Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Luc 18.23
Bible en Swahili de l’est


Parabole de la veuve et du juge

1 Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa.
Colossiens 4.2 1 Thessaloniciens 5.17 Romains 12.12 Philippiens 4.6 Ephésiens 6.18
2 Akasema, Palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu.
Proverbes 29.7 Luc 18.4 2 Chroniques 19.3-19.9 Ezéchiel 22.6-22.8 Exode 18.21-18.22
3 Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea-endea, akisema, Nipatie haki na adui wangu.
Esaïe 1.17 Job 29.13 Romains 13.3-13.4 Deutéronome 27.19 Esaïe 1.21-1.23
4 Naye kwa muda alikataa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu,
Luc 12.17 Luc 16.3 Hébreux 4.12-4.13
5 lakini, kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima.
Luc 11.8 Matthieu 15.23 Marc 10.47-10.48 Luc 18.39 2 Samuel 13.24-13.27
6 Bwana akasema, Sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu.
Luc 7.13
7 Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao?
Apocalypse 6.10 Psaumes 88.1 2 Pierre 3.9 Romains 8.33 Hébreux 10.35-10.37
8 Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?
Hébreux 10.23-10.26 Matthieu 24.9-24.13 2 Pierre 3.8-3.9 2 Pierre 2.3 1 Thessaloniciens 5.1-5.3

Parabole du pharisien et du collecteur d’impôts

9 Akawaambia mfano huu watu waliojikinai ya kuwa wao ni wenye haki, wakiwadharau wengine wote.
Luc 16.15 Esaïe 65.5 Romains 14.10 Proverbes 30.12 Romains 7.9
10 Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili mtoza ushuru.
Actes 3.1 Luc 19.46 Actes 23.6-23.8 Matthieu 21.31-21.32 Luc 7.29-7.30
11 Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang’anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru.
Matthieu 6.5 Marc 11.25 Apocalypse 3.17 Ezéchiel 33.31 Philippiens 3.6
12 Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato yangu yote.
Luc 11.42 Matthieu 9.14 Malachie 3.8 Lévitique 27.30-27.33 Matthieu 23.23-23.24
13 Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi.
Luc 23.48 Esdras 9.6 Actes 2.37 1 Timothée 1.15 Romains 5.8
14 Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.
Luc 14.11 Matthieu 23.12 Luc 16.15 Romains 3.20 Luc 1.52

Les petits enfants et l’homme riche

15 Wakamletea na watoto wachanga ili awaguse; lakini wanafunzi walipoona waliwakemea.
Matthieu 19.13-19.15 Marc 10.13-10.16 1 Samuel 1.24 Luc 9.49-9.50 Luc 9.54
16 Bali Yesu akawaita waje kwake, akasema, Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa kuwa watu kama hao ufalme wa Mungu ni wao.
Actes 2.39 Deutéronome 31.12 1 Corinthiens 14.20 1 Corinthiens 7.14 Genèse 21.4
17 Amin, nawaambia, Mtu ye yote asiyeupokea ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hauingii kamwe.
Marc 10.15 1 Pierre 1.14 Psaumes 131.1-131.2 Matthieu 18.3
18 Tena, mtu mkubwa mmoja alimwuliza, akisema, Mwalimu mwema, nifanye nini ili nipate kuurithi uzima wa milele?
Marc 10.17-10.31 Ezéchiel 33.31 Actes 16.30 Matthieu 19.16-19.30 Luc 6.46
19 Yesu akamwambia, Mbona unaniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, naye ndiye Mungu.
Jacques 1.17 Job 15.14-15.16 Hébreux 7.26 Luc 11.13 1 Timothée 3.16
20 Wazijua amri; Usizini, Usiue, Usiibe, Usishuhudie uongo, Waheshimu baba yako na mama yako.
Exode 20.12-20.17 Romains 13.9 Jacques 2.8-2.11 Deutéronome 5.16-5.21 Galates 3.10-3.13
21 Akasema, Hayo yote nimeyashika tangu utoto wangu.
Philippiens 3.6 Luc 15.29 Luc 18.11-18.12 Marc 10.20-10.21 Matthieu 19.20-19.21
22 Yesu aliposikia hayo alimwambia, Umepungukiwa na neno moja bado; viuze ulivyo navyo vyote, ukawagawanyie maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha, njoo unifuate.
Luc 16.9 Luc 12.33 Matthieu 6.19-6.20 Luc 10.42 Matthieu 19.21
23 Lakini aliposikia hayo alihuzunika sana, maana alikuwa na mali nyingi.
Ezéchiel 33.31 Luc 12.15 1 Jean 2.15 Luc 21.34 Luc 8.14
24 Yesu alipoona vile alisema, Kwa shida gani wenye mali watauingia ufalme wa Mungu!
Proverbes 11.28 Psaumes 73.5-73.12 Deutéronome 6.10-6.12 Proverbes 30.9 Jérémie 5.5
25 Kwa maana ni vyepesi ngamia kupita katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.
Matthieu 23.24
26 Nao waliosikia walisema, Ni nani basi awezaye kuokoka?
Luc 13.23
27 Akasema, Yasiyowezekana kwa wanadamu yawezekana kwa Mungu.
Jérémie 32.17 Matthieu 19.26 Luc 1.37 Job 42.2 Genèse 18.14
28 Petro akasema, Tazama, sisi tumeviacha vitu vyetu vyote na kukufuata.
Marc 10.28 Luc 5.11 Matthieu 9.9 Philippiens 3.7 Matthieu 4.19-4.22
29 Akawaambia, Hakika nawaambia, hakuna mtu aliyeacha nyumba, au mke, au ndugu, au wazazi, au wana, kwa ajili ya ufalme wa Mungu,
Marc 10.29-10.31 Matthieu 19.28-19.30 Luc 14.26-14.28 Matthieu 10.37-10.39 Deutéronome 33.9
30 asiyepokea zaidi mara nyingi katika zamani hizi, na katika ulimwengu ujao uzima wa milele.
Job 42.10 Matthieu 12.32 1 Timothée 6.6 Hébreux 13.5-13.6 Psaumes 37.16
31 Akawachukua wale Thenashara, akawaambia, Tazameni, tunapanda kwenda Yerusalemu, na mambo yote yatatimizwa, Mwana wa Adamu aliyoandikiwa na manabii.
Psaumes 22.1-22.31 Esaïe 53.1-53.12 Matthieu 20.17-20.19 Luc 9.51 Daniel 9.26
32 Kwa kuwa atatiwa mikononi mwa Mataifa, atafanyiwa dhihaka; atatendwa jeuri, na kutemewa mate;
Luc 23.11 Actes 3.13 Jean 18.30 Marc 14.65 Matthieu 27.28-27.30
33 nao watampiga mijeledi, kisha watamwua; na siku ya tatu atafufuka.
Matthieu 16.21 1 Corinthiens 15.3-15.4 Luc 24.21 Matthieu 27.63 Luc 24.7
34 Walakini hawakuelewa maneno hayo hata kidogo, na jambo hilo lilikuwa limefichwa kwao, wala hawakufahamu yaliyonenwa.
Marc 9.32 Luc 9.45 Jean 16.1-16.19 Luc 24.45 Jean 10.6

Jésus à Jéricho

35 Ikawa alipokaribia Yeriko, mtu mmoja kipofu alikuwa ameketi kando ya njia, akiomba sadaka;
Jean 9.8 Luc 19.1 Marc 10.46-10.52 Actes 3.2 Matthieu 20.29-20.34
36 na alipowasikia makutano wakipita, aliuliza, Kuna nini?
Luc 15.26 Matthieu 21.10-21.11
37 Wakamwambia, Yesu wa Nazareti anapita.
Matthieu 2.23 Jean 19.19 Jean 1.45 Actes 2.22 Actes 4.10
38 Akapiga kelele, akisema, Yesu, Mwana wa Daudi, unirehemu.
Matthieu 9.27 Luc 18.39 Matthieu 15.22 Matthieu 22.42-22.45 Esaïe 11.1
39 Basi wale waliotangulia wakamkemea ili anyamaze; lakini yeye alizidi sana kupaza sauti, Ee Mwana wa Daudi, unirehemu.
Luc 18.15 Luc 19.39 Matthieu 7.7 2 Corinthiens 12.8 Jérémie 29.12-29.13
40 Yesu akasimama, akaamuru aletwe kwake; na alipomkaribia, alimwuliza,
Marc 10.48-10.52 Matthieu 20.31-20.34
41 Wataka nikufanyie nini? Akasema, Bwana, nipate kuona.
1 Rois 3.5-3.15 Romains 8.25 Philippiens 4.6 Matthieu 20.21-20.22
42 Yesu akamwambia, Upewe kuona; imani yako imekuponya.
Matthieu 9.22 Luc 7.50 Luc 17.19 Luc 8.48 Matthieu 8.3
43 Mara hiyo akapata kuona, akamfuata, huku akimtukuza Mungu. Na watu wote walipoona hayo walimsifu Mungu.
Esaïe 35.5 Psaumes 107.31-107.32 Psaumes 107.15 Actes 11.18 Luc 5.26

Cette Bible est dans le domaine public.