Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Corinthiens 6.11
Bible en Swahili de l’est


Scandale des procès entre chrétiens

1 Je! Mtu wa kwenu akiwa ana daawa juu ya mwenzake athubutu kushitaki mbele ya wasio haki, wala si mbele ya watakatifu?
Actes 18.14-18.15 Actes 19.38 1 Corinthiens 16.1 Matthieu 18.15-18.17 1 Corinthiens 14.33
2 Au hamjui ya kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu utahukumiwa na ninyi, je! Hamstahili kukata hukumu zilizo ndogo?
Matthieu 19.28 Apocalypse 20.4 Luc 22.30 Apocalypse 3.21 Apocalypse 2.26-2.27
3 Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika, basi si zaidi sana mambo ya maisha haya?
Luc 8.14 Matthieu 25.41 Jude 1.6 Luc 21.34 1 Corinthiens 6.4
4 Basi, mkiwa na mahali panapohukumiwa mambo ya maisha haya, mwawaweka kuwa waamuzi hao waliohesabiwa kuwa si kitu; katika kanisa?
1 Corinthiens 5.12 Actes 6.2-6.4
5 Nasema hayo nipate kuwatahayarisha. Je! Ndivyo, kwamba kwenu hakuna hata mtu mmoja mwenye hekima, awezaye kukata maneno ya ndugu zake?
1 Corinthiens 4.14 1 Corinthiens 15.34 Jacques 3.13-3.18 Proverbes 14.8 1 Corinthiens 3.18
6 Bali mwashitakiana, ndugu kwa ndugu, tena mbele yao wasioamini.
1 Jean 3.11-3.15 Actes 7.26 Genèse 45.24 1 Corinthiens 6.7 Psaumes 133.1-133.3
7 Basi imekuwa upungufu kwenu kabisa kwamba mnashitakiana ninyi kwa ninyi. Maana si afadhali kudhulumiwa? Maana si afadhali kunyang’anywa mali zenu?
Proverbes 20.22 1 Pierre 3.9 1 Pierre 2.19-2.23 Jacques 4.1-4.3 Romains 12.17-12.19
8 Bali kinyume cha hayo ninyi wenyewe mwadhulumu watu na kunyang’anya mali zao; naam, hata za ndugu zenu.
1 Thessaloniciens 4.6 Marc 10.19 Colossiens 3.25 Malachie 3.5 Michée 2.2
9 Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,
1 Timothée 1.9-1.10 Lévitique 20.13 Ephésiens 5.4-5.5 Lévitique 18.22 Galates 5.19-5.21
10 wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi.
1 Corinthiens 5.11 Galates 5.21 Ezéchiel 22.27 Matthieu 23.33 Ezéchiel 22.29
11 Na baadhi yenu mlikuwa watu wa namna hii; lakini mlioshwa, lakini mlitakaswa, lakini mlihesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu Kristo, na katika Roho wa Mungu wetu.
1 Corinthiens 1.2 Ephésiens 5.26 Hébreux 10.22 Actes 22.16 1 Corinthiens 12.2

Liberté chrétienne et appartenance à Christ

12 Vitu vyote ni halali kwangu, lakini si vyote vifaavyo; vitu vyote ni halali kwangu, lakini mimi sitatiwa chini ya uwezo wa kitu cho chote.
1 Corinthiens 10.23-10.33 1 Corinthiens 9.27 Romains 14.14-14.23 1 Corinthiens 8.7-8.13 Hébreux 12.15-12.16
13 Vyakula ni kwa tumbo, na tumbo ni kwa vyakula; lakini Mungu atavitowesha vyote viwili, tumbo na vyakula. Lakini mwili si kwa zinaa, bali ni kwa Bwana, naye Bwana ni kwa mwili.
1 Corinthiens 6.19 Matthieu 15.17 1 Corinthiens 6.15 1 Corinthiens 3.16 Romains 6.12
14 Naye Mungu alimfufua Bwana, na tena atatufufua sisi kwa uweza wake.
Actes 2.24 Ephésiens 1.19-1.20 Jean 6.39-6.40 Philippiens 3.10-3.11 1 Corinthiens 15.15-15.20
15 Je! Hamjui ya kuwa miili yenu ni viungo vya Kristo? Basi nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya kahaba? Hasha!
Romains 12.5 1 Corinthiens 12.27 Ephésiens 5.30 Ephésiens 4.15-4.16 Ephésiens 4.12
16 Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja.
Genèse 2.24 Ephésiens 5.31 Marc 10.8 Matthieu 19.5-19.6 Juges 16.1
17 Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye.
Jean 17.21-17.23 1 Corinthiens 12.13 Jean 3.6 Ephésiens 4.3-4.4 Galates 2.20
18 Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe.
Hébreux 13.4 Colossiens 3.5 1 Thessaloniciens 4.3 Romains 6.12-6.13 1 Corinthiens 6.9
19 Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;
1 Corinthiens 3.16 2 Corinthiens 6.16 1 Pierre 2.5 Ephésiens 2.21-2.22 Jean 2.21
20 maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu.
1 Corinthiens 7.23 Romains 12.1 1 Pierre 2.9 1 Pierre 1.18 Actes 20.28

Cette Bible est dans le domaine public.