Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Luc 18.34
Bible en Swahili de l’est


Parabole de la veuve et du juge

1 Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa.
Colossiens 4.2 1 Thessaloniciens 5.17 Romains 12.12 Philippiens 4.6 Ephésiens 6.18
2 Akasema, Palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu.
Proverbes 29.7 Luc 18.4 Exode 18.21-18.22 Romains 3.14-3.18 Job 29.7-29.17
3 Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea-endea, akisema, Nipatie haki na adui wangu.
Esaïe 1.17 Romains 13.3-13.4 Deutéronome 27.19 Esaïe 1.21-1.23 Job 22.9
4 Naye kwa muda alikataa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu,
Luc 16.3 Hébreux 4.12-4.13 Luc 12.17
5 lakini, kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima.
Luc 11.8 Marc 10.47-10.48 Luc 18.39 2 Samuel 13.24-13.27 Juges 16.16
6 Bwana akasema, Sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu.
Luc 7.13
7 Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao?
Apocalypse 6.10 Psaumes 88.1 2 Pierre 3.9 2 Thessaloniciens 1.6 Romains 8.33
8 Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?
Hébreux 10.23-10.26 Matthieu 24.9-24.13 2 Pierre 3.8-3.9 2 Pierre 2.3 1 Thessaloniciens 5.1-5.3

Parabole du pharisien et du collecteur d’impôts

9 Akawaambia mfano huu watu waliojikinai ya kuwa wao ni wenye haki, wakiwadharau wengine wote.
Luc 16.15 Esaïe 65.5 Romains 14.10 Proverbes 30.12 Romains 10.3
10 Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili mtoza ushuru.
Actes 3.1 Matthieu 21.31-21.32 Luc 7.29-7.30 2 Rois 20.8 1 Rois 8.30
11 Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang’anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru.
Matthieu 6.5 Marc 11.25 Apocalypse 3.17 Matthieu 3.7-3.10 Luc 20.47
12 Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato yangu yote.
Luc 11.42 Matthieu 9.14 Malachie 3.8 Nombres 23.4 Ephésiens 2.9
13 Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi.
Luc 23.48 Esdras 9.6 1 Timothée 1.15 Romains 5.8 Actes 2.37
14 Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.
Luc 14.11 Luc 16.15 Matthieu 23.12 Romains 3.20 Romains 8.33

Les petits enfants et l’homme riche

15 Wakamletea na watoto wachanga ili awaguse; lakini wanafunzi walipoona waliwakemea.
Matthieu 19.13-19.15 Marc 10.13-10.16 Luc 9.49-9.50 Luc 9.54 1 Samuel 1.24
16 Bali Yesu akawaita waje kwake, akasema, Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa kuwa watu kama hao ufalme wa Mungu ni wao.
Actes 2.39 Deutéronome 31.12 1 Corinthiens 14.20 Jérémie 32.39 1 Pierre 2.2
17 Amin, nawaambia, Mtu ye yote asiyeupokea ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hauingii kamwe.
Marc 10.15 1 Pierre 1.14 Matthieu 18.3 Psaumes 131.1-131.2
18 Tena, mtu mkubwa mmoja alimwuliza, akisema, Mwalimu mwema, nifanye nini ili nipate kuurithi uzima wa milele?
Marc 10.17-10.31 Ezéchiel 33.31 Actes 16.30 Matthieu 19.16-19.30 Luc 6.46
19 Yesu akamwambia, Mbona unaniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, naye ndiye Mungu.
Jacques 1.17 Hébreux 7.26 Luc 11.13 1 Timothée 3.16 Job 14.4
20 Wazijua amri; Usizini, Usiue, Usiibe, Usishuhudie uongo, Waheshimu baba yako na mama yako.
Exode 20.12-20.17 Romains 13.9 Esaïe 8.20 Ephésiens 6.2 Matthieu 19.17-19.19
21 Akasema, Hayo yote nimeyashika tangu utoto wangu.
Philippiens 3.6 Luc 18.11-18.12 Marc 10.20-10.21 Matthieu 19.20-19.21 Romains 10.2-10.3
22 Yesu aliposikia hayo alimwambia, Umepungukiwa na neno moja bado; viuze ulivyo navyo vyote, ukawagawanyie maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha, njoo unifuate.
Luc 10.42 Matthieu 19.21 Luc 16.9 Luc 12.33 Matthieu 6.19-6.20
23 Lakini aliposikia hayo alihuzunika sana, maana alikuwa na mali nyingi.
Ezéchiel 33.31 Marc 10.22 Job 31.24-31.25 Colossiens 3.5 Juges 18.23-18.24
24 Yesu alipoona vile alisema, Kwa shida gani wenye mali watauingia ufalme wa Mungu!
Proverbes 11.28 1 Corinthiens 1.26-1.27 Matthieu 19.23-19.25 Marc 10.23-10.27 Marc 6.26
25 Kwa maana ni vyepesi ngamia kupita katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.
Matthieu 23.24
26 Nao waliosikia walisema, Ni nani basi awezaye kuokoka?
Luc 13.23
27 Akasema, Yasiyowezekana kwa wanadamu yawezekana kwa Mungu.
Jérémie 32.17 Matthieu 19.26 Luc 1.37 Job 42.2 Genèse 18.14
28 Petro akasema, Tazama, sisi tumeviacha vitu vyetu vyote na kukufuata.
Marc 10.28 Luc 5.11 Philippiens 3.7 Matthieu 4.19-4.22 Matthieu 19.27
29 Akawaambia, Hakika nawaambia, hakuna mtu aliyeacha nyumba, au mke, au ndugu, au wazazi, au wana, kwa ajili ya ufalme wa Mungu,
Marc 10.29-10.31 Matthieu 19.28-19.30 Luc 14.26-14.28 Deutéronome 33.9 Matthieu 10.37-10.39
30 asiyepokea zaidi mara nyingi katika zamani hizi, na katika ulimwengu ujao uzima wa milele.
Job 42.10 Matthieu 12.32 Psaumes 63.4-63.5 Apocalypse 3.21 Psaumes 119.127
31 Akawachukua wale Thenashara, akawaambia, Tazameni, tunapanda kwenda Yerusalemu, na mambo yote yatatimizwa, Mwana wa Adamu aliyoandikiwa na manabii.
Esaïe 53.1-53.12 Matthieu 20.17-20.19 Psaumes 22.1-22.31 Zacharie 13.7 Matthieu 16.21
32 Kwa kuwa atatiwa mikononi mwa Mataifa, atafanyiwa dhihaka; atatendwa jeuri, na kutemewa mate;
Luc 23.11 Marc 14.65 Matthieu 27.28-27.30 Matthieu 27.2 Matthieu 26.67
33 nao watampiga mijeledi, kisha watamwua; na siku ya tatu atafufuka.
1 Corinthiens 15.3-15.4 Luc 24.21 Matthieu 27.63 Luc 24.7 Matthieu 16.21
34 Walakini hawakuelewa maneno hayo hata kidogo, na jambo hilo lilikuwa limefichwa kwao, wala hawakufahamu yaliyonenwa.
Marc 9.32 Luc 9.45 Luc 24.45 Jean 10.6 Luc 2.50

Jésus à Jéricho

35 Ikawa alipokaribia Yeriko, mtu mmoja kipofu alikuwa ameketi kando ya njia, akiomba sadaka;
Jean 9.8 Marc 10.46-10.52 Actes 3.2 Matthieu 20.29-20.34 Luc 16.20-16.21
36 na alipowasikia makutano wakipita, aliuliza, Kuna nini?
Matthieu 21.10-21.11 Luc 15.26
37 Wakamwambia, Yesu wa Nazareti anapita.
Matthieu 2.23 Jean 1.45 Actes 2.22 Actes 4.10 Luc 2.51
38 Akapiga kelele, akisema, Yesu, Mwana wa Daudi, unirehemu.
Matthieu 9.27 Matthieu 15.22 Luc 18.39 Matthieu 12.23 Romains 1.3
39 Basi wale waliotangulia wakamkemea ili anyamaze; lakini yeye alizidi sana kupaza sauti, Ee Mwana wa Daudi, unirehemu.
Luc 18.15 Luc 18.38 Matthieu 26.40-26.44 Luc 8.49 Luc 18.1
40 Yesu akasimama, akaamuru aletwe kwake; na alipomkaribia, alimwuliza,
Matthieu 20.31-20.34 Marc 10.48-10.52
41 Wataka nikufanyie nini? Akasema, Bwana, nipate kuona.
1 Rois 3.5-3.15 Philippiens 4.6 Matthieu 20.21-20.22 Romains 8.25
42 Yesu akamwambia, Upewe kuona; imani yako imekuponya.
Matthieu 9.22 Luc 7.50 Luc 17.19 Luc 8.48 Matthieu 15.28
43 Mara hiyo akapata kuona, akamfuata, huku akimtukuza Mungu. Na watu wote walipoona hayo walimsifu Mungu.
Psaumes 146.8 Psaumes 30.2 Esaïe 29.18-29.19 2 Thessaloniciens 1.10-1.12 Luc 13.17

Cette Bible est dans le domaine public.