Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 4.15
Bible en Swahili de l’est


Appel à découvrir la sagesse de la loi

1 Na sasa, Ee Israeli, zisikilizeni amri na hukumu niwafundishazo, ili mzitende; mpate kuishi na kuingia na kuimiliki nchi awapayo Bwana, Mungu wa baba zenu.
Deutéronome 8.1 Romains 10.5 Ezéchiel 20.11 Lévitique 18.5 Jean 15.14
2 Msiliongeze neno niwaamurulo wala msilipunguze, mpate kuzishika amri za Bwana, Mungu wenu, niwaamuruzo.
Deutéronome 12.32 Proverbes 30.6 Josué 1.7 Apocalypse 22.18-22.19 Galates 3.15
3 Macho yenu yameona aliyoyatenda Bwana kwa sababu ya Baal-peori; maana wote waliomfuata Baal-peori, Bwana, Mungu wako, amewaangamiza kutoka kati yako.
Nombres 25.1-25.9 Psaumes 106.28-106.29 Josué 22.17 Nombres 31.16 Nombres 26.64
4 Bali ninyi mlioambatana na Bwana, Mungu wenu, mnaishi kila mmoja wenu, hata leo.
Actes 11.23 Josué 23.8 Ruth 1.14-1.17 Romains 12.9 Jean 6.67-6.69
5 Angalieni nimewafundisha amri na hukumu, vile vile kama Bwana, Mungu wangu, alivyoniamuru, ili mzitende katika nchi mwingiayo ili kuimiliki.
Hébreux 3.5 1 Corinthiens 11.28 Matthieu 28.20 1 Thessaloniciens 4.1-4.2 Actes 20.27
6 Zishikeni basi, mkazitende, maana hii ndiyo hekima yenu na akili zenu, machoni pa mataifa watakaozisikia amri hizi zote, nao watasema, Hakika taifa hili kubwa ni watu wenye hekima na akili.
Job 28.28 Proverbes 1.7 Psaumes 111.10 Psaumes 19.7 Daniel 5.11-5.16
7 Kwa maana liko taifa gani kubwa, lililo na Mungu aliye karibu nao, kama Bwana, Mungu wetu, alivyo, kila tumwitapo?
Psaumes 145.18 2 Samuel 7.23 Psaumes 148.14 Psaumes 34.18 Jacques 4.8
8 Tena liko taifa gani kubwa, lililo na amri na hukumu zenye haki kama torati hii yote, ninayoiweka mbele yenu leo.
Psaumes 147.19-147.20 2 Timothée 3.16-3.17 Psaumes 119.127-119.128 Psaumes 19.7-19.11 Deutéronome 10.12-10.13
9 Lakini, jihadhari nafsi yako, ukailinde roho yako kwa bidii, usije ukayasahau mambo yale uliyoyaona kwa macho yako, yakaondoka moyoni mwako siku zote za maisha yako; bali uwajulishe watoto wako na watoto wa watoto wako;
Deutéronome 6.7 Deutéronome 11.19 Genèse 18.19 Deutéronome 32.46 Ephésiens 6.4
10 siku ile uliyosimama mbele za Bwana wako huko Horebu, Bwana aliponiambia, Nikusanyieni watu hawa, nami nitawasikizisha maneno yangu, ili wajifunze kunicha mimi siku zote watakazoishi duniani, wakapate na kuwafundisha watoto wao.
Exode 19.9 Exode 19.16 Hébreux 12.18-12.19 Deutéronome 17.19 Deutéronome 5.29
11 Mkakaribia, mkasimama chini ya ule mlima; mlima ukawaka moto mpaka kati ya mbinguni, kwa giza na mawingu, na giza kuu.
Deutéronome 5.23 Exode 19.16-19.18 Hébreux 12.18-12.19 Exode 20.18-20.19
12 Bwana akasema nanyi kutoka kati ya moto; mkasikia sauti ya maneno, lakini hamkuona umbo lo lote; sauti tu.
Exode 20.22 Deutéronome 5.4 Deutéronome 5.22 Deutéronome 4.15 Deutéronome 4.36
13 Akawahubiri agano lake, alilowaamuru kulitenda, yaani, zile amri kumi; akaziandika juu ya mbao mbili za mawe.
Exode 34.28 Exode 31.18 Exode 24.12 Hébreux 9.4 Exode 19.5
14 Bwana akaniamuru wakati ule niwafundishe maagizo na hukumu, mpate kuzitenda katika nchi ile mtakayoivukia ili kuimiliki.
Psaumes 105.44-105.45 Ezéchiel 21.1-21.23
15 Jihadharini nafsi zenu basi; maana hamkuona umbo la namna yo yote siku ile Bwana aliyosema nanyi kutoka kati ya moto;
Josué 23.11 Esaïe 40.18 Deutéronome 4.12 Proverbes 4.27 Malachie 2.15
16 msije mkajiharibu nafsi zenu, mkajifanyia sanamu ya kuchonga, mfano wa sura yo yote, mfano wa mwanamume au mwanamke,
Deutéronome 4.23 Exode 20.4-20.5 Deutéronome 5.8 Exode 32.7 Actes 17.29
17 mfano wa mnyama ye yote aliye duniani, au mfano wa ndege ye yote arukaye mbinguni,
Romains 1.23
18 au mfano wa kitu cho chote kitambaacho juu ya ardhi, au mfano wa samaki ye yote aliye majini chini ya nchi;
19 tena usije ukainua macho yako hata mbinguni, na ulionapo jua, na mwezi, na nyota, jeshi la mbinguni lote pia, ukashawishwa na kuviabudu, na kuvitumikia, ambavyo Bwana, Mungu wako amewagawanyia watu wote chini ya mbingu zote.
2 Rois 17.16 Deutéronome 17.3 2 Rois 21.3 Genèse 2.1 Romains 1.25
20 Bali Bwana amewatwaa ninyi, na kuwatoa katika tanuu ya chuma, katika Misri, mpate kuwa watu wa urithi kwake, kama mlivyo leo hivi.
1 Rois 8.51 Jérémie 11.4 Deutéronome 9.29 1 Pierre 2.9 Tite 2.14
21 Tena Bwana alinikasirikia kwa ajili yenu, akaapa ya kwamba sitavuka Yordani, na ya kwamba sitaingia nchi ile njema, awapayo Bwana, Mungu wenu, iwe urithi.
Deutéronome 1.37 Nombres 20.12 Psaumes 106.32-106.33 Deutéronome 31.2 Deutéronome 3.26
22 Lakini mimi nitakufa katika nchi hii, sina ruhusa kuvuka Yordani; bali ninyi mtavuka, na kuimiliki nchi ile njema.
Deutéronome 3.25 Deutéronome 3.27 2 Pierre 1.13-1.15 Hébreux 12.6-12.10 1 Rois 13.21-13.22
23 Jihadharini nafsi zenu, msije mkalisahau agano la Bwana, Mungu wenu, alilolifanya nanyi, mkajifanyia sanamu ya kuchonga, mfano wa umbo la kitu cho chote ulichokatazwa na Bwana, Mungu wenu,
Deutéronome 4.9 Josué 23.11 Deutéronome 27.9 Deutéronome 4.15-4.16 Josué 23.16
24 kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, ni moto ulao, Mungu mwenye wivu.
Hébreux 12.29 Exode 24.17 Deutéronome 9.3 Exode 20.5 Deutéronome 6.15
25 Utakapozaa wana, na wana wa wana, mkisha kuwa katika nchi siku nyingi, mkajiharibu na kufanya sanamu ya kuchonga kwa umbo la kitu cho chote, mkafanya ambayo ni maovu machoni pa Bwana, Mungu wako, na kumtia hasira;
Deutéronome 4.16 2 Rois 21.14-21.16 Deutéronome 31.29 Osée 9.9 2 Chroniques 36.12-36.16
26 nawashuhudizia mbingu na nchi hivi leo, kwamba karibu mtaangamia kabisa juu ya nchi mwivukiayo Yordani kuimiliki, hamtafanya siku zenu ziwe nyingi juu yake, ila mtaangamizwa kabisa.
Michée 6.2 Deutéronome 30.18-30.19 Esaïe 1.2 Deutéronome 32.1 Deutéronome 31.28
27 Na Bwana atawatawanya kati ya mataifa, nanyi mtasalia watu kidogo hesabu yenu kati ya makabila, mtakakopelekwa mbali na Bwana.
Lévitique 26.33 Deutéronome 28.62-28.64 Néhémie 1.3 Ezéchiel 32.26 Ezéchiel 12.15
28 Na huko mtatumikia miungu, kazi za mikono ya watu, miti na mawe, ambao hawaoni, wala hawasikii, hawali, wala hawanusi.
Jérémie 16.13 Deutéronome 28.64 Deutéronome 28.36 Esaïe 44.9 1 Samuel 26.19
29 Lakini huko, kama mkimtafuta Bwana, Mungu wako, utampata, ukimtafuta kwa moyo wako wote, na roho yako yote.
2 Chroniques 15.4 Esaïe 55.6-55.7 Jérémie 29.12-29.14 Psaumes 119.2 Deutéronome 30.10
30 Na wakati uwapo katika mashaka, ukiisha kupatwa na mambo haya yote, siku za mwisho, utamrudia Bwana, Mungu wako, na kuisikiza sauti yake;
Deutéronome 31.29 Jérémie 23.20 Osée 3.5 Hébreux 1.2 Nombres 24.20
31 kwa kuwa Bwana, Mungu wako, ni Mungu wa rehema; hatakukosa wala kukuangamiza, wala hatalisahau agano la baba zako alilowaapia.
Deutéronome 31.8 Lévitique 26.42 Jonas 4.2 Néhémie 9.31 2 Chroniques 30.9
32 Maana uliza sasa siku zilizopita, zilizokuwa kabla yako, tangu siku ile Mungu aliyoumba mwanadamu juu ya nchi, na toka pembe hii ya mbingu hata pembe hii, kwamba kumetukia neno lo lote kama neno hili kubwa, au kwamba kumesikiwa habari ya neno kama hili?
Job 8.8 Matthieu 24.31 Psaumes 44.1 Deutéronome 30.4 Marc 13.27
33 Je! Watu wakati wo wote wameisikia sauti ya Mungu ikinena toka kati ya moto, kama wewe ulivyosikia, wasife?
Deutéronome 5.24 Juges 6.22 Exode 24.11 Exode 33.20 Deutéronome 5.26
34 Au Mungu amekwenda wakati gani akajitwalia taifa toka kati ya taifa lingine, kwa majaribu, na kwa ishara, na kwa maajabu, na kwa vita, na kwa mkono hodari, na kwa mkono ulionyoshwa, na kwa maogofya makuu, kama vile Bwana, Mungu wenu, alivyowatendea ninyi katika Misri, mbele ya macho yenu?
Deutéronome 26.8 Deutéronome 7.19 Deutéronome 5.15 Deutéronome 7.8-7.9 Exode 6.6
35 Wewe umeonyeshwa haya, ili upate kujua ya kuwa Bwana ndiye Mungu, hapana mwingine ila yeye.
Esaïe 45.5 Esaïe 45.18 1 Samuel 2.2 Marc 12.32 Esaïe 44.8
36 Kutoka mbinguni amekusikizisha sauti yake, ili akufundishe; na juu ya nchi alikuonyesha moto wake mkuu; ukasikia maneno yake toka kati ya moto.
Exode 19.19 Exode 19.9 Deutéronome 4.33 Néhémie 9.13 Hébreux 12.25
37 Na kwa sababu aliwapenda baba zenu, kwa sababu hiyo aliwachagua wazao wao baada yao, akakutoa katika Misri kwa kuwako pamoja nawe, kwa uweza wake mwingi,
Deutéronome 10.15 Exode 13.14 Exode 13.3 Exode 13.9 Esaïe 41.8-41.9
38 ili kufukuza mbele yako mataifa, walio wakubwa, wenye nguvu kukupita wewe, ili kukuingiza, na kukupa nchi yao iwe urithi, kama ilivyo leo.
Deutéronome 7.1 Exode 23.27-23.28 Deutéronome 9.1-9.5 Deutéronome 11.23 Psaumes 44.2-44.3
39 Kwa hiyo ujue, leo hivi, ukaweke moyoni mwako, ya kuwa Bwana ndiye Mungu katika mbingu juu, na katika nchi chini; hapana mwingine.
Josué 2.11 Deutéronome 4.35 2 Chroniques 20.6 Daniel 4.35 Esaïe 5.12
40 Basi, zishike sheria zake, na amri zake, ninazokuamuru leo, upate kufanikiwa, wewe na watoto wako baada yako, na siku zako ziwe nyingi katika nchi ile akupayo Bwana, Mungu wako, milele.
Deutéronome 6.3 Deutéronome 5.16 Lévitique 22.31 Deutéronome 6.18 Deutéronome 12.28
41 Ndipo Musa akabagua miji mitatu ng’ambo ya Yordani upande wa matokeo ya jua;
Nombres 35.6 Nombres 35.14-35.15 Josué 20.2-20.9
42 ili kwamba amwuaye mtu apate kukimbilia huko, amwuaye jirani yake pasipo kujua, wala hakumchukia tangu hapo; ili apate kuishi akimbiliapo mmojawapo miji hiyo;
Nombres 35.11-35.12 Nombres 35.6 Nombres 35.15-35.28 Deutéronome 19.1-19.10 Hébreux 6.18
43 nayo ni hii, Beseri ya barani iliyo katika nchi tambarare, kwa Wareubeni; na Ramothi iliyo Gileadi, kwa Wagadi; na Golani iliyo Bashani, kwa Wamanase.
Josué 20.8 1 Rois 4.13 1 Chroniques 6.71 Josué 21.38 Josué 21.27

Rappel des dix commandements

44 Na torati Musa aliyowawekea wana wa Israeli ni hii;
Deutéronome 1.5 Deutéronome 27.8 Lévitique 27.34 Malachie 4.4 Deutéronome 17.18-17.19
45 haya ndiyo mashuhudizo, na amri, na hukumu, Musa alizowaambia wana wa Israeli walipotoka Misri;
Psaumes 119.14 Deutéronome 4.1 Psaumes 119.5 Psaumes 119.2 Deutéronome 6.17
46 ng’ambo ya Yordani, katika bonde lililoelekea Beth-peori, katika nchi ya Sihoni mfalme wa Waamori, aliyekuwa akikaa Heshboni ndiye aliyepigwa na Musa na wana wa Israeli, walipotoka Misri;
Deutéronome 3.29 Deutéronome 1.4-1.5 Deutéronome 2.30-2.36 Deutéronome 3.8 Nombres 32.19
47 wakaishika nchi yake, ikawa milki yao, na nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, ndio wafalme wawili wa Waamori, waliokuwa ng’ambo ya Yordani upande wa matokeo ya jua;
Deutéronome 3.1-3.14 Nombres 21.33-21.35 Deutéronome 29.7-29.8
48 toka Aroeri, iliyo juu ya ukingoni pa bonde la Arnoni, hata mpaka mlima wa Sioni (nao ndio Hermoni),
Deutéronome 3.9 Deutéronome 2.36 Psaumes 133.3 Deutéronome 3.12 Josué 13.24-13.33
49 na Araba yote iliyo ng’ambo ya Yordani upande wa mashariki, hata mpaka bahari ya Araba, chini ya matelemko ya Pisga.
Deutéronome 3.17 Josué 13.20 Deutéronome 34.1

Cette Bible est dans le domaine public.