Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Galates 5.24
Bible en Swahili de l’est


Une liberté à conserver

1 Katika ungwana huo Kristo alituandika huru; kwa hiyo simameni, wala msinaswe tena chini ya kongwa la utumwa.
2 Corinthiens 3.17 Galates 5.13 Jean 8.32-8.36 Galates 2.4 1 Corinthiens 16.13
2 Tazama, mimi Paulo nawaambia ninyi ya kwamba, mkitahiriwa, Kristo hatawafaidia neno.
Galates 5.6 Romains 9.31-9.32 Galates 5.3-5.4 Actes 15.1 Galates 2.3-2.5
3 Tena namshuhudia kila mtu atahiriwaye, kwamba ni wajibu wake kuitimiza torati yote.
Galates 3.10 Ephésiens 4.17 Jacques 2.10-2.11 Romains 2.25 Deutéronome 27.26
4 Mmetengwa na Kristo, ninyi mtakao kuhesabiwa haki kwa sheria; mmeanguka na kutoka katika hali ya neema.
2 Pierre 2.20-2.22 Galates 2.21 Hébreux 12.15 Romains 11.6 Romains 9.31-9.32
5 Maana sisi kwa Roho tunalitazamia tumaini la haki kwa njia ya imani.
Psaumes 130.5 Psaumes 62.5 Psaumes 25.5 1 Thessaloniciens 1.10 Romains 8.23-8.25
6 Maana katika Kristo Yesu kutahiriwa hakufai neno, wala kutokutahiriwa, bali imani itendayo kazi kwa upendo.
1 Thessaloniciens 1.3 Jacques 2.14-2.26 1 Jean 3.14-3.20 Matthieu 25.31-25.40 1 Corinthiens 7.19
7 Mlikuwa mkipiga mbio vizuri; ni nani aliyewazuia msiitii kweli?
1 Corinthiens 9.24 Galates 3.1 1 Pierre 1.22 Romains 6.17 Hébreux 12.1
8 Kushawishi huku hakukutoka kwake yeye anayewaita ninyi.
Galates 1.6 Romains 8.28
9 Chachu kidogo huchachua donge zima.
1 Corinthiens 15.33 1 Corinthiens 5.6-5.7 Marc 8.15 Luc 12.1 Luc 13.21
10 Nina matumaini kwenu katika Bwana, ya kwamba hamtakuwa na nia ya namna nyingine. Lakini yeye anayewafadhaisha atachukua hukumu yake, awaye yote.
Galates 1.7 Galates 5.12 2 Corinthiens 2.3 Galates 2.6 Galates 6.12-6.13
11 Nami, ndugu zangu ikiwa ninahubiri habari ya kutahiriwa, kwa nini ningali ninaudhiwa? Hapo kwazo la msalaba limebatilika!
1 Corinthiens 1.23 Galates 4.29 Galates 6.12 Actes 16.3 Galates 6.17
12 Laiti hao wanaowatia mashaka wangejikata nafsi zao!
Galates 5.10 Actes 15.1-15.2 Actes 5.9 Exode 30.33 Josué 7.12
13 Maana ninyi, ndugu, mliitwa mpate uhuru; lakini uhuru wenu usiwe sababu ya kuufuata mwili, bali tumikianeni kwa upendo.
1 Corinthiens 9.19 1 Pierre 2.16 1 Corinthiens 8.9 Galates 5.14 Romains 15.1-15.2
14 Maana torati yote imetimilika katika neno moja, nalo ni hili, Umpende jirani yako kama nafsi yako.
Matthieu 7.12 Lévitique 19.18 Matthieu 22.39-22.40 Galates 6.2 Romains 13.8-13.10
15 Lakini mkiumana na kulana, angalieni msije mkaangamizana.
1 Corinthiens 3.3 Galates 5.26 Jacques 3.14-4.3 Esaïe 9.20-9.21 2 Corinthiens 12.20
16 Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
Galates 5.24-5.25 Galates 5.19-5.21 Ephésiens 2.3 2 Corinthiens 7.1 Colossiens 3.5-3.10
17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.
Romains 8.5-8.8 Romains 8.13 Jean 3.6 Psaumes 119.20 Ecclésiaste 7.20
18 Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.
Romains 8.14 Romains 6.14-6.15 Romains 8.12 Psaumes 25.4-25.5 Psaumes 143.8-143.10
19 Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,
1 Corinthiens 6.9-6.10 1 Pierre 4.2-4.4 Matthieu 15.18-15.19 Colossiens 3.5-3.8 Apocalypse 21.8
20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
Actes 8.9-8.11 Apocalypse 21.8 Actes 16.16-16.19 1 Samuel 15.23 Deutéronome 18.10
21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.
Romains 13.13 1 Corinthiens 6.9-6.10 Romains 8.13 Colossiens 3.6 1 Corinthiens 5.11
22 Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,
Colossiens 3.12-3.17 1 Corinthiens 13.4-13.7 Jean 15.5 Ephésiens 5.9 Jean 15.2
23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.
1 Timothée 1.9 Actes 24.25 Tite 2.2 Tite 1.8 1 Corinthiens 9.25
24 Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake.
Romains 6.6 Romains 13.14 Romains 8.13 1 Corinthiens 3.23 1 Corinthiens 15.23
25 Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho.
Galates 5.16 Jean 6.63 2 Corinthiens 3.6 Romains 8.2 Romains 8.4-8.5
26 Tusijisifu bure, tukichokozana na kuhusudiana.
1 Corinthiens 3.7 Luc 14.10 Jacques 4.16 Jacques 3.14-3.16 Philippiens 2.1-2.3

Cette Bible est dans le domaine public.