Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Luc 16.30
Bible en Swahili de l’est


Parabole de l’intendant infidèle

1 Tena, aliwaambia wanafunzi wake, Palikuwa na mtu mmoja, tajiri, aliyekuwa na wakili wake; huyu alishitakiwa kwake kuwa anatapanya mali zake.
Luc 15.13 Luc 12.42 Luc 15.30 1 Pierre 4.10 Genèse 15.2
2 Akamwita, akamwambia, Ni habari gani hii ninayosikia juu yako? Toa hesabu ya uwakili wako, kwa kuwa huwezi kuwa wakili tena.
2 Corinthiens 5.10 1 Corinthiens 1.11 Apocalypse 20.12 1 Corinthiens 4.2 Genèse 18.20-18.21
3 Yule wakili akasema moyoni mwake, Nifanyeje? Maana, bwana wangu ananiondolea uwakili. Kulima, siwezi; kuomba, naona haya.
2 Thessaloniciens 3.11 Proverbes 21.25-21.26 Proverbes 29.21 Marc 10.46 Proverbes 19.15
4 Najua nitakalotenda, ili nitakapotolewa katika uwakili, wanikaribishe nyumbani mwao.
Jacques 3.15 Proverbes 30.9 Jérémie 4.22
5 Akawaita wadeni wa bwana wake, kila mmoja; akamwambia wa kwanza, Wawiwani na bwana wangu?
Luc 7.41-7.42 Matthieu 18.24
6 Akasema, Vipimo mia vya mafuta. Akamwambia, Twaa hati yako, keti upesi, andika hamsini.
Luc 16.12 Tite 2.10 Luc 16.9
7 Kisha akamwambia mwingine, Na wewe wawiwani? Akasema, Makanda mia ya ngano. Akamwambia, Twaa hati yako, andika themanini.
Luc 20.12 Luc 20.9 Cantique 8.11-8.12
8 Yule bwana akamsifu wakili dhalimu kwa vile alivyotenda kwa busara; kwa kuwa wana wa ulimwengu huu katika kizazi chao wenyewe huwa na busara kuliko wana wa nuru.
Ephésiens 5.8 1 Thessaloniciens 5.5 Jean 12.36 Luc 20.34 Psaumes 17.14
9 Nami nawaambia, Jifanyieni rafiki kwa mali ya udhalimu, ili itakapokosekana wawakaribishe katika makao ya milele.
Matthieu 19.21 Luc 16.11 1 Timothée 6.17-6.19 Luc 12.33 Luc 16.13
10 Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia; na aliye dhalimu katika lililo dogo, huwa dhalimu katika lililo kubwa pia.
Matthieu 25.21 Luc 19.17 Matthieu 25.23 Luc 16.11-16.12 Hébreux 3.2
11 Basi, kama ninyi hamkuwa waaminifu katika mali ya udhalimu, ni nani atakayewapa amana mali ya kweli?
Luc 18.22 Ephésiens 3.8 Luc 12.33 Jacques 2.5 Proverbes 8.18-8.19
12 Na kama hamkuwa waaminifu katika mali ya mtu mwingine, ni nani atakayewapa iliyo yenu wenyewe?
Luc 19.13-19.26 1 Chroniques 29.14-29.16 Job 1.21 Ezéchiel 16.16-16.21 Osée 2.8
13 Hakuna mtumishi awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana, ama atamchukia huyu na kumpenda huyu, ama atashikamana na huyu na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali.
1 Jean 2.15-2.16 Matthieu 6.24 Jacques 4.4 Luc 16.9 Romains 8.5-8.8
14 Basi Mafarisayo, ambao wenyewe ni wapenda fedha, waliyasikia hayo yote, wakamdhihaki.
Luc 23.35 Luc 20.47 Ezéchiel 22.25-22.29 Hébreux 12.2-12.3 Luc 8.53
15 Akawaambia, Ninyi ndinyi mnaojidai haki mbele ya wanadamu, lakini Mungu awajua mioyo yenu; kwa kuwa lililotukuka kwa wanadamu huwa chukizo mbele za Mungu.
1 Samuel 16.7 Proverbes 16.5 1 Pierre 3.4 Proverbes 21.2 1 Corinthiens 4.5
16 Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu.
Matthieu 11.9-11.14 Matthieu 3.2 Actes 3.18 Actes 3.24-3.25 Jean 1.45
17 Lakini ni vyepesi zaidi mbingu na nchi vitoweke, kuliko itanguke nukta moja ya torati.
Matthieu 5.18 Luc 21.33 Esaïe 40.8 1 Pierre 1.25 Psaumes 102.25-102.27
18 Kila amwachaye mkewe na kumwoa mke mwingine azini; naye amwoaye yeye aliyeachwa na mumewe azini.
Matthieu 19.9 Matthieu 5.31-5.32 Marc 10.11-10.12 1 Corinthiens 7.4 1 Corinthiens 7.10-7.12

Histoire de l’homme riche et du pauvre Lazare

19 Akasema, Palikuwa na mtu mmoja, tajiri, aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, na kula sikuzote kwa anasa.
Esther 8.15 Ezéchiel 16.49 Apocalypse 18.16 Marc 15.17 Marc 15.20
20 Na maskini mmoja, jina lake Lazaro, huwekwa mlangoni pake, ana vidonda vingi,
Actes 3.2 Psaumes 34.19 Jacques 2.5 1 Samuel 2.8 Jacques 1.9
21 naye alikuwa akitamani kushibishwa kwa makombo yaliyoanguka katika meza ya yule tajiri; hata mbwa wakaja wakamramba vidonda vyake.
Matthieu 15.27 Marc 7.28 2 Corinthiens 11.27 1 Corinthiens 4.11 Jean 6.12
22 Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa.
Jean 13.23 Marc 8.36 Apocalypse 14.13 Jacques 1.11 Psaumes 49.6-49.12
23 Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake.
Luc 16.28 Psaumes 9.17 Matthieu 5.29 Matthieu 8.11-8.12 Matthieu 18.9
24 Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.
Matthieu 25.41 Luc 16.30 Esaïe 66.24 Luc 3.8 Zacharie 14.12
25 Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa.
Luc 6.24 Psaumes 17.14 1 Jean 2.15 Marc 9.45 Lamentations 1.7
26 Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku kwenda kwenu wasiweze; wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu.
Matthieu 25.46 2 Thessaloniciens 1.4-1.10 Malachie 3.18 Ezéchiel 28.24 1 Samuel 25.36
27 Akasema, Basi, baba, nakuomba, umtume nyumbani kwa baba yangu,
28 kwa kuwa ninao ndugu watano, ili awashuhudie, wasije wao pia wakafika mahali hapa pa mateso.
Actes 20.23 Psaumes 49.12-49.13 1 Thessaloniciens 4.6 Actes 2.40
29 Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao.
Actes 15.21 Luc 24.27 Luc 16.16 Jean 5.39-5.47 Esaïe 8.20
30 Akasema, La, baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea mtu atokaye kwa wafu, watatubu.
Apocalypse 16.9-16.11 Luc 3.8 Luc 16.24 Luc 13.5 Luc 13.3
31 Akamwambia, Wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishwa hata mtu akifufuka katika wafu.
Actes 19.8 Genèse 9.27 2 Corinthiens 5.11 Actes 26.28 Jean 11.43-11.53

Cette Bible est dans le domaine public.