1 Laiti mngechukuliana nami katika upumbavu wangu kidogo! Naam, mchukuliane nami.
2 Corinthiens 11.4  2 Corinthiens 11.19  2 Corinthiens 5.13  2 Corinthiens 11.21  2 Corinthiens 11.16-11.17  
 2 Maana nawaonea wivu, wivu wa Mungu; kwa kuwa naliwaposea mume mmoja, ili nimletee Kristo bikira safi.
Osée 2.19-2.20  Esaïe 54.5  Ephésiens 5.26-5.27  Jean 3.29  Lévitique 21.13-21.15  
 3 Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo.
1 Timothée 2.14  Apocalypse 12.9  Colossiens 2.4  Galates 1.6  Colossiens 2.8  
 4 Maana yeye ajaye akihubiri Yesu mwingine ambaye sisi hatukumhubiri, au mkipokea roho nyingine msiyoipokea, au injili nyingine msiyoikubali, mnatenda vema kuvumiliana naye!
1 Corinthiens 3.11  Galates 1.6-1.8  Romains 8.15  Ephésiens 4.4-4.5  Actes 4.12  
 5 Maana nadhani ya kuwa mimi sikupungukiwa na kitu walicho nacho mitume walio wakuu.
2 Corinthiens 12.11-12.12  Galates 2.6-2.9  1 Corinthiens 15.10  
 6 Lakini nijapokuwa mimi ni mtu asiyejua kunena, hii si hali yangu katika elimu; ila katika kila neno tumedhihirishwa kwenu.
Ephésiens 3.4  1 Corinthiens 1.17  2 Corinthiens 4.2  2 Corinthiens 5.11  2 Corinthiens 12.12  
 7 Je! Nalifanya dhambi kwa kunyenyekea ili ninyi mtukuzwe, kwa sababu naliwahubiri Injili ya Mungu bila ujira?
2 Corinthiens 12.13  2 Thessaloniciens 3.8  1 Thessaloniciens 2.9  2 Corinthiens 10.1  1 Corinthiens 9.6  
 8 Naliwanyang’anya makanisa mengine mali yao, nikitwaa posho langu ili niwahudumie ninyi.
2 Corinthiens 11.9  Philippiens 4.14-4.16  Philippiens 4.18  
 9 Nami nilipokuwa pamoja nanyi na kuhitaji sikumlemea mtu. Maana hao ndugu waliokuja kutoka Makedonia walinipa kadiri ya mahitaji yangu; nami katika mambo yote najilinda nafsi yangu nisiwalemee hata kidogo; tena najilinda.
1 Thessaloniciens 2.6  1 Thessaloniciens 2.9  2 Corinthiens 12.13-12.16  2 Thessaloniciens 3.8-3.9  Philippiens 4.10-4.16  
 10 Kama vile ile kweli ya Kristo ilivyo ndani yangu, hakuna mtu atakayenifumba kinywa katika kujisifu huku, katika mipaka ya Akaya.
Romains 9.1  Actes 18.12  Romains 1.9  2 Corinthiens 1.23  2 Corinthiens 11.31  
 11 Kwa nini? Je! Ni kwa sababu siwapendi ninyi? Mungu anajua.
2 Corinthiens 12.15  2 Corinthiens 6.11-6.12  2 Corinthiens 7.3  Apocalypse 2.23  Jean 2.24-2.25  
 12 Lakini nifanyalo nitalifanya, ili niwapinge hao watafutao nafasi wasipate nafasi; ili kwamba katika neno hilo wajisifialo waonekane kuwa kama sisi.
1 Corinthiens 9.12  2 Corinthiens 11.9  Galates 6.13-6.14  Galates 1.7  1 Corinthiens 5.6  
 13 Maana watu kama hao ni mitume wa uongo, watendao kazi kwa hila, wanaojigeuza wawe mfano wa mitume wa Kristo.
Apocalypse 2.2  Philippiens 3.2  Galates 2.4  Galates 1.7  1 Jean 4.1  
 14 Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.
Galates 1.8  Apocalypse 12.9  2 Corinthiens 2.11  2 Corinthiens 11.3  Genèse 3.1-3.5  
 15 Basi si neno kubwa watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa watumishi wa haki, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao.
Philippiens 3.19  Jérémie 23.14-23.15  Jude 1.4  2 Corinthiens 3.9  2 Thessaloniciens 2.8-2.12  
 16 Nasema tena, mtu asidhani ya kuwa mimi ni mpumbavu; lakini mjaponidhania hivi, mnikubali kama mpumbavu; ili mimi nami nipate kujisifu ngaa kidogo.
2 Corinthiens 11.1  2 Corinthiens 12.6  2 Corinthiens 11.21-11.23  2 Corinthiens 11.19  2 Corinthiens 12.11  
 17 Ninenalo silineni agizo la Bwana, bali kama kwa upumbavu, katika ujasiri huu wa kujisifu.
1 Corinthiens 7.12  2 Corinthiens 9.4  Philippiens 3.3-3.6  1 Corinthiens 7.6  1 Corinthiens 7.25  
 18 Kwa sababu wengi wanajisifu kwa jinsi ya mwili, mimi nami nitajisifu.
Jérémie 9.23-9.24  Philippiens 3.3-3.4  2 Corinthiens 12.11  1 Pierre 1.24  2 Corinthiens 12.5-12.6  
 19 Ninyi, kwa kuwa mna akili, mnachukuliana na wajinga kwa furaha.
1 Corinthiens 4.10  1 Corinthiens 8.1  1 Corinthiens 10.15  Apocalypse 3.17  
 20 Maana mwachukuliana na mtu akiwatia utumwani, akiwameza, akiwateka nyara, akijikuza, akiwapiga usoni.
Galates 2.4  Galates 5.1  Galates 4.3  Galates 4.9  2 Corinthiens 1.24  
 21 Nanena kwa jinsi ya kujidhili kana kwamba sisi tulikuwa dhaifu. Walakini, akiwa mtu anao ujasiri kwa lo lote, (nanena kipuuzi), mimi nami ninao ujasiri.
2 Corinthiens 10.10  2 Corinthiens 10.1-10.2  2 Corinthiens 11.22-11.27  2 Corinthiens 11.17  2 Corinthiens 13.10  
 22 Wao ni Waebrania? Na mimi pia. Wao ni Waisraeli? Na mimi pia. Wao ni uzao wa Ibrahimu? Na mimi pia.
Philippiens 3.5  Romains 11.1  Romains 9.4  2 Chroniques 20.7  Jean 8.33-8.39  
 23 Wao ni wahudumu wa Kristo? (Nanena kiwazimu), mimi ni zaidi; katika taabu kuzidi sana; katika vifungo kuzidi sana; katika mapigo kupita kiasi; katika mauti mara nyingi.
1 Corinthiens 15.10  2 Corinthiens 6.4-6.5  Actes 9.16  2 Corinthiens 3.6  1 Corinthiens 3.5  
 24 Kwa Wayahudi mara tano nalipata mapigo arobaini kasoro moja.
Deutéronome 25.2-25.3  Marc 13.9  Matthieu 10.17  
 25 Mara tatu nalipigwa kwa bakora; mara moja nalipigwa kwa mawe; mara tatu nalivunjikiwa jahazi; kuchwa kucha nimepata kukaa kilindini;
Actes 14.19  Matthieu 21.35  Actes 14.5  Hébreux 11.37  Actes 16.22-16.23  
 26 katika kusafiri mara nyingi; hatari za mito; hatari za wanyang’anyi; hatari kwa taifa langu; hatari kwa mataifa mengine; hatari za mjini; hatari za jangwani; hatari za baharini; hatari kwa ndugu za uongo;
Actes 14.5  Actes 20.19  Actes 17.5  Actes 13.50  Actes 25.3  
 27 katika taabu na masumbufu; katika kukesha mara nyingi; katika njaa na kiu; katika kufunga mara nyingi; katika baridi na kuwa uchi.
2 Corinthiens 6.5  Philippiens 4.12  2 Thessaloniciens 3.8  1 Thessaloniciens 2.9  1 Corinthiens 4.11-4.12  
 28 Baghairi ya mambo ya nje, yako yanijiayo kila siku, ndiyo maangalizi ya makanisa yote.
Actes 20.2  Actes 20.18-20.35  Romains 1.14  Romains 16.4  Actes 18.23  
 29 Ni nani aliye dhaifu, nisiwe dhaifu nami? Ni nani aliyekwazwa nami nisichukiwe?
1 Corinthiens 8.13  1 Corinthiens 9.22  2 Corinthiens 13.9  2 Corinthiens 7.5-7.6  Néhémie 5.6-5.13  
 30 Ikinibidi kujisifu, nitajisifia mambo ya udhaifu wangu.
1 Corinthiens 2.3  2 Corinthiens 12.5-12.11  Proverbes 25.27  Colossiens 1.24  2 Corinthiens 11.16-11.18  
 31 Mungu, Baba wa Bwana Yesu, aliye mtukufu hata milele, anajua ya kuwa sisemi uongo.
Romains 9.5  Romains 1.25  Jean 10.30  Ephésiens 1.3  1 Timothée 1.17  
 32 Huko Dameski liwali wa mfalme Areta alikuwa akiulinda mji wa Wadameski, ili kunikamata;
Actes 9.24-9.25  2 Corinthiens 11.26  
 33 nami nikatelemshwa ndani ya kapu, katika dirisha la ukutani, nikaokoka katika mikono yake.Actes 9.25  1 Samuel 19.12  Josué 2.18