Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Actes 24.12
Bible en Swahili de l’est


Paul devant le gouverneur Félix

1 Baada ya siku tano, Anania, Kuhani Mkuu, akatelemka na baadhi ya wazee pamoja naye, na msemi mmoja, Tertulo, nao wakamweleza liwali habari za Paulo.
Actes 23.2 Actes 24.11 Actes 25.2 Actes 21.27 Actes 23.30
2 Naye alipoitwa, Tertulo akaanza kumshitaki, akisema, Kwa kuwa mnapata amani nyingi chini yako, Feliki mtukufu, na kwa maangalizi yako mambo mabaya yanatengenezwa kwa ajili ya taifa hili,
Proverbes 29.5 Psaumes 12.2-12.3 Proverbes 26.28 Actes 24.26-24.27 Jude 1.16
3 basi tunayapokea kila wakati na kila mahali, kwa shukrani yote.
Actes 26.25 Actes 23.26 Luc 1.3
4 Lakini nisikuudhi zaidi, nakusihi utusikilize maneno machache kwa fadhili zako.
Hébreux 11.32
5 Kwa maana tumemwona mtu huyu mkorofi, mwanzilishi wa fitina katika Wayahudi wote duniani, tena ni kichwa cha madhehebu ya Wanazorayo.
Actes 28.22 Actes 24.14 Actes 15.5 Actes 26.5 Actes 16.20-16.21
6 Na tena alijaribu kulitia hekalu unajisi; tukamkamata; [tukataka kumhukumu kwa sheria yetu.
Jean 19.7-19.8 Actes 23.10-23.15 Jean 18.31 Actes 19.37 Actes 24.12
7 Lakini Lisia jemadari akafika akamwondoa mikononi mwetu kwa nguvu,
8 Akawaamuru wale waliomshitaki waje kwako.] Wewe mwenyewe kwa kumwuliza-uliza utaweza kupata habari ya mambo yale yote tunayomshitaki sisi.
Actes 23.35 Actes 25.15-25.16 Actes 25.5 Actes 23.30
9 Wayahudi nao wakamshitaki, wakisema ya kuwa ndivyo yalivyo.
Michée 6.12-6.13 Michée 7.2-7.3 Psaumes 4.2 Psaumes 64.2-64.8 Jérémie 9.3-9.6
10 Na liwali alipompungia mkono ili anene, Paulo akajibu, Kwa kuwa ninajua ya kwamba wewe umekuwa mwamuzi wa taifa hili kwa muda wa miaka mingi, najitetea mwenyewe kwa moyo wa furaha.
Luc 12.14 Actes 21.40 Actes 26.1 Actes 13.16 Actes 19.33
11 Maana waweza kujua ya kuwa hazijapita siku zaidi ya kumi na mbili tangu nilipopanda kwenda Yerusalemu ili kuabudu.
Actes 24.1 Actes 21.18 Actes 22.30 Actes 23.11 Actes 23.23
12 Watu hawa hawakuniona ndani ya hekalu, nikihojiana na mtu, au kufanya fujo katika mkutano, wala katika masinagogi wala ndani ya mji.
Actes 25.8 Actes 24.18 Actes 28.17 Actes 24.5
13 Wala hawawezi kuyahakikisha mambo haya wanayonishitaki sasa.
Actes 25.7 1 Pierre 3.16
14 Ila neno hili naungama kwako ya kwamba kwa Njia ile ambayo waiita uzushi, ndivyo ninavyomwabudu Mungu wa baba zetu, nikiyaamini yote yanayopatana na torati na yaliyoandikwa katika vyuo vya manabii.
Actes 3.13 Actes 9.2 Actes 26.22 Actes 24.5 Actes 28.23
15 Nina tumaini kwa Mungu, ambalo hata hao nao wanalitazamia, ya kwamba kutakuwa na ufufuo wa wafu, wenye haki na wasio haki pia.
Daniel 12.2 1 Thessaloniciens 4.14-4.16 Jean 5.28-5.29 Apocalypse 20.12-20.13 Actes 23.6-23.8
16 Nami ninajizoeza katika neno hili niwe na dhamiri isiyo na hatia mbele za Mungu na mbele ya watu siku zote.
Actes 23.1 1 Timothée 1.5 2 Corinthiens 4.2 Tite 2.11-2.13 Hébreux 9.14
17 Baada ya miaka mingi nalifika niwaletee watu wa taifa langu sadaka na matoleo.
Galates 2.10 2 Corinthiens 8.1-8.4 Actes 20.16 Romains 15.25-15.28 Actes 11.29-11.30
18 Wakaniona ndani ya hekalu nikishughulika na mambo haya, hali nimetakaswa, wala sikuwa na mkutano wala ghasia; lakini walikuwako baadhi ya Wayahudi waliotoka Asia,
Actes 26.21 Actes 21.26-21.30 Actes 24.12
19 ambao imewapasa hao kuwapo hapa mbele yako na kunishitaki, kama wana neno lo lote juu yangu.
Actes 23.30 Actes 25.16
20 Au watu hawa wenyewe na waseme, ni kosa gani waliloliona kwangu niliposimama mbele ya baraza,
21 isipokuwa kwa ajili ya sauti hii moja, nilipolia nikisimama katikati yao, na kusema, Kwa ajili ya ufufuo wa wafu ninahukumiwa mbele yenu hivi leo.
Actes 23.6 Actes 26.6-26.8 Actes 28.20 Actes 4.2
22 Basi Feliki aliwaahirisha, kwa sababu alijua habari za Njia ile kwa usahihi zaidi, akasema, Lisia jemadari atakapotelemka nitakata maneno yenu.
Actes 24.6 Actes 24.24 Actes 25.26 Actes 26.3 Actes 24.10
23 Akamwamuru yule akida kwamba Paulo alindwe; ila awe na nafasi, wala asimkataze mmojawapo wa rafiki zake kumtumikia.
Actes 27.3 Actes 28.16 Actes 23.16 Actes 21.8-21.14 Actes 24.26
24 Baada ya siku kadha wa kadha, Feliki akafika pamoja na Drusila mkewe aliyekuwa Myahudi, akatuma kumwita Paulo akamsikiliza habari za imani iliyo kwa Kristo Yesu.
Actes 20.21 Galates 2.16 Luc 23.8 Marc 6.20 Actes 26.22
25 Na Paulo alipokuwa akitoa hoja zake katika habari ya haki, na kuwa na kiasi, na hukumu itakayokuja, Feliki akafanya hofu akajibu, Sasa enenda zako, nami nikipata nafasi nitakuita.
Galates 5.23 2 Pierre 1.6 Actes 10.42 Jérémie 37.17-37.21 Actes 24.15
26 Pamoja na hayo alitaraji kwamba atapewa fedha na Paulo; kwa hiyo alimwita mara nyingi akaongea naye.
Ezéchiel 33.31 Job 15.34 Proverbes 17.23 Amos 2.6-2.7 Exode 23.8
27 Na miaka miwili ilipotimia, Feliki akampokea Porkio Festo atawale badala yake. Na Feliki, akitaka kuwafanyia Wayahudi fadhili, akamwacha Paulo amefungwa.
Actes 25.9 Actes 25.14 Actes 25.1 Actes 12.3 Marc 15.15

Cette Bible est dans le domaine public.