Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Corinthiens 11.26
Bible en Swahili de l’est


Comparaison entre Paul et les prétendus apôtres

1 Laiti mngechukuliana nami katika upumbavu wangu kidogo! Naam, mchukuliane nami.
2 Corinthiens 11.4 2 Corinthiens 11.19 2 Corinthiens 5.13 2 Corinthiens 11.16-11.17 2 Corinthiens 11.21
2 Maana nawaonea wivu, wivu wa Mungu; kwa kuwa naliwaposea mume mmoja, ili nimletee Kristo bikira safi.
Osée 2.19-2.20 Esaïe 54.5 Jean 3.29 Ephésiens 5.26-5.27 Ezéchiel 44.22
3 Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo.
Apocalypse 12.9 1 Timothée 2.14 Jean 8.44 Colossiens 2.4 Galates 1.6
4 Maana yeye ajaye akihubiri Yesu mwingine ambaye sisi hatukumhubiri, au mkipokea roho nyingine msiyoipokea, au injili nyingine msiyoikubali, mnatenda vema kuvumiliana naye!
Galates 1.6-1.8 1 Corinthiens 3.11 1 Corinthiens 12.4-12.11 1 Timothée 2.5 Romains 8.15
5 Maana nadhani ya kuwa mimi sikupungukiwa na kitu walicho nacho mitume walio wakuu.
2 Corinthiens 12.11-12.12 Galates 2.6-2.9 1 Corinthiens 15.10
6 Lakini nijapokuwa mimi ni mtu asiyejua kunena, hii si hali yangu katika elimu; ila katika kila neno tumedhihirishwa kwenu.
Ephésiens 3.4 1 Corinthiens 1.17 2 Corinthiens 4.2 2 Corinthiens 5.11 2 Corinthiens 12.12
7 Je! Nalifanya dhambi kwa kunyenyekea ili ninyi mtukuzwe, kwa sababu naliwahubiri Injili ya Mungu bila ujira?
2 Corinthiens 12.13 1 Corinthiens 9.14-9.18 1 Corinthiens 9.12 1 Corinthiens 4.10-4.12 2 Thessaloniciens 3.8
8 Naliwanyang’anya makanisa mengine mali yao, nikitwaa posho langu ili niwahudumie ninyi.
2 Corinthiens 11.9 Philippiens 4.14-4.16 Philippiens 4.18
9 Nami nilipokuwa pamoja nanyi na kuhitaji sikumlemea mtu. Maana hao ndugu waliokuja kutoka Makedonia walinipa kadiri ya mahitaji yangu; nami katika mambo yote najilinda nafsi yangu nisiwalemee hata kidogo; tena najilinda.
1 Thessaloniciens 2.6 Philippiens 4.10-4.16 1 Thessaloniciens 2.9 2 Corinthiens 12.13-12.16 2 Thessaloniciens 3.8-3.9
10 Kama vile ile kweli ya Kristo ilivyo ndani yangu, hakuna mtu atakayenifumba kinywa katika kujisifu huku, katika mipaka ya Akaya.
Romains 9.1 Romains 1.9 Actes 18.12 2 Corinthiens 1.23 Romains 16.5
11 Kwa nini? Je! Ni kwa sababu siwapendi ninyi? Mungu anajua.
2 Corinthiens 12.15 2 Corinthiens 6.11-6.12 2 Corinthiens 7.3 2 Corinthiens 11.31 Actes 15.8
12 Lakini nifanyalo nitalifanya, ili niwapinge hao watafutao nafasi wasipate nafasi; ili kwamba katika neno hilo wajisifialo waonekane kuwa kama sisi.
1 Corinthiens 9.12 2 Corinthiens 10.17 1 Timothée 5.14 Philippiens 1.15-1.30 2 Corinthiens 11.9
13 Maana watu kama hao ni mitume wa uongo, watendao kazi kwa hila, wanaojigeuza wawe mfano wa mitume wa Kristo.
Apocalypse 2.2 Philippiens 3.2 Galates 2.4 Galates 1.7 1 Jean 4.1
14 Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.
Galates 1.8 2 Corinthiens 11.3 Apocalypse 12.9 2 Corinthiens 2.11 Matthieu 4.1-4.10
15 Basi si neno kubwa watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa watumishi wa haki, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao.
Philippiens 3.19 2 Corinthiens 3.9 Jérémie 23.14-23.15 Jude 1.4 2 Pierre 2.13-2.22
16 Nasema tena, mtu asidhani ya kuwa mimi ni mpumbavu; lakini mjaponidhania hivi, mnikubali kama mpumbavu; ili mimi nami nipate kujisifu ngaa kidogo.
2 Corinthiens 11.1 2 Corinthiens 12.6 2 Corinthiens 11.21-11.23 2 Corinthiens 11.19 2 Corinthiens 12.11
17 Ninenalo silineni agizo la Bwana, bali kama kwa upumbavu, katika ujasiri huu wa kujisifu.
1 Corinthiens 7.12 2 Corinthiens 9.4 1 Corinthiens 7.25 2 Corinthiens 11.18-11.27 Philippiens 3.3-3.6
18 Kwa sababu wengi wanajisifu kwa jinsi ya mwili, mimi nami nitajisifu.
1 Corinthiens 4.10 2 Corinthiens 12.9 2 Corinthiens 10.12-10.18 Jérémie 9.23-9.24 Philippiens 3.3-3.4
19 Ninyi, kwa kuwa mna akili, mnachukuliana na wajinga kwa furaha.
1 Corinthiens 4.10 1 Corinthiens 8.1 1 Corinthiens 10.15 Apocalypse 3.17
20 Maana mwachukuliana na mtu akiwatia utumwani, akiwameza, akiwateka nyara, akijikuza, akiwapiga usoni.
Galates 2.4 Galates 4.9 Galates 5.1 Galates 4.3 2 Corinthiens 1.24
21 Nanena kwa jinsi ya kujidhili kana kwamba sisi tulikuwa dhaifu. Walakini, akiwa mtu anao ujasiri kwa lo lote, (nanena kipuuzi), mimi nami ninao ujasiri.
2 Corinthiens 10.10 2 Corinthiens 11.17 2 Corinthiens 10.1-10.2 2 Corinthiens 11.22-11.27 Philippiens 3.3-3.6
22 Wao ni Waebrania? Na mimi pia. Wao ni Waisraeli? Na mimi pia. Wao ni uzao wa Ibrahimu? Na mimi pia.
Philippiens 3.5 Romains 11.1 Romains 9.4 Actes 22.3 Exode 7.16
23 Wao ni wahudumu wa Kristo? (Nanena kiwazimu), mimi ni zaidi; katika taabu kuzidi sana; katika vifungo kuzidi sana; katika mapigo kupita kiasi; katika mauti mara nyingi.
1 Corinthiens 15.10 2 Corinthiens 6.4-6.5 Actes 9.16 2 Corinthiens 3.6 2 Corinthiens 6.9
24 Kwa Wayahudi mara tano nalipata mapigo arobaini kasoro moja.
Deutéronome 25.2-25.3 Marc 13.9 Matthieu 10.17
25 Mara tatu nalipigwa kwa bakora; mara moja nalipigwa kwa mawe; mara tatu nalivunjikiwa jahazi; kuchwa kucha nimepata kukaa kilindini;
Actes 14.19 Actes 16.33 Actes 27.1-27.44 Matthieu 21.35 Actes 14.5
26 katika kusafiri mara nyingi; hatari za mito; hatari za wanyang’anyi; hatari kwa taifa langu; hatari kwa mataifa mengine; hatari za mjini; hatari za jangwani; hatari za baharini; hatari kwa ndugu za uongo;
Actes 14.5 Actes 25.3 Actes 20.19 Actes 17.5 Actes 13.50
27 katika taabu na masumbufu; katika kukesha mara nyingi; katika njaa na kiu; katika kufunga mara nyingi; katika baridi na kuwa uchi.
2 Corinthiens 6.5 2 Thessaloniciens 3.8 1 Thessaloniciens 2.9 Philippiens 4.12 1 Corinthiens 4.11-4.12
28 Baghairi ya mambo ya nje, yako yanijiayo kila siku, ndiyo maangalizi ya makanisa yote.
Actes 15.40-15.41 Colossiens 2.1 Romains 11.13 Actes 20.2 Actes 20.18-20.35
29 Ni nani aliye dhaifu, nisiwe dhaifu nami? Ni nani aliyekwazwa nami nisichukiwe?
1 Corinthiens 9.22 1 Corinthiens 8.13 Nombres 25.6-25.11 Apocalypse 3.15-3.18 1 Corinthiens 6.15-6.18
30 Ikinibidi kujisifu, nitajisifia mambo ya udhaifu wangu.
1 Corinthiens 2.3 2 Corinthiens 12.5-12.11 2 Corinthiens 12.1 Proverbes 27.2 Proverbes 25.27
31 Mungu, Baba wa Bwana Yesu, aliye mtukufu hata milele, anajua ya kuwa sisemi uongo.
Romains 9.5 Ephésiens 1.3 Romains 1.25 Jean 10.30 Ephésiens 3.14
32 Huko Dameski liwali wa mfalme Areta alikuwa akiulinda mji wa Wadameski, ili kunikamata;
Actes 9.24-9.25 2 Corinthiens 11.26
33 nami nikatelemshwa ndani ya kapu, katika dirisha la ukutani, nikaokoka katika mikono yake.
Actes 9.25 1 Samuel 19.12 Josué 2.18

Cette Bible est dans le domaine public.