Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Galates 6.6
Bible en Swahili de l’est


Mise en pratique de la vie nouvelle

1 Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lo lote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe.
Romains 15.1 2 Timothée 2.25 2 Thessaloniciens 3.15 Hébreux 12.13 1 Jean 5.16
2 Mchukuliane mizigo na kuitimiza hivyo sheria ya Kristo.
Romains 15.1 Jean 13.34 1 Thessaloniciens 5.14 1 Jean 4.21 Jacques 2.8
3 Maana mtu akijiona kuwa ni kitu, naye si kitu, ajidanganya nafsi yake.
1 Corinthiens 3.18 2 Corinthiens 12.11 1 Corinthiens 8.2 2 Timothée 3.13 Galates 2.6
4 Lakini kila mtu na aipime kazi yake mwenyewe, ndipo atakapokuwa na sababu ya kujisifu ndani ya nafsi yake tu, wala si kwa mwenzake.
2 Corinthiens 13.5 1 Jean 3.19-3.22 1 Corinthiens 11.28 1 Corinthiens 1.12-1.13 Luc 18.11
5 Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe.
Romains 14.10-14.12 Jérémie 32.19 1 Corinthiens 3.8 Apocalypse 20.12-20.15 1 Corinthiens 4.5
6 Mwanafunzi na amshirikishe mkufunzi wake katika mema yote.
Romains 15.27 Matthieu 10.10 1 Timothée 5.17-5.18 1 Corinthiens 9.9-9.14 Deutéronome 12.19
7 Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna.
2 Corinthiens 9.6 Osée 10.12 Romains 2.6-2.10 Proverbes 11.18 1 Corinthiens 15.33
8 Maana yeye apandaye kwa mwili wake, katika mwili wake atavuna uharibifu; bali yeye apandaye kwa Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele.
Jacques 3.18 2 Pierre 2.19 Romains 8.13 Romains 6.21-6.22 Job 4.8
9 Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho.
1 Corinthiens 15.58 2 Thessaloniciens 3.13 Esaïe 40.30-40.31 Hébreux 10.35-10.39 Hébreux 12.3
10 Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio.
Hébreux 13.16 Proverbes 3.27 Ephésiens 2.19 3 Jean 1.5-1.8 Matthieu 12.50

Conclusion et salutations

11 Tazameni ni kwa herufi gani kubwa nimewaandikia kwa mkono wangu mimi mwenyewe!
1 Corinthiens 16.21-16.23 Romains 16.22
12 Wote watakao kuonekana ni wazuri kwa mambo ya mwili, ndio wanaowashurutisha kutahiriwa; makusudi wasiudhiwe kwa ajili ya msalaba wa Kristo, hilo tu.
Galates 5.11 Actes 15.1 2 Corinthiens 11.13 Colossiens 2.23 Galates 2.3
13 Kwa maana hata wao wenyewe waliotahiriwa hawaishiki sheria; bali wanataka ninyi mtahiriwe, wapate kuona fahari katika miili yenu.
Philippiens 3.3 Romains 3.9-3.19 Matthieu 23.15 2 Pierre 2.19 Matthieu 23.3
14 Lakini mimi, hasha, nisione fahari juu ya kitu cho chote ila msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambao kwa huo ulimwengu umesulibishwa kwangu, na mimi kwa ulimwengu.
Romains 6.6 Philippiens 3.3 2 Corinthiens 12.10-12.11 Galates 5.24 Romains 1.16
15 Kwa sababu kutahiriwa si kitu, wala kutokutahiriwa, bali kiumbe kipya.
2 Corinthiens 5.17 Galates 5.6 1 Corinthiens 7.19 Colossiens 3.10-3.11 Ephésiens 2.10
16 Na wote watakaoenenda kwa kanuni hiyo, amani na iwe kwao na rehema, naam, kwa Israeli wa Mungu.
Galates 3.29 Philippiens 3.3 Romains 9.6-9.8 Galates 3.7-3.9 Romains 4.12
17 Tangu sasa mtu asinitaabishe; kwa maana ninachukua mwilini mwangu chapa zake Yesu.
2 Corinthiens 1.5 Colossiens 1.24 2 Corinthiens 4.10 Galates 5.11-5.12 Esaïe 44.5
18 Ndugu zangu, neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja na roho zenu. Amina.
Romains 16.20 2 Timothée 4.22 Philémon 1.25 Apocalypse 22.21 2 Corinthiens 13.14

Cette Bible est dans le domaine public.