26
19 Miji yote ya wana wa Haruni, makuhani, ilikuwa ni miji kumi na mitatu, pamoja na malisho yake.
20 Na jamaa za wana wa Kohathi, Walawi, hao wana wengine wa Kohathi waliosalia, wao walikuwa na miji ya kura yao katika kabila ya Efraimu.
1 Chroniques 6.66 Josué 21.5
21 Nao wakawapa Shekemu pamoja na malisho yake, katika nchi ya vilima ya Efraimu, huo mji wa makimbilio kwa ajili ya mwuaji; na Gezeri pamoja na malisho yake;
Josué 20.7 1 Chroniques 6.67 1 Rois 12.1 Josué 16.10 Juges 9.1
22 na Kibisaumu pamoja na malisho yake, na Beth-horoni pamoja na malisho yake, miji minne.
Josué 16.5 Josué 18.13-18.14 1 Chroniques 6.68 Josué 16.3
23 Tena katika kabila ya Dani Elteke pamoja na malisho yake, na Gibethoni pamoja na malisho yake;
Josué 19.44-19.45
24 na Aiyaloni pamoja na malisho yake, na Gath-rimoni pamoja na malisho yake; miji minne.
1 Chroniques 6.69 Josué 10.12 Josué 19.42
25 Tena katika hiyo nusu ya kabila ya Manase, Taanaki pamoja na malisho yake, na Gath-rimoni pamoja na malisho yake; miji miwili.
Juges 5.19 Josué 17.11
26 Miji yote ya jamaa za wana wa Kohathi waliosalia ilikuwa ni miji kumi, pamoja na malisho yake.
27 Tena wana wa Gershoni, katika jamaa za Walawi, waliwapa, katika hiyo nusu ya kabila ya Manase, Golani katika Bashani pamoja na malisho yake, huo mji wa makimbilio kwa ajili ya mwuaji; na Beeshtera pamoja na malisho yake; miji miwili.
1 Chroniques 6.71 Deutéronome 1.4 Deutéronome 4.43 Josué 20.8
28 Tena katika kabila ya Isakari, Kishioni pamoja na malisho yake, na Daberathi pamoja na malisho yake;
1 Chroniques 6.72-6.73 Josué 19.12
29 na Yarmuthi pamoja na malisho yake, na Enganimu pamoja na malisho yake; miji minne.
Josué 12.11 Josué 10.3 Josué 10.23
30 Tena katika kabila ya Asheri, Mishali pamoja na malisho yake, na Abdoni pamoja na malisho yake;
Josué 19.25-19.28 1 Chroniques 6.74-6.75
31 na Helkathi pamoja na malisho yake, na Rehobu pamoja na malisho yake; miji minne.
1 Chroniques 6.75 Juges 18.21 Juges 1.31
32 Tena katika kabila ya Naftali, Kedeshi katika Galilaya pamoja na malisho yake, huo mji wa makimbilio kwa ajili ya mwuaji, na Hamoth-dori pamoja na malisho yake, na Kartani pamoja na malisho yake; miji mitatu.
1 Chroniques 6.76 Josué 20.7 Josué 19.37 Josué 19.35
33 Miji yote ya Wagershoni kwa kuandama jamaa zao ilikuwa ni miji kumi na mitatu, pamoja na malisho yake.
34 Tena jamaa za wana wa Merari, hao Walawi waliosalia, katika kabila ya Zabuloni, Yokneamu pamoja na malisho yake, na Karta pamoja na malisho yake,
1 Chroniques 6.77 Josué 19.11 Josué 19.15 Josué 21.7 Josué 12.22
35 na Dimna pamoja na malisho yake, na Nahalali pamoja na malisho yake; miji minne.
36 Tena katika kabila ya Reubeni, Bezeri pamoja na malisho yake, na Yahasa pamoja na malisho yake,
Josué 20.8 Deutéronome 4.43 Nombres 21.23 Josué 13.18 1 Chroniques 6.78-6.79
37 na Kedemothi pamoja na malisho yake, na Mefaathi pamoja na malisho yake; miji minne.
38 Tena katika kabila ya Gadi Ramothi katika Gileadi pamoja na malisho yake, huo mji wa makimbilio kwa ajili ya mwuaji, na Mahanaimu pamoja na malisho yake;
Genèse 32.2 1 Rois 22.3 2 Samuel 17.24 2 Samuel 19.32 1 Chroniques 6.80
39 na Heshboni pamoja na malisho yake, na Yazeri pamoja na malisho yake; jumla yake miji minne.
1 Chroniques 6.81 Esaïe 16.8-16.9 Nombres 32.1 Josué 13.21 Nombres 32.3
40 Miji hiyo yote ilikuwa ni miji ya wana wa Merari kwa kuandama jamaa zao, ni hizo jamaa za Walawi zilizosalia; na kura yao ilikuwa ni miji kumi na miwili.
41 Miji yote ya Walawi iliyokuwa kati ya milki ya wana wa Israeli ilikuwa ni miji arobaini na minane, pamoja na malisho yake.
Genèse 49.7 Deutéronome 33.10 Nombres 35.1-35.8
42 Miji hiyo kila mmoja ulikuwa pamoja na malisho yake, yaliyouzunguka pande zote; ndivyo ilivyokuwa katika miji hiyo yote.

Les promesses divines accomplies

43 Basi Bwana aliwapa Israeli nchi hiyo yote, ambayo aliapa kwamba atawapa baba zao; nao wakaimiliki, na kukaa mumo.
Exode 23.27-23.31 Genèse 28.4 Genèse 13.15 Deutéronome 34.4 Psaumes 106.42-106.45
44 Kisha Bwana akawapa raha pande zote, sawasawa na hayo yote aliyokuwa amewaapia baba zao; wala katika adui zao wote hakusimama hata mtu mmoja miongoni mwao mbele zao; yeye Bwana akawatia adui zao wote mikononi mwao.
Josué 11.23 Josué 22.4 Josué 1.13 Deutéronome 31.3-31.5 Hébreux 4.9
45 Halikuanguka neno lo lote katika jambo lo lote lililokuwa ni jema ambalo Bwana alikuwa amelinena katika habari ya nyumba ya Israeli; yalitimia mambo yote.
Josué 23.14-23.15 1 Rois 8.56 1 Thessaloniciens 5.24 Hébreux 6.18 Nombres 23.19

Cette Bible est dans le domaine public.