Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Corinthiens 1.20
Bible en Swahili de l’est


Discordes et désordres dans l’Église Salutation et louange

1 Paulo, aliyeitwa kuwa mtume wa Yesu Kristo kwa mapenzi ya Mungu, na Sosthene ndugu yetu,
Romains 1.1 2 Corinthiens 1.1 Ephésiens 1.1 Actes 18.17 Actes 1.25-1.26
2 kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, wale waliotakaswa katika Kristo Yesu, walioitwa wawe watakatifu, pamoja na wote wanaoliitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo kila mahali, Bwana wao na wetu.
Romains 1.7 Actes 18.1 1 Corinthiens 1.30 Actes 9.14 Hébreux 13.12
3 Neema na iwe kwenu na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana Yesu Kristo.
Romains 1.7 2 Corinthiens 1.2 Ephésiens 1.2 1 Pierre 1.2
4 Namshukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu, kwa sababu ya neema ya Mungu mliyopewa katika Kristo Yesu;
Romains 1.8 Jean 14.16 Jean 14.26 Jean 15.26 1 Timothée 1.14
5 kwa kuwa katika kila jambo mlitajirika katika yeye, katika maneno yote, na maarifa yote;
2 Corinthiens 8.7 2 Corinthiens 9.11 Philippiens 1.9 1 Corinthiens 12.8 Romains 15.14
6 kama ushuhuda wa Kristo ulivyothibitika kwenu;
Apocalypse 1.2 2 Timothée 1.8 1 Timothée 2.6 2 Thessaloniciens 1.10 Actes 23.11
7 hata hamkupungukiwa na karama yo yote, mkikutazamia sana kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo;
Philippiens 3.20 2 Pierre 3.12 Romains 8.19 Luc 17.30 Hébreux 9.28
8 ambaye atawathibitisha hata mwisho, ili msilaumiwe siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo.
1 Thessaloniciens 3.13 Philippiens 1.6 1 Thessaloniciens 5.23-5.24 2 Thessaloniciens 3.3 Colossiens 1.22
9 Mungu ni mwaminifu ambaye mliitwa na yeye mwingie katika ushirika wa Mwanawe, Yesu Kristo Bwana wetu.
2 Thessaloniciens 3.3 Esaïe 49.7 Deutéronome 7.9 1 Jean 1.3 Romains 8.28

Rivalités humaines et sagesse divine

10 Basi ndugu, nawasihi, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba nyote mnene mamoja; wala pasiwe kwenu faraka, bali mhitimu katika nia moja na shauri moja.
Philippiens 2.1-2.4 Ephésiens 4.1-4.7 Philippiens 1.27 Psaumes 133.1 Jacques 3.13-3.18
11 Kwa maana, ndugu zangu, nimearifiwa habari zenu na wale walio wa nyumbani mwa Kloe, ya kwamba iko fitina kwenu.
1 Corinthiens 3.3 Galates 5.15 2 Corinthiens 12.20 Jacques 4.1-4.2 1 Corinthiens 6.1-6.7
12 Basi, maana yangu ni hii, ya kwamba kila mtu wa kwenu kusema, Mimi ni wa Paulo, na, Mimi ni wa Apolo, na, Mimi ni wa Kefa, na, Mimi ni wa Kristo.
Jean 1.42 1 Corinthiens 3.21-3.23 1 Corinthiens 9.5 2 Corinthiens 9.6 Actes 18.24-19.1
13 Je! Kristo amegawanyika? Je! Paulo alisulibiwa kwa ajili yenu? Au je! Mlibatizwa kwa jina la Paulo?
Actes 2.38 Ephésiens 4.5 Matthieu 28.19 2 Corinthiens 11.4 Actes 10.48
14 Nashukuru, kwa sababu sikumbatiza mtu kwenu, ila Krispo na Gayo;
Actes 18.8 Romains 16.23 2 Corinthiens 2.14 Philémon 1.4 1 Timothée 1.12
15 mtu asije akasema kwamba mlibatizwa kwa jina langu.
2 Corinthiens 11.2 Jean 3.28-3.29 Jean 7.18
16 Tena naliwabatiza watu wa nyumbani mwa Stefana; zaidi ya hao, sijui kama nalimbatiza mtu ye yote mwingine.
1 Corinthiens 16.15 1 Corinthiens 16.17 Actes 16.33 Actes 16.15
17 Maana Kristo hakunituma ili nibatize, bali niihubiri Habari Njema; wala si kwa hekima ya maneno, msalaba wa Kristo usije ukabatilika.
1 Corinthiens 2.1 1 Corinthiens 2.13 2 Corinthiens 10.10 Jean 4.2 1 Corinthiens 2.4-2.5
18 Kwa sababu neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuzi, bali kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu.
1 Corinthiens 2.14 1 Corinthiens 1.23-1.25 2 Corinthiens 4.3 2 Thessaloniciens 2.10 Romains 1.16
19 Kwa kuwa imeandikwa, Nitaiharibu hekima yao wenye hekima, Na akili zao wenye akili nitazikataa.
Esaïe 29.14 Jérémie 8.9 1 Corinthiens 3.19 Job 5.12-5.13 Esaïe 19.11
20 Yu wapi mwenye hekima? Yu wapi mwandishi? Yu wapi mlete hoja wa zamani hizi? Je! Mungu hakuifanya hekima ya dunia kuwa ni upumbavu?
Romains 1.22 Job 12.17 Esaïe 44.25 Esaïe 33.18 2 Samuel 16.23
21 Kwa maana katika hekima ya Mungu, dunia isipopata kumjua Mungu kwa hekima yake, Mungu alipenda kuwaokoa waaminio kwa upuzi wa lile neno linalohubiriwa.
Luc 10.21 Matthieu 11.25 Romains 1.28 1 Corinthiens 1.24 Daniel 2.20
22 Kwa sababu Wayahudi wanataka ishara, na Wayunani wanatafuta hekima;
Actes 17.18-17.21 Matthieu 12.38-12.39 Jean 2.18 Luc 11.16 Matthieu 16.1-16.4
23 bali sisi tunamhubiri Kristo, aliyesulibiwa; kwa Wayahudi ni kikwazo, na kwa Wayunani ni upuzi;
1 Corinthiens 2.14 1 Pierre 2.8 Galates 5.11 1 Corinthiens 2.2 Luc 2.34
24 bali kwao waitwao, Wayahudi kwa Wayunani, ni Kristo, nguvu ya Mungu, na hekima ya Mungu.
1 Corinthiens 1.30 Colossiens 2.3 Romains 8.28-8.30 1 Corinthiens 1.18 1 Corinthiens 1.9
25 Kwa sababu upumbavu wa Mungu una hekima zaidi ya wanadamu, na udhaifu wa Mungu una nguvu zaidi ya wanadamu.
1 Corinthiens 1.18 2 Corinthiens 13.4 1 Corinthiens 1.27-1.29 Romains 11.33-11.36 Josué 6.2-6.5
26 Maana, ndugu zangu, angalieni mwito wenu, ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa;
1 Corinthiens 1.20 1 Corinthiens 3.18-3.20 Jacques 2.5 Actes 13.7 Jean 19.38-19.39
27 bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu;
Jacques 2.5 1 Corinthiens 1.20 Psaumes 8.2 Esaïe 29.14 Matthieu 11.25
28 tena Mungu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, naam, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko;
Romains 4.17 Job 34.24 Job 34.19-34.20 Psaumes 37.35-37.36 Esaïe 2.17
29 mwenye mwili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu.
Ephésiens 2.9 Romains 15.17 Jérémie 9.23 1 Corinthiens 4.7 Romains 3.19
30 Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanywa kwetu hekima itokayo kwa Mungu, na haki, na utakatifu, na ukombozi;
1 Corinthiens 1.2 Ephésiens 1.7 Romains 8.1 Philippiens 3.9 Colossiens 1.14
31 kusudi, kama ilivyoandikwa, Yeye aonaye fahari na aone fahari juu ya Bwana.
2 Corinthiens 10.17 Jérémie 9.23-9.24 Philippiens 3.3 Jérémie 4.2 Esaïe 41.16

Cette Bible est dans le domaine public.