Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Galates 5
Bible en Swahili de l’est


Une liberté à conserver

1 Katika ungwana huo Kristo alituandika huru; kwa hiyo simameni, wala msinaswe tena chini ya kongwa la utumwa.
2 Corinthiens 3.17 Galates 5.13 Jean 8.32-8.36 Galates 2.4 Romains 8.2
2 Tazama, mimi Paulo nawaambia ninyi ya kwamba, mkitahiriwa, Kristo hatawafaidia neno.
Galates 5.6 Galates 2.3-2.5 Romains 9.31-9.32 Galates 5.3-5.4 Actes 15.1
3 Tena namshuhudia kila mtu atahiriwaye, kwamba ni wajibu wake kuitimiza torati yote.
Galates 3.10 Jacques 2.10-2.11 Romains 2.25 Ephésiens 4.17 Luc 16.28
4 Mmetengwa na Kristo, ninyi mtakao kuhesabiwa haki kwa sheria; mmeanguka na kutoka katika hali ya neema.
Galates 2.21 2 Pierre 2.20-2.22 Romains 11.6 Romains 9.31-9.32 Galates 5.2
5 Maana sisi kwa Roho tunalitazamia tumaini la haki kwa njia ya imani.
1 Thessaloniciens 1.10 Romains 8.23-8.25 Genèse 49.18 Philippiens 3.9 Psaumes 130.5
6 Maana katika Kristo Yesu kutahiriwa hakufai neno, wala kutokutahiriwa, bali imani itendayo kazi kwa upendo.
Matthieu 25.31-25.40 1 Thessaloniciens 1.3 Jacques 2.14-2.26 1 Jean 3.14-3.20 1 Corinthiens 7.19
7 Mlikuwa mkipiga mbio vizuri; ni nani aliyewazuia msiitii kweli?
1 Corinthiens 9.24 Galates 3.1 1 Pierre 1.22 Hébreux 12.1 Romains 6.17
8 Kushawishi huku hakukutoka kwake yeye anayewaita ninyi.
Galates 1.6 Romains 8.28
9 Chachu kidogo huchachua donge zima.
1 Corinthiens 15.33 Luc 13.21 1 Corinthiens 5.6-5.7 Marc 8.15 Luc 12.1
10 Nina matumaini kwenu katika Bwana, ya kwamba hamtakuwa na nia ya namna nyingine. Lakini yeye anayewafadhaisha atachukua hukumu yake, awaye yote.
Galates 5.12 2 Corinthiens 2.3 Galates 1.7 Actes 15.24 Galates 2.4
11 Nami, ndugu zangu ikiwa ninahubiri habari ya kutahiriwa, kwa nini ningali ninaudhiwa? Hapo kwazo la msalaba limebatilika!
Galates 4.29 Galates 6.12 1 Corinthiens 1.23 Actes 22.21-22.22 Actes 21.28
12 Laiti hao wanaowatia mashaka wangejikata nafsi zao!
Galates 5.10 1 Corinthiens 5.13 Tite 3.10 Jean 9.34 Actes 15.24
13 Maana ninyi, ndugu, mliitwa mpate uhuru; lakini uhuru wenu usiwe sababu ya kuufuata mwili, bali tumikianeni kwa upendo.
1 Corinthiens 9.19 1 Pierre 2.16 1 Corinthiens 8.9 Galates 5.14 Romains 15.1-15.2
14 Maana torati yote imetimilika katika neno moja, nalo ni hili, Umpende jirani yako kama nafsi yako.
Matthieu 7.12 Lévitique 19.18 Matthieu 22.39-22.40 Galates 6.2 Romains 13.8-13.10
15 Lakini mkiumana na kulana, angalieni msije mkaangamizana.
1 Corinthiens 3.3 Jacques 3.14-4.3 Galates 5.26 Esaïe 11.13 1 Corinthiens 6.6-6.8
16 Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
Galates 5.24-5.25 Ephésiens 2.3 Galates 5.19-5.21 2 Corinthiens 7.1 Colossiens 3.5-3.10
17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.
Romains 8.5-8.8 Jean 3.6 Romains 8.13 Psaumes 51.10-51.12 Jacques 4.5-4.6
18 Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.
Romains 8.14 Romains 6.14-6.15 Galates 5.25 1 Jean 2.20-2.27 1 Timothée 1.9
19 Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,
1 Corinthiens 6.9-6.10 1 Pierre 4.2-4.4 Matthieu 15.18-15.19 Colossiens 3.5-3.8 Apocalypse 21.8
20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
Deutéronome 18.10 1 Corinthiens 11.19 Actes 8.9-8.11 Apocalypse 21.8 Actes 16.16-16.19
21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.
Romains 13.13 1 Corinthiens 6.9-6.10 Colossiens 3.6 1 Corinthiens 5.11 Romains 8.13
22 Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,
Colossiens 3.12-3.17 1 Corinthiens 13.4-13.7 Jean 15.5 Ephésiens 5.9 Jean 15.2
23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.
1 Timothée 1.9 Actes 24.25 Tite 1.8 Tite 2.2 1 Corinthiens 9.25
24 Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake.
Romains 6.6 Romains 13.14 Romains 8.13 Galates 5.16-5.18 Galates 3.29
25 Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho.
Galates 5.16 Jean 6.63 Romains 8.10 2 Corinthiens 3.6 Romains 8.2
26 Tusijisifu bure, tukichokozana na kuhusudiana.
Philippiens 2.1-2.3 Galates 5.15 1 Pierre 5.5 1 Corinthiens 3.7 Luc 14.10

Cette Bible est dans le domaine public.