Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Hébreux 4.8
Bible en Swahili de l’est


1 Basi, ikiwa ikaliko ahadi ya kuingia katika raha yake, na tuogope, mmoja wenu asije akaonekana ameikosa.
Hébreux 12.15 Hébreux 4.9 Proverbes 28.14 Hébreux 4.3-4.5 Hébreux 13.7
2 Maana ni kweli, sisi nasi tumehubiriwa habari njema vile vile kama hao. Lakini neno lile lililosikiwa halikuwafaa hao, kwa sababu halikuchanganyika na imani ndani yao waliosikia.
1 Thessaloniciens 2.13 1 Timothée 4.8 Hébreux 4.6 Romains 2.25 1 Thessaloniciens 1.5
3 Maana sisi tulioamini tunaingia katika raha ile; kama vile alivyosema, Kama nilivyoapa kwa hasira yangu, Hawataingia rahani mwangu:
Hébreux 3.11 Matthieu 11.28-11.29 Psaumes 95.11 Exode 20.11 Hébreux 3.14
4 Kwa maana ameinena siku ya saba mahali fulani hivi, Mungu alistarehe siku ya saba, akaziacha kazi zake zote;
Exode 20.11 Exode 31.17 Genèse 2.1-2.2 Hébreux 2.6
5 na hapa napo, Hawataingia rahani mwangu.
Psaumes 95.11 Hébreux 4.3 Hébreux 3.11
6 Basi, kwa kuwa neno hili limebaki kwamba wako watu watakaoingia humo, na wale waliohubiriwa habari ile zamani walikosa kuingia kwa sababu ya kuasi kwao,
Hébreux 3.18-3.19 Actes 13.46-13.47 Galates 3.8 Hébreux 4.9 Nombres 14.12
7 aweka tena siku fulani, akisema katika Daudi baada ya muda mwingi namna hii, Leo; kama ilivyonenwa tangu zamani, Leo,kama mtaisikia sauti yake, Msifanye migumu mioyo yenu.
Psaumes 95.7 Hébreux 3.7-3.8 Hébreux 3.15 1 Rois 6.1 Actes 2.31
8 Maana kama Yoshua angaliwapa raha, asingaliinena siku nyingine baadaye.
Josué 22.4 Josué 1.15 Hébreux 11.13-11.15 Psaumes 78.55 Psaumes 105.44
9 Basi, imesalia raha ya sabato kwa watu wa Mungu.
1 Pierre 2.10 Esaïe 60.19-60.20 Tite 2.14 Apocalypse 7.14-7.17 Apocalypse 21.4
10 Kwa maana yeye aliyeingia katika raha yake amestarehe mwenyewe katika kazi yake, kama vile Mungu alivyostarehe katika kazi zake.
Apocalypse 14.13 Hébreux 4.3-4.4 Hébreux 1.3 Jean 19.30 1 Pierre 4.1-4.2
11 Basi, na tufanye bidii kuingia katika raha ile, ili kwamba mtu ye yote asije akaanguka kwa mfano uo huo wa kuasi.
Hébreux 3.12 Luc 13.24 Tite 3.3 Ephésiens 2.2 Ephésiens 5.6
12 Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.
Jérémie 23.29 Ephésiens 6.17 Esaïe 55.11 Esaïe 49.2 1 Pierre 1.23
13 Wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu.
Psaumes 33.13-33.15 1 Corinthiens 4.5 Proverbes 15.3 Ecclésiaste 12.14 Job 34.21

Supériorité de Christ le grand-prêtre

Christ supérieur aux grands-prêtres lévitiques

14 Basi, iwapo tunaye kuhani mkuu aliyeingia katika mbingu, Yesu, Mwana wa Mungu, na tuyashike sana maungamo yetu.
Hébreux 6.20 Hébreux 12.2 Hébreux 9.24 Ephésiens 4.10 Hébreux 2.17-3.1
15 Kwa kuwa hamna kuhani mkuu asiyeweza kuchukuana nasi katika mambo yetu ya udhaifu; bali yeye alijaribiwa sawasawa na sisi katika mambo yote, bila kufanya dhambi.
2 Corinthiens 5.21 Hébreux 2.17-2.18 1 Jean 3.5 Hébreux 7.26 Jean 8.46
16 Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri, ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.
Ephésiens 3.12 Hébreux 7.25 Hébreux 13.6 Esaïe 55.6-55.7 Philippiens 4.6-4.7

Cette Bible est dans le domaine public.