Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 21.3
Bible en Swahili de l’est


Meurtres dont les auteurs sont inconnus

1 Aonekanapo mtu ameuawa katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako, kuimiliki, amelala kondeni, wala haijulikani ni nani aliyempiga;
Proverbes 28.17 Psaumes 9.12 Esaïe 26.21 Psaumes 5.6 Actes 28.4
2 na watoke nje wazee wako na waamuzi wako, nao wapime hapo mpaka miji iliyomzunguka huyo aliyeuawa;
Romains 13.3-13.4 Deutéronome 16.18-16.19
3 na iwe, mji ulio karibu na yule aliyeuawa, wale wazee wake mji huo watwae mtamba katika kundi la ng’ombe, ambaye hajafanya kazi, wala hajakokota jembe la nira;
Nombres 19.2 Philippiens 2.8 Jérémie 31.18 Matthieu 11.28-11.30
4 wazee wa mji huo na wamshushe yule mtamba mpaka bonde lenye maji ya mtoni, lisilolimwa wala kupandwa, wakamvunje yule mtamba shingo yake humo bondeni;
1 Pierre 2.21-2.24 1 Pierre 3.18
5 nao makuhani wana wa Lawi wasongee karibu, kwa kuwa ndio aliowachagua Bwana, Mungu wako, wamtumikie, na kubariki katika jina la Bwana na kila neno lishindaniwalo, na kila pigo, litakuwa kwa kufuata maneno yao;
1 Chroniques 23.13 Deutéronome 10.8 Malachie 2.7 Deutéronome 17.8-17.12 Deutéronome 19.17
6 na wazee wote wa mji ule, ulio karibu sana na yule aliyeuawa, na waoshe mikono yao juu ya huyo mtamba aliyevunjwa shingo yake humo bondeni;
Psaumes 73.13 Psaumes 26.6 Psaumes 51.7 Psaumes 19.12 Jérémie 2.22
7 na wajibizane kwamba, Mikono yetu haikumwaga damu hii, wala macho yetu hayakuiona.
2 Samuel 16.8 Nombres 5.19-5.28 Psaumes 7.3-7.4 Job 21.21-21.23 Job 21.31-21.34
8 Ee Bwana, samehe watu wako Israeli, uliowakomboa, wala usiache damu ya asiye makosa ikakaa katikati ya watu wako Israeli. Na ile damu utasamehewa kwao.
Jonas 1.14 2 Samuel 3.28 2 Rois 24.4 1 Thessaloniciens 2.15-2.16 Nombres 35.33-35.34
9 Ndivyo utakavyoondoa damu ya asiye makosa katikati yako, utakapofanya yaliyo sawa machoni pa Bwana.
Deutéronome 19.12-19.13 Deutéronome 13.18 2 Rois 10.30-10.31

Règles pour la tenue de la famille

10 Utakapokwenda vitani kupigana juu ya adui zako, na Bwana, Mungu wako, awatiapo mikononi mwako, nawe uwachukuapo mateka,
Deutéronome 20.10-20.16 Josué 21.44
11 ukaona kati ya mateka mwanamke mzuri, ukafanya tamaa kwake, ukawaza kumtwaa kuwa mkeo;
Proverbes 6.25 Juges 14.2-14.3 Genèse 12.14-12.15 Proverbes 31.10 Genèse 34.3
12 ndipo umchukue kwenu nyumbani kwako, naye atanyoa kichwa, akate na kucha;
Ephésiens 4.22 Nombres 6.9 Lévitique 14.9 1 Corinthiens 11.6
13 avue na mavazi ya uteka wake akae nyumbani mwako, awakalie matanga babaye na mamaye mwezi mzima, kisha uingie kwake uwe mumewe, naye awe mkeo.
Psaumes 45.10-45.11 Luc 14.26-14.27
14 Tena utakapokuwa huna furaha naye, mpe ruhusa aende atakako; lakini usimwuze kabisa kwa fedha, usimfanye kama mtumwa, kwa kuwa ulimtweza.
Genèse 34.2 Deutéronome 22.24 Deutéronome 22.19 Deutéronome 22.29 Juges 19.24
15 Akiwa mtu yuna wake wawili, mmoja ampenda, mmoja hampendi, nao wamemzalia watoto, ampendaye na asiyempenda wote wawili; na yule mzaliwa wa kwanza akiwa ni wa mke asiyependwa;
Genèse 29.33 1 Samuel 1.4-1.5 Genèse 29.18 Genèse 29.30-29.31 Genèse 29.20
16 ndipo itakapokuwa ya kwamba siku atakayowarithisha wanawe alivyo navyo, asimweke mwana wa ampendaye kuwa mzaliwa wa kwanza mbele ya mwana wa asiyempenda, naye ndiye mzaliwa wa kwanza huyu;
1 Chroniques 26.10 1 Chroniques 5.2 Philippiens 4.8 Romains 8.29 2 Chroniques 21.3
17 lakini amkubali mzaliwa wa kwanza mwana wa yule asiyempenda, kwa kumpa mafungu mawili katika vyote alivyo navyo; kwa maana ndiye mwanzo wa nguvu zake; haki ya mzaliwa wa kwanza ni yake yeye.
Genèse 49.3 Genèse 25.31-25.34 1 Chroniques 5.1-5.2 Psaumes 105.36 Genèse 25.5-25.6
18 Mtu akiwa na mwana mkaidi, mshupavu, asiyetii sauti ya baba yake, wala sauti ya mama yake, nao wajapomwadhibu hawasikizi,
Exode 20.12 Lévitique 19.3 Esaïe 1.5 Exode 21.15 Proverbes 22.15
19 ndipo babaye na mamaye na wamkamate, na kumpeleka kwa wazee wa mji wake, katika lango la mahali pake;
Zacharie 13.3 Deutéronome 16.18 Deutéronome 25.7 Deutéronome 21.2
20 wawaambie wazee wa mji wake, Huyu mwana wetu ni mkaidi, mshupavu, hasikizi sauti yetu; ni mwasherati, tena ni mlevi.
Proverbes 20.1 Proverbes 29.17 Proverbes 23.19-23.21 Proverbes 19.26 Proverbes 23.29-23.35
21 Waume wote wa mji wake na wamtupie mawe, afe; ndivyo utakavyoondoa uovu katikati yako; na Israeli wote watasikia na kuogopa.
Deutéronome 19.19-19.20 Lévitique 24.16 Deutéronome 13.5 Deutéronome 13.10-13.11 Deutéronome 22.21

Instructions diverses

22 Akiwa mtu ametenda dhambi ipasayo kufa, akauawa, nawe ukamtundika juu ya mti;
Deutéronome 22.26 Actes 23.29 Matthieu 26.66 Jean 19.31-19.38 2 Samuel 21.9
23 mzoga wake usikae usiku kucha juu ya mti; lazima utamzika siku iyo hiyo; kwani aliyetundikwa amelaaniwa na Mungu; usije ukatia unajisi katika nchi yako akupayo Bwana, Mungu wako, iwe urithi wako.
Galates 3.13 Lévitique 18.25 Jean 19.31 2 Corinthiens 5.21 Josué 8.29

Cette Bible est dans le domaine public.