Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Marc 10.30
Bible en Swahili de l’est


Ministère de Jésus en Judée

Le divorce

1 Akaondoka huko akafika mipakani mwa Uyahudi, na ng’ambo ya Yordani; makutano mengi wakakutanika tena wakamwendea; akawafundisha tena kama alivyozoea.
Jean 10.40 Jean 11.7 Matthieu 19.1-19.12 Jean 18.20 Ecclésiaste 12.9
2 Basi Mafarisayo wakamwendea, wakamwuliza, Je! Ni halali mtu kumwacha mkewe? Huku wakimjaribu.
Matthieu 23.13 Jean 8.6 Luc 11.53-11.54 Luc 16.14 Luc 6.7
3 Naye akajibu, akawaambia, Musa aliwaamuru nini?
Jean 5.39 Galates 4.21 Esaïe 8.20 Luc 10.25
4 Wakasema, Musa alitoa ruhusa kuandika hati ya talaka na kumwacha.
Deutéronome 24.1-24.4 Matthieu 5.31-5.32 Jérémie 3.1 Esaïe 50.1 Matthieu 19.7
5 Yesu akawaambia, Kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu aliwaandikia amri hii.
Matthieu 19.8 Néhémie 9.16-9.17 Actes 7.51 Deutéronome 31.27 Néhémie 9.26
6 Lakini tangu mwanzo wa kuumbwa ulimwengu, aliwafanya mume na mke.
Genèse 1.27 Genèse 5.2 2 Pierre 3.4 Malachie 2.14-2.16 Marc 13.19
7 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe;
Genèse 2.24 Ephésiens 5.31 Matthieu 19.5-19.6
8 na hao wawili watakuwa mwili mmoja; hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja.
1 Corinthiens 6.16 Genèse 2.24 Ephésiens 5.28
9 Basi alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.
Romains 7.1-7.3
10 Hata nyumbani tena wanafunzi wakamwuliza habari ya neno hilo.
Marc 9.33 Marc 9.28 Marc 4.10
11 Akawaambia, Kila mtu atakayemwacha mkewe na kuoa mwingine azini juu yake;
Luc 16.18 Matthieu 19.9 1 Corinthiens 7.4 Hébreux 13.4 Matthieu 5.31-5.32
12 na mke, akimwacha mumewe na kuolewa na mtu mwingine, azini.
1 Corinthiens 7.11 1 Corinthiens 7.13

Les petits enfants et l’homme riche

13 Basi wakamletea watoto wadogo ili awaguse; wanafunzi wake wakawakemea.
Matthieu 19.13-19.15 Luc 18.15-18.17 Marc 10.48 Marc 9.38 Joël 2.16
14 Ila Yesu alipoona alichukizwa sana, akawaambia, Waacheni watoto wadogo waje kwangu, msiwazuie; kwa maana watoto kama hawa ufalme wa Mungu ni wao.
Matthieu 18.4 Matthieu 19.14 Matthieu 18.10 1 Pierre 2.2 Ephésiens 4.26
15 Amin, nawaambieni, Ye yote asiyeukubali ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hatauingia kabisa.
Matthieu 18.3 Luc 18.17 Jean 3.3-3.6
16 Akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabarikia.
Marc 9.36 Luc 24.50-24.51 Esaïe 40.11 Jean 21.15-21.17 Genèse 48.14-48.16
17 Hata alipokuwa akitoka kwenda njiani, mtu mmoja akaja mbio, akampigia magoti, akamwuliza, Mwalimu mwema, nifanye nini nipate kuurithi uzima wa milele?
Luc 18.18-18.30 Marc 1.40 Matthieu 19.16-19.30 Luc 10.25 Actes 20.32
18 Yesu akamwambia, Kwa nini kuniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, ndiye Mungu.
Luc 18.19 1 Samuel 2.2 Matthieu 19.17 1 Jean 4.16 Psaumes 36.7-36.8
19 Wazijua amri, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo, Usidanganye, Waheshimu baba yako na mama yako.
Romains 13.9 Exode 20.12-20.17 Luc 18.20 Deutéronome 5.16-5.24 Romains 3.20
20 Akamwambia, Mwalimu, haya yote nimeyashika tangu utoto wangu.
Philippiens 3.6 Matthieu 19.20 Luc 10.29 2 Timothée 3.5 Ezéchiel 5.14
21 Yesu akamkazia macho, akampenda, akamwambia, Umepungukiwa na neno moja. Enenda, ukauze ulivyo navyo vyote, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate.
Actes 2.45 Luc 12.33 Luc 16.9 Matthieu 6.19-6.21 1 Timothée 6.17-6.19
22 Walakini yeye akakunja uso kwa neno hilo, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
1 Timothée 6.9-6.10 1 Jean 2.15-2.16 Luc 12.15 2 Timothée 4.10 Matthieu 19.22
23 Yesu akatazama kotekote, akawaambia wanafunzi wake, Jinsi itakavyokuwa shida wenye mali kuingia katika ufalme wa Mungu!
Marc 3.5 1 Corinthiens 1.26 Luc 18.24 Marc 10.15 Matthieu 19.23-19.26
24 Wanafunzi wakashangaa kwa maneno yake. Yesu akajibu tena, akawaambia, Watoto, jinsi ilivyo shida wenye kutegemea mali kuingia katika ufalme wa Mungu!
Jean 21.5 Psaumes 52.7 Jean 13.33 Proverbes 11.28 1 Timothée 6.17
25 Ni rahisi ngamia kupenya katika tundu ya sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.
Jérémie 13.23 Matthieu 23.24 Matthieu 7.3-7.5 Matthieu 19.24-19.25 Luc 18.25
26 Nao wakashangaa mno, wakimwambia, Ni nani, basi, awezaye kuokoka?
Actes 16.31 2 Corinthiens 11.23 Romains 10.9-10.13 Marc 6.51 Luc 18.26
27 Yesu akawakazia macho, akasema, Kwa wanadamu haiwezekani, bali kwa Mungu sivyo; maana yote yawezekana kwa Mungu.
Matthieu 19.26 Luc 1.37 Jérémie 32.17 Luc 18.27 Job 42.2
28 Petro akaanza kumwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata wewe.
Luc 18.28-18.30 Luc 14.33 Marc 1.16-1.20 Matthieu 4.20 Matthieu 4.22
29 Yesu akasema, Amin, nawaambieni, Hakuna mtu aliyeacha nyumba, au ndugu waume, au ndugu wake, au mama, au baba, au watoto, au mashamba, kwa ajili yangu, na kwa ajili ya Injili,
Marc 8.35 Apocalypse 2.3 Genèse 12.1-12.3 1 Corinthiens 9.23 Hébreux 11.24-11.26
30 ila atapewa mara mia sasa wakati huu, nyumba, na ndugu waume, na ndugu wake, na mama, na watoto, na mashamba, pamoja na udhia; na katika ulimwengu ujao uzima wa milele.
Jean 16.22-16.23 Luc 18.30 Philippiens 3.8 2 Corinthiens 6.10 Psaumes 84.11
31 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho; na wa mwisho watakuwa wa kwanza.
Matthieu 19.30 Matthieu 20.16 Luc 13.30 Luc 7.40-7.47 Matthieu 21.31

Demande de Jacques et Jean

32 Nao walikuwako njiani, huku wakipanda kwenda Yerusalemu; na Yesu alikuwa akiwatangulia, wakashangaa, nao katika kufuata wakaogopa. Akawatwaa tena wale Thenashara, akaanza kuwaambia habari za mambo yatakayompata,
Matthieu 20.17-20.19 Luc 9.51 Luc 18.31-18.34 Zacharie 3.8 Matthieu 11.25
33 akisema, Angalieni, tunapanda kwenda Yerusalemu; na Mwana wa Adamu atatiwa mikononi mwa wakuu wa makuhani na waandishi, nao watamhukumu afe, watamtia mikononi mwa Mataifa,
Matthieu 27.2 Actes 3.13-3.14 Matthieu 16.21 Matthieu 26.66 Marc 8.31
34 nao watamdhihaki, na kumtemea mate, na kumpiga mijeledi, na kumwua; na baada ya siku tatu atafufuka.
Marc 14.65 Matthieu 16.21 Matthieu 26.67 Psaumes 22.6-22.8 Luc 22.63-22.65
35 Na Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, wakamwendea, wakamwambia, Mwalimu, twataka utufanyie lo lote tutakalokuomba.
Matthieu 20.20-20.28 1 Rois 2.16 Marc 1.19-1.20 Marc 14.33 1 Rois 2.20
36 Akawaambia, Mwataka niwafanyie nini?
Marc 10.51 Jean 15.7 1 Rois 3.5-3.15
37 Wakamwambia, Utujalie sisi tuketi, mmoja mkono wako wa kuume, na mmoja mkono wako wa kushoto, katika utukufu wako.
Matthieu 19.28 Luc 24.26 1 Pierre 1.11 Marc 8.38 Marc 16.19
38 Yesu akawaambia, Hamjui mnaloliomba. Mwaweza kunywea kikombe ninyweacho mimi, au kubatizwa ubatizo nibatizwao mimi?
Luc 12.50 Luc 22.42 Marc 14.36 Jean 18.11 Esaïe 51.22
39 Wakamwambia, Twaweza. Yesu akawaambia, Kikombe ninyweacho mimi mtakinywea, na ubatizo nibatizwao mimi mtabatizwa;
Actes 12.2 Apocalypse 1.9 Marc 14.31 Matthieu 10.25 Colossiens 1.24
40 lakini habari ya kuketi mkono wangu wa kuume au mkono wangu wa kushoto si langu kuwapa, ila wao watapewa waliowekewa tayari.
Matthieu 25.34 Jean 17.2 Hébreux 11.16 Jean 17.24 Matthieu 20.23
41 Hata wale kumi waliposikia wakaanza kuwakasirikia Yakobo na Yohana.
Proverbes 13.10 Romains 12.10 Philippiens 2.3 Jacques 4.5 Matthieu 20.24
42 Yesu akawaita, akawaambia, Mwajua ya kuwa wale wanaohesabiwa kuwa wakuu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, na wakubwa wao huwatumikisha.
1 Pierre 5.3 Luc 22.25 Matthieu 20.25
43 Lakini haitakuwa hivyo kwenu; bali mtu anayetaka kuwa mkubwa kwenu, atakuwa mtumishi wenu,
Matthieu 23.8-23.12 1 Corinthiens 9.19-9.23 Marc 9.35 Luc 18.14 Matthieu 20.26-20.27
44 na mtu anayetaka kuwa wa kwanza wenu, atakuwa mtumwa wa wote.
45 Kwa maana Mwana wa Adamu naye hakuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi.
Matthieu 20.28 Philippiens 2.5-2.8 Jean 13.14 Tite 2.14 2 Corinthiens 5.21

Guérison d’un aveugle

46 Wakafika Yeriko; hata alipokuwa akishika njia kutoka Yeriko, pamoja na wanafunzi wake, na mkutano mkubwa, mwana wa Timayo, Bartimayo, yule mwombaji kipofu, alikuwa ameketi kando ya njia.
Matthieu 20.29-20.34 Luc 18.35-19.1 Jean 9.8 Luc 16.22 Luc 16.20
47 Naye aliposikia ya kwamba ni Yesu Mnazareti, alianza kupaza sauti yake, na kusema, Mwana wa Daudi, Yesu, unirehemu.
Matthieu 9.27 Luc 18.36-18.37 Marc 1.24 Jérémie 23.5-23.6 Matthieu 2.23
48 Na wengi wakamkemea ili anyamaze, lakini alizidi kupaza sauti, Mwana wa Daudi, unirehemu.
Matthieu 19.13 Marc 7.26-7.29 Luc 18.1-18.8 Matthieu 20.31 Hébreux 5.7
49 Yesu akasimama akasema, Mwiteni. Wakamwita yule kipofu, wakamwambia, Jipe moyo; inuka, anakuita.
Jean 11.28 Luc 18.40 Psaumes 145.8 Hébreux 2.17 Matthieu 20.32-20.34
50 Akatupa vazi lake, akaruka, akamwendea Yesu.
Hébreux 12.1 Philippiens 3.7-3.9
51 Yesu akamjibu, akamwambia, Wataka nikufanyie nini? Yule kipofu akamwambia, Mwalimu wangu, nataka nipate kuona.
Marc 10.36 Matthieu 23.7 Philippiens 4.6 Matthieu 7.7 Matthieu 6.8
52 Yesu akamwambia, Enenda zako, imani yako imekuponya. Mara akapata kuona; akamfuata njiani.
Matthieu 9.22 Marc 5.34 Marc 8.25 Luc 7.50 Matthieu 21.14

Cette Bible est dans le domaine public.