Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ephésiens 2.1
Bible en Swahili de l’est


Un salut accordé par grâce

1 Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu;
Colossiens 2.13 Ephésiens 2.5-2.6 Ephésiens 4.18 Jean 11.25-11.26 Colossiens 3.1-3.4
2 ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi;
Ephésiens 6.12 Ephésiens 2.3 Ephésiens 5.6 Jean 12.31 1 Corinthiens 6.11
3 ambao zamani, sisi sote nasi tulienenda kati yao, katika tamaa za miili yetu, tulipoyatimiza mapenzi ya mwili na ya nia, tukawa kwa tabia yetu watoto wa hasira kama na hao wengine.
Tite 3.3 Psaumes 51.5 Galates 2.15-2.16 1 Corinthiens 4.7 Ephésiens 4.22
4 Lakini Mungu, kwa kuwa ni mwingi wa rehema, kwa mapenzi yake makuu aliyotupenda;
1 Pierre 1.3 Ephésiens 1.7 Ephésiens 2.7 Psaumes 86.15 Psaumes 145.8
5 hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, tumeokolewa kwa neema.
Ephésiens 2.1 Actes 15.11 Romains 5.8 Ephésiens 2.8 Romains 5.10
6 Akatufufua pamoja naye, akatuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho, katika Kristo Yesu;
Ephésiens 1.3 Colossiens 3.1-3.3 Romains 6.4-6.5 Colossiens 2.12-2.13 Jean 17.21-17.26
7 ili katika zamani zinazokuja audhihirishe wingi wa neema yake upitao kiasi kwa wema wake kwetu sisi katika Kristo Yesu.
Tite 3.4 Ephésiens 2.4 Apocalypse 5.9-5.14 Esaïe 60.15 1 Timothée 1.16-1.17
8 Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu;
Ephésiens 2.5 Romains 3.22-3.26 Romains 4.16 Jacques 1.16-1.18 Actes 16.31
9 wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu.
2 Timothée 1.9 Romains 11.6 Tite 3.3-3.5 1 Corinthiens 1.29-1.31 Romains 9.11
10 Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.
Colossiens 1.10 Philippiens 2.13 2 Corinthiens 5.17 Hébreux 13.21 Ephésiens 4.24

Juifs et non-Juifs unis en Christ

11 Kwa ajili ya hayo kumbukeni ya kwamba zamani ninyi, mlio watu wa Mataifa kwa jinsi ya mwili, mnaoitwa Wasiotahiriwa na wale wanaoitwa Waliotahiriwa, yaani, tohara ya mwilini iliyofanyika kwa mikono;
Colossiens 2.11 Colossiens 2.13 1 Corinthiens 12.2 Colossiens 3.11 Colossiens 1.21
12 kwamba zamani zile mlikuwa hamna Kristo, mmefarakana na jamii ya Israeli, wageni wasio wa maagano ya ahadi ile. Mlikuwa hamna tumaini, hamna Mungu duniani.
Galates 4.8 Colossiens 1.21 1 Thessaloniciens 4.13 1 Thessaloniciens 4.5 Psaumes 89.3-89.18
13 Lakini sasa, katika Kristo Yesu, ninyi mliokuwa mbali hapo kwanza mmekuwa karibu kwa damu yake Kristo.
Actes 2.39 Esaïe 57.19 Actes 26.18 Romains 3.23-3.30 Colossiens 1.13-1.14
14 Kwa maana yeye ndiye amani yetu, aliyetufanya sisi sote tuliokuwa wawili kuwa mmoja; akakibomoa kiambaza cha kati kilichotutenga.
Ephésiens 2.15 Galates 3.28 Colossiens 3.11 Colossiens 1.20 Hébreux 13.20
15 Naye akiisha kuuondoa ule uadui kwa mwili wake; ndiyo sheria ya amri zilizo katika maagizo; ili afanye hao wawili kuwa mtu mpya mmoja ndani ya nafsi yake; akafanya amani.
Colossiens 2.14 Colossiens 2.20 Galates 3.28 Colossiens 3.10 Hébreux 7.16
16 Akawapatanisha wote wawili na Mungu katika mwili mmoja, kwa njia ya msalaba, akiisha kuufisha ule uadui kwa huo msalaba.
Colossiens 1.20-1.22 Ephésiens 2.15 2 Corinthiens 5.18-5.21 Romains 8.3 Romains 5.10
17 Akaja akahubiri amani kwenu ninyi mliokuwa mbali, na amani kwao wale waliokuwa karibu.
Actes 10.36 Psaumes 148.14 Esaïe 57.19-57.21 Deutéronome 4.7 Ephésiens 2.13-2.14
18 Kwa maana kwa yeye sisi sote tumepata njia ya kumkaribia Baba katika Roho mmoja.
Ephésiens 3.12 1 Corinthiens 12.13 Romains 5.2 Jean 14.6 Jean 10.9
19 Basi tangu sasa ninyi si wageni wala wapitaji, bali ninyi ni wenyeji pamoja na watakatifu, watu wa nyumbani mwake Mungu.
Galates 6.10 Philippiens 3.20 Ephésiens 3.6 Hébreux 12.22-12.24 Galates 3.26-3.28
20 Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni.
Apocalypse 21.14 Esaïe 28.16 Matthieu 16.18 1 Pierre 2.4-2.5 1 Pierre 2.7-2.8
21 Katika yeye jengo lote linaungamanishwa vema na kukua hata liwe hekalu takatifu katika Bwana.
1 Corinthiens 3.16-3.17 Ephésiens 4.13-4.16 2 Corinthiens 6.16 Ezéchiel 42.12 Ezéchiel 40.1-40.42
22 Katika yeye ninyi nanyi mnajengwa pamoja kuwa maskani ya Mungu katika Roho.
1 Corinthiens 3.16 1 Pierre 2.4-2.5 1 Jean 4.16 2 Corinthiens 6.16 1 Jean 4.13

Cette Bible est dans le domaine public.