Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Timothée 3.16
Bible en Swahili de l’est


Qualifications des responsables de l’Église

1 Ni neno la kuaminiwa; mtu akitaka kazi ya askofu, atamani kazi njema.
Actes 20.28 1 Pierre 5.2 1 Timothée 1.15 Tite 1.7 1 Pierre 2.25
2 Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha;
2 Timothée 2.24 Romains 12.13 Tite 1.6-1.9 1 Pierre 4.9 1 Timothée 5.9
3 si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu wa kujadiliana, wala asiwe mwenye kupenda fedha;
Tite 1.7 1 Timothée 3.8 Jacques 4.1 Tite 3.2 Esaïe 28.7
4 mwenye kuisimamia nyumba yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu;
1 Timothée 3.12 Tite 1.6 Genèse 18.19 Actes 10.2 Psaumes 101.2-101.8
5 (yaani, mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?)
1 Timothée 3.15 1 Samuel 3.13 Ephésiens 5.24 Actes 20.28 Ephésiens 1.22
6 Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi.
1 Timothée 6.4 Proverbes 18.12 1 Corinthiens 4.6-4.8 Proverbes 29.23 Luc 10.18
7 Tena imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje; ili asianguke katika lawama na mtego wa Ibilisi.
2 Timothée 2.26 2 Corinthiens 8.21 1 Corinthiens 10.32 1 Timothée 6.9 1 Thessaloniciens 4.12
8 Vivyo hivyo mashemasi na wawe wastahivu; si wenye kauli mbili, si watu wa kutumia mvinyo sana,si watu wanaotamani fedha ya aibu.
Philippiens 1.1 Tite 2.3 1 Timothée 3.3 Psaumes 12.2 Lévitique 10.9
9 wakiishika siri ya imani katika dhamiri safi.
1 Timothée 1.19 1 Timothée 1.5 2 Jean 1.9-1.10 1 Timothée 3.16
10 Hawa pia na wajaribiwe kwanza; baadaye waitende kazi ya shemasi, wakiisha kuonekana kuwa hawana hatia.
1 Timothée 5.22 1 Jean 4.1 Tite 1.6-1.7 1 Timothée 3.2 1 Timothée 3.6
11 Vivyo hivyo wake zao na wawe wastahivu; si wasingiziaji; watu wa kiasi, waaminifu katika mambo yote.
Tite 2.3 1 Timothée 3.2 2 Timothée 3.3 Lévitique 21.7 Jérémie 9.4
12 Mashemasi na wawe waume wa mke mmoja, wakiwasimamia watoto wao vizuri, na nyumba zao.
1 Timothée 3.2 Philippiens 1.1 1 Timothée 3.8 1 Timothée 3.4-3.5
13 Kwa maana watendao vema kazi ya shemasi hujipatia daraja nzuri, na ujasiri mwingi katika imani iliyo katika Kristo Yesu.
Matthieu 25.21 2 Timothée 2.1 Actes 6.15-7.53 Actes 6.8 Philippiens 1.14
14 Nakuandikia hayo nikitaraji kuja kwako hivi karibu.
2 Jean 1.12 1 Corinthiens 16.5-16.7 3 Jean 1.14 Philémon 1.22 1 Timothée 4.13
15 Lakini nikikawia, upate kujua jinsi iwapasavyo watu kuenenda katika nyumba ya Mungu, iliyo kanisa la Mungu aliye hai, nguzo na msingi wa kweli.
1 Pierre 2.5 1 Timothée 4.10 Matthieu 16.16 Matthieu 18.18 Galates 2.9
16 Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu.
Jean 1.14 Hébreux 1.3 Colossiens 1.23 Romains 16.25 Luc 24.4

Cette Bible est dans le domaine public.