Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Hébreux 12.21
Bible en Swahili de l’est


Persévérer dans la vie chrétienne

1 Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu,
1 Corinthiens 9.24-9.27 2 Timothée 4.7 Luc 21.34 Philippiens 2.16 Hébreux 10.35-10.39
2 tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu.
Michée 7.7 Hébreux 1.3 Tite 2.13-2.14 Ephésiens 5.2 1 Pierre 3.18
3 Maana mtafakarini sana yeye aliyeyastahimili mapingamizi makuu namna hii ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu.
2 Corinthiens 4.16 Galates 6.9 Jean 15.18-15.24 Apocalypse 2.3 1 Corinthiens 15.58
4 Hamjafanya vita hata kumwagika damu, mkishindana na dhambi;
Hébreux 10.32-10.34 Hébreux 12.2 Matthieu 24.9 Apocalypse 6.9-6.11 2 Timothée 4.6-4.7
5 tena mmeyasahau yale maonyo, yasemayo nanyi kama kusema na wana, Mwanangu, usiyadharau marudia ya Bwana, Wala usizimie moyo ukikemewa naye;
Proverbes 3.11-3.12 Job 5.17-5.18 Deutéronome 4.9-4.10 Apocalypse 3.19 1 Corinthiens 11.32
6 Maana yeye ambaye Bwana ampenda, humrudi, Naye humpiga kila mwana amkubaliye.
Apocalypse 3.19 Psaumes 119.75 Proverbes 3.12 Psaumes 32.1-32.5 2 Samuel 7.14
7 Ni kwa ajili ya kurudiwa mwastahimili; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana yupi asiyerudiwa na babaye?
Proverbes 19.18 Proverbes 29.15 Proverbes 13.24 Deutéronome 8.5 Proverbes 23.13-23.14
8 Basi kama mkiwa hamna kurudiwa, ambako ni fungu la wote, ndipo mmekuwa wana wa haramu ninyi, wala si wana wa halali.
Hébreux 12.6 1 Pierre 5.9-5.10 Psaumes 73.14-73.15 Psaumes 73.1
9 Na pamoja na hayo tulikuwa na baba zetu wa mwili walioturudi, nasi tukawastahi; basi si afadhali sana kujitia chini ya Baba wa roho zetu na kuishi?
Nombres 16.22 Lévitique 19.3 Exode 20.12 Deutéronome 21.18-21.21 Proverbes 30.17
10 Maana ni hakika, hao kwa siku chache waliturudi kama walivyoona vema wenyewe; bali yeye kwa faida yetu, ili tuushiriki utakatifu wake.
2 Pierre 1.4 Lévitique 19.2 Ephésiens 5.26-5.27 Lévitique 11.44-11.45 Psaumes 17.15
11 Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani.
Jacques 3.17-3.18 Esaïe 32.17 Psaumes 119.165 Psaumes 118.18 Proverbes 19.18
12 Kwa hiyo inyosheni mikono iliyolegea na magoti yaliyopooza,
Esaïe 35.3 Hébreux 12.3 Job 4.3-4.4 1 Thessaloniciens 5.14 Hébreux 12.5
13 mkaifanyie miguu yenu njia za kunyoka, ili kitu kilicho kiwete kisipotoshwe, bali afadhali kiponywe.
Galates 6.1 Proverbes 4.26-4.27 Esaïe 35.6 Luc 3.5 Esaïe 40.3-40.4
14 Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;
2 Corinthiens 7.1 1 Pierre 1.15-1.16 1 Thessaloniciens 4.7 3 Jean 1.11 Romains 14.19
15 mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo.
Galates 5.4 Hébreux 3.12 Deutéronome 29.18 2 Corinthiens 6.1 1 Corinthiens 15.33
16 Asiwepo mwasherati wala asiyemcha Mungu, kama Esau, aliyeuuza urithi wake wa mzaliwa wa kwanza kwa ajili ya chakula kimoja.
Hébreux 13.4 Genèse 25.31-25.34 Actes 15.29 Genèse 27.36 1 Thessaloniciens 4.3-4.7
17 Maana mwajua ya kuwa hata alipotaka baadaye kuirithi baraka, alikataliwa (maana hakuona nafasi ya kutubu), ijapokuwa aliitafuta sana kwa machozi.
Luc 13.24-13.27 Matthieu 7.23 Jérémie 6.30 Hébreux 6.4-6.6 Matthieu 25.11-25.12
18 Maana hamkufikilia mlima uwezao kuguswa, uliowaka moto, wala wingu jeusi, na giza, na tufani,
Deutéronome 4.11 Exode 20.18 Exode 19.12-19.22 Exode 24.17 Romains 6.14
19 na mlio wa baragumu na sauti ya maneno; ambayo wale walioisikia walisihi wasiambiwe neno lo lote lingine;
Deutéronome 18.16 Deutéronome 4.12 Deutéronome 5.24-5.27 Exode 20.22 1 Corinthiens 15.52
20 maana hawakuweza kustahimili neno lile lililoamriwa, Hata mnyama akiugusa huo mlima atapigwa kwa mawe.
Exode 19.12-19.13 Deutéronome 33.2 Galates 3.10 Romains 3.19-3.20 Galates 2.19
21 Na hayo yaliyoonekana jinsi yalivyokuwa ya kutisha, hata Musa akasema, Nimeshikwa na hofu na kutetemeka.
Exode 19.16 Psaumes 119.120 Esaïe 6.3-6.5 Daniel 10.17 Deutéronome 9.19
22 Bali ninyi mmeufikilia mlima Sayuni, na mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni, na majeshi ya malaika elfu nyingi,
Galates 4.26 Philippiens 3.20 Psaumes 48.2 Apocalypse 14.1 Apocalypse 21.2
23 mkutano mkuu na kanisa la wazaliwa wa kwanza walioandikwa mbinguni, na Mungu mwamuzi wa watu wote, na roho za watu wenye haki waliokamilika,
Exode 4.22 Luc 10.20 Genèse 18.25 Psaumes 94.2 Hébreux 11.40
24 na Yesu mjumbe wa agano jipya, na damu ya kunyunyizwa, inenayo mema kuliko ile ya Habili.
Genèse 4.10 Hébreux 11.4 Hébreux 10.22 Hébreux 9.15 Hébreux 8.6
25 Angalieni msimkatae yeye anenaye. Maana ikiwa hawakuokoka wale waliomkataa yeye aliyewaonya juu ya nchi, zaidi sana hatutaokoka sisi tukijiepusha na yeye atuonyaye kutoka mbinguni;
Hébreux 8.5 Hébreux 11.7 Zacharie 7.11 Ezéchiel 5.6 Proverbes 13.18
26 ambaye sauti yake iliitetemesha nchi wakati ule; lakini sasa ameahidi akisema, Mara moja tena nitatetemesha si nchi tu, bali na mbingu pia.
Exode 19.18 Hébreux 12.27 Aggée 2.22 Habakuk 3.10 Esaïe 13.13
27 Lakini neno lile, Mara moja tena, ladhihirisha kuhamishwa vile viwezavyo kutetemeshwa, kama vitu vilivyoumbwa, vitu visivyoweza kutetemeshwa vikae.
1 Corinthiens 7.31 Ezéchiel 21.27 Apocalypse 21.1 2 Pierre 3.10-3.11 Matthieu 24.35
28 Basi kwa kuwa tunapokea ufalme usioweza kutetemeshwa, na mwe na neema, ambayo kwa hiyo tumtolee Mungu ibada ya kumpendeza, pamoja na unyenyekevu na kicho;
Daniel 2.44 Esaïe 56.7 Hébreux 5.7 Hébreux 13.15 1 Pierre 1.4-1.5
29 maana Mungu wetu ni moto ulao.
Deutéronome 4.24 Deutéronome 9.3 Hébreux 10.27 Daniel 7.9 Nombres 11.1

Cette Bible est dans le domaine public.