Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Philippiens 1.16
Bible en Swahili de l’est


Salutation et louange

1 Paulo na Timotheo, watumwa wa Kristo Yesu, kwa watakatifu wote katika Kristo Yesu, walioko Filipi, pamoja na maaskofu na mashemasi.
2 Corinthiens 1.1 1 Timothée 3.8 Actes 20.28 Tite 1.7 1 Timothée 3.1-3.2
2 Neema na iwe kwenu na amani zitokazo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
Romains 1.7 2 Corinthiens 1.2 1 Pierre 1.2
3 Namshukuru Mungu wangu kila niwakumbukapo,
1 Corinthiens 1.4 2 Timothée 1.3 2 Thessaloniciens 1.3 Romains 1.8-1.9 Ephésiens 1.15-1.16
4 sikuzote kila niwaombeapo ninyi nyote nikisema sala zangu kwa furaha,
Romains 1.9 Luc 15.7 Luc 15.10 Philippiens 4.1 1 Thessaloniciens 1.2
5 kwa sababu ya ushirika wenu katika kuieneza Injili, tangu siku ile ya kwanza hata leo hivi.
Actes 16.12-16.40 Philippiens 1.7 Philippiens 4.14-4.15 Philémon 1.17 1 Jean 1.7
6 Nami niliaminilo ndilo hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu;
1 Thessaloniciens 5.23-5.24 Philippiens 2.13 Ephésiens 4.12 Hébreux 13.20-13.21 Romains 8.28-8.30
7 vile vile kama ilivyo wajibu wangu kufikiri haya juu yenu nyote; kwa sababu ninyi mmo moyoni mwangu; kwa kuwa katika kufungwa kwangu na katika kazi ya kutetea Injili na kuithibitisha, ninyi nyote mmeshirikiana nami neema hii.
2 Corinthiens 7.3 2 Timothée 2.9 Philippiens 1.5 Ephésiens 3.1 Ephésiens 6.20
8 Maana Mungu ni shahidi wangu, jinsi ninavyowaonea shauku ninyi nyote katika moyo wake Kristo Yesu.
Romains 1.9 2 Timothée 1.4 Romains 9.1 Philippiens 4.1 1 Thessaloniciens 2.5
9 Na hii ndiyo dua yangu, kwamba pendo lenu lizidi kuwa jingi sana, katika hekima na ufahamu wote;
1 Thessaloniciens 3.12 2 Pierre 1.5-1.6 Colossiens 1.9 Colossiens 3.10 1 Thessaloniciens 4.9-4.10
10 mpate kuyakubali yaliyo mema; ili mpate kuwa na mioyo safi, bila kosa, mpaka siku ya Kristo;
1 Thessaloniciens 3.13 1 Thessaloniciens 5.23 Romains 12.2 1 Corinthiens 1.8 Philippiens 1.6
11 hali mmejazwa matunda ya haki, kwa njia ya Yesu Kristo, kwa utukufu na sifa ya Mungu.
Colossiens 1.6 Jean 15.8 Hébreux 12.11 Jean 15.4-15.5 Matthieu 5.16

Nouvelles de Paul

12 Lakini, ndugu zangu, nataka mjue ya kuwa mambo yote yaliyonipata yametokea zaidi kwa kuieneza Injili;
Romains 8.28 2 Timothée 2.9 Romains 8.37 Actes 28.1-28.31 Actes 22.1-22.30
13 hata vifungo vyangu vimekuwa dhahiri katika Kristo, miongoni mwa askari, na kwa wengine wote pia.
Philippiens 1.7 Philippiens 4.22 1 Thessaloniciens 1.8-1.9 Colossiens 4.3-4.18 Actes 28.17
14 Na wengi wa hao ndugu walio katika Bwana, hali wakapata kuthibitika kwa ajili ya kufungwa kwangu, wamezidi sana kuthubutu kunena neno la Mungu pasipo hofu.
Ephésiens 6.19-6.20 Philippiens 4.1 Colossiens 4.4 Luc 12.5-12.7 Ephésiens 3.13
15 Wengine wanahubiri habari za Kristo kwa sababu ya husuda na fitina; na wengine kwa nia njema.
Philippiens 2.3 Romains 16.17-16.18 2 Corinthiens 11.13 1 Corinthiens 3.3-3.4 2 Corinthiens 1.19
16 Hawa wanamhubiri kwa pendo, wakijua ya kuwa nimewekwa ili niitetee Injili;
Philippiens 1.7 Job 6.14 Philippiens 1.12 Philippiens 1.10 Psaumes 69.26
17 bali wengine wanamhubiri Kristo kwa fitina, wala si kwa moyo mweupe, wakidhani kuongeza dhiki za kufungwa kwangu.
Philippiens 2.3 Philippiens 1.7 Actes 26.1 2 Timothée 4.6-4.7 1 Timothée 2.7
18 Yadhuru nini? Lakini kwa njia zote, ikiwa ni kwa hila, au ikiwa ni kwa kweli, Kristo anahubiriwa; na kwa hiyo nafurahi, naam, nami nitafurahi.
Luc 9.50 1 Corinthiens 15.11 Marc 9.38-9.40 2 Jean 1.9-1.11 1 Corinthiens 10.19
19 Maana najua ya kuwa haya yatanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa sababu ya kuomba kwenu, na kuruzukiwa Roho wa Yesu Kristo;
2 Corinthiens 1.11 Romains 8.28 Galates 4.6 Actes 16.7 Romains 8.9
20 kama vile nilivyotazamia sana, na kutumaini, kwamba sitaaibika kamwe, bali kwa uthabiti wote, kama sikuzote na sasa vivyo hivyo Kristo ataadhimishwa katika mwili wangu; ikiwa kwa maisha yangu, au ikiwa kwa mauti yangu.
1 Corinthiens 6.20 Romains 8.19 1 Pierre 4.16 Romains 5.5 Esaïe 50.7
21 Kwa maana kwangu mimi kuishi ni Kristo, na kufa ni faida.
Galates 2.20 Philippiens 1.23 Philippiens 1.20 Romains 8.35-8.39 2 Corinthiens 5.8
22 Ila ikiwa kuishi katika mwili, kwangu mimi ni matunda ya kazi; basi nitakalolichagua silitambui.
Colossiens 2.1 Philippiens 1.24 Psaumes 71.18 Exode 32.1 1 Pierre 4.2
23 Ninasongwa katikati ya mambo mawili; ninatamani kwenda zangu nikae na Kristo maana ni vizuri zaidi sana;
2 Corinthiens 5.8 2 Timothée 4.6 Job 19.26-19.27 Psaumes 16.10-16.11 Jean 12.26
24 bali kudumu katika mwili kwahitajiwa zaidi kwa ajili yenu.
Jean 16.7 Philippiens 1.22 Philippiens 1.25-1.26 Actes 20.29-20.31
25 Nami nikitumaini hayo, najua ya kuwa nitakaa na kudumu pamoja nanyi, ili mpate kuendelea na kufurahi katika imani;
Philippiens 2.24 Actes 20.25 Romains 15.13 2 Corinthiens 1.24 Romains 5.2
26 hata mzidi kuona fahari katika Kristo Yesu juu yangu kwa sababu ya kuwapo kwangu pamoja nanyi tena.
2 Corinthiens 1.14 2 Corinthiens 5.12 Cantique 5.1 Jean 16.22 Philippiens 3.3

Appel à suivre l’exemple de Christ

27 Lakini mwenendo wenu na uwe kama inavyoipasa Injili ya Kristo, ili, nikija na kuwaona ninyi, au nisipokuwapo, niyasikie mambo yenu, kama mnasimama imara katika roho moja, kwa moyo mmoja mkiishindania imani ya Injili;
Ephésiens 4.1 Jude 1.3 2 Pierre 3.14 Philippiens 2.12 1 Corinthiens 16.13-16.14
28 wala hamwaogopi adui zenu, katika neno lo lote; kwao hao ni ishara mathubuti ya kupotea, bali kwenu ninyi ni ishara ya wokovu, huo utokao kwa Mungu.
2 Thessaloniciens 1.5-1.6 Psaumes 68.19-68.20 Genèse 49.18 Romains 8.17 Matthieu 10.28
29 Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake;
Actes 5.41 Jacques 1.2 Romains 5.3 Actes 14.22 1 Pierre 4.13
30 mkiwa na mashindano yale yale mliyoyaona kwangu, na kusikia kwamba ninayo hata sasa.
Actes 16.19-16.40 1 Thessaloniciens 2.2 Hébreux 12.4 2 Timothée 4.7 Romains 8.35-8.37

Cette Bible est dans le domaine public.