Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Nombres 7.4
Bible en Swahili de l’est


Offrandes des douze princes

1 Ilikuwa siku hiyo Musa alipokwisha kuisimamisha maskani, na kuitia mafuta, na kuitakasa, na vyombo vyake vyote, na hiyo madhabahu na vyombo vyake vyote, na kuvitia mafuta, na kuvitakasa;
Lévitique 8.10-8.11 Exode 40.17-40.19 Nombres 7.84 Exode 30.23-30.30 Exode 40.9-40.10
2 ndipo wakuu wa Israeli, vichwa vya nyumba za baba zao, wakatoa matoleo; hao ndio wakuu wa kabila, hao ndio waliokuwa juu yao waliohesabiwa;
Nombres 1.4-1.16 2 Chroniques 35.8 Néhémie 7.70-7.72 Esdras 2.68-2.69 Exode 35.27
3 nao wakamletea Bwana matoleo yao, magari sita yenye mafuniko juu, na ng’ombe kumi na wawili; gari moja kwa wakuu wawili wawili, na ng’ombe mmoja kwa kila mkuu; nao wakayasongeza hapo mbele ya maskani.
4 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
5 Pokea mikononi mwao, ili kwamba viwe vya kutumiwa katika utumishi wa hema ya kukutania; nawe utawapa Walawi vitu hivyo, kila mtu utampa kama utumishi wake ulivyo.
Exode 25.1-25.11 Ephésiens 4.11-4.13 Exode 35.4-35.10 Psaumes 16.2-16.3 Esaïe 42.1-42.7
6 Basi Musa akapokea hayo magari, na ng’ombe, akawapa Walawi.
7 Wana wa Gershoni akawapa magari mawili na ng’ombe wanne, kama utumishi wao ulivyokuwa;
Nombres 4.24-4.28 Nombres 3.25-3.26
8 na wana wa Merari akawapa magari manne na ng’ombe wanane kama utumishi wao ulivyokuwa, chini ya mkono wa Ithamari, mwana wa Haruni kuhani.
Nombres 3.36-3.37 Nombres 4.28-4.33
9 Lakini hakuwapa wana wa Kohathi; maana, utumishi wa vile vitu vitakatifu ulikuwa ni wao; nao wakavichukua mabegani mwao.
Nombres 3.31 2 Samuel 6.13 1 Chroniques 23.26 Nombres 4.4-4.16 2 Samuel 6.6
10 Kisha wale wakuu wakatoa matoleo kwa ajili ya kuiweka wakfu madhabahu, katika siku hiyo iliyotiwa mafuta, wakuu wakayatoa matoleo yao mbele ya madhabahu.
2 Chroniques 7.9 1 Rois 8.63 Deutéronome 20.5 Néhémie 12.27 2 Chroniques 7.5
11 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia, Watasongeza matoleo yao, kila mkuu kwa siku yake, kwa ajili ya kuiweka wakfu madhabahu.
1 Corinthiens 14.33 Colossiens 2.5 1 Corinthiens 14.40
12 Basi aliyetoa matoleo yake siku ya kwanza ni Nashoni mwana wa Aminadabu, wa kabila ya Yuda;
Nombres 10.14 Genèse 49.10 Matthieu 1.4 Genèse 49.8 Luc 3.32
13 na matoleo yake yalikuwa sahani moja ya fedha, uzani wake ni shekeli mia na thelathini, na bakuli moja ya fedha uzani wake ni shekeli sabini, kwa shekeli ya mahali patakatifu; vyombo hivyo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga;
Exode 30.13 Exode 37.16 Exode 25.29 Lévitique 2.1 Nombres 3.47
14 na kijiko kimoja cha dhahabu, uzani wake shekeli kumi, kimejaa uvumba;
Exode 30.7-30.8 Exode 37.16 Exode 35.8 2 Chroniques 4.22 2 Chroniques 24.14
15 ng’ombe mmoja mume mchanga, na kondoo mmoja mume, na mwana-kondoo mume mmoja wa mwaka wa kwanza, kuwa sadaka ya kuteketezwa;
Esaïe 53.10-53.11 Romains 5.16-5.21 Nombres 25.1-25.18 Romains 5.6-5.11 1 Pierre 3.18
16 mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi;
Lévitique 4.23 Lévitique 4.25
17 na kwa ajili ya dhabihu ya sadaka za amani, ng’ombe waume wawili, na kondoo waume watano, na mbuzi waume watano, na wana-kondoo watano waume wa mwaka wa kwanza; hayo ndiyo matoleo ya Nashoni mwana wa Aminadabu.
2 Corinthiens 5.19-5.21 Lévitique 3.1-3.17
18 Siku ya pili Nethaneli mwana wa Suari, mkuu wa Isakari, alitoa;
Nombres 1.8 Nombres 2.5
19 yeye akasongeza matoleo yake, sahani moja ya fedha, uzani wake ni shekeli mia na thelathini, na bakuli moja ya fedha, uzani wake shekeli sabini, kwa shekeli ya mahali patakatifu; vyombo hivyo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, kuwa ni sadaka ya unga;
20 na kijiko kimoja cha dhahabu, uzani wake shekeli kumi, kilikuwa kimejaa uvumba;
21 na ng’ombe mmoja mume mchanga, na kondoo mume mmoja, na mwana-kondoo mume mmoja wa mwaka wa kwanza, kuwa sadaka ya kuteketezwa;
Romains 12.1 Genèse 8.20 Ephésiens 5.2
22 na mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi;
23 na kwa dhabihu ya sadaka za amani, ng’ombe wawili waume, na kondoo waume watano, na mbuzi waume watano, na wana-kondoo watano waume wa mwaka wa kwanza; hayo ndiyo matoleo ya Nethaneli mwana wa Suari.
Lévitique 7.11-7.13 Colossiens 1.1 1 Rois 8.63 Proverbes 7.14
24 Siku ya tatu Eliabu mwana wa Heloni, mkuu wa wana wa Zabuloni;
Nombres 1.9 Nombres 2.7
25 matoleo yake yalikuwa sahani moja ya fedha, uzani wake ni shekeli mia na thelathini, na bakuli moja ya fedha, uzani wake shekeli sabini, kwa shekeli ya mahali patakatifu; vyombo hivyo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, kuwa sadaka ya unga;
26 na kijiko kimoja cha dhahabu, uzani wake shekeli kumi, kilichojaa uvumba;
27 na ng’ombe mmoja mume mchanga, na kondoo mume mmoja, na mwana-kondoo mume mmoja wa mwaka wa kwanza, kuwa sadaka ya kuteketezwa;
Psaumes 51.16 Jérémie 7.22 Amos 5.22 Psaumes 50.8-50.14 Esaïe 1.11
28 na mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi;
29 tena kwa ajili ya dhabihu ya sadaka za amani, ng’ombe wawili waume, na kondoo waume watano, na mbuzi waume watano, na wana-kondoo watano waume wa mwaka wa kwanza; hayo ndiyo matoleo ya Eliabu mwana wa Heloni.
30 Siku ya nne Elisuri mwana wa Shedeuri, mkuu wa wana wa Reubeni;
Nombres 1.5 Nombres 2.10
31 matoleo yake yalikuwa sahani moja ya fedha, uzani wake ni shekeli mia na thelathini, na bakuli moja ya fedha, uzani wake shekeli sabini, kwa shekeli ya mahali patakatifu; vyombo hivyo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, kuwa sadaka ya unga;
32 na kijiko kimoja cha dhahabu, uzani wake shekeli kumi, kilichojaa uvumba;
Luc 1.10 Apocalypse 8.3 Psaumes 66.15 Malachie 1.11
33 na ng’ombe mmoja mume mchanga, na kondoo mume mmoja, na mwana-kondoo mume mmoja wa mwaka wa kwanza, kuwa sadaka ya kuteketezwa;
34 na mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi;
35 tena kwa ajili ya dhabihu ya sadaka za amani, ng’ombe wawili waume, na kondoo waume watano, na mbuzi waume watano, na wana-kondoo watano waume wa mwaka wa kwanza; hayo ndiyo matoleo ya Elisuri mwana wa Shedeuri.
36 Siku ya tano Shelumieli mwana wa Suri-shadai, mkuu wa wana Simeoni;
Nombres 1.6 Nombres 2.12
37 matoleo yake yalikuwa sahani moja ya fedha, uzani wake ni shekeli mia na thelathini, na bakuli moja ya fedha, uzani wake shekeli sabini, kwa shekeli ya mahali patakatifu; vyombo hivyo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, kuwa sadaka ya unga;
38 na kijiko kimoja cha dhahabu, uzani wake shekeli kumi, kilichojaa uvumba;
39 na ng’ombe mmoja mume mchanga, na kondoo mume mmoja, na mwana-kondoo mume mmoja wa mwaka wa kwanza, kuwa sadaka ya kuteketezwa;
Apocalypse 5.6 Exode 12.5 Actes 8.32 Jean 1.29 1 Pierre 1.19
40 na mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi;
41 tena kwa ajili ya dhabihu ya sadaka za amani, ng’ombe wawili waume, na kondoo waume watano, na mbuzi waume watano, na wana-kondoo watano waume wa mwaka wa kwanza; hayo ndiyo matoleo ya Shelumieli mwana wa Suri-shadai
42 Siku ya sita Eliasafu mwana wa Deueli, mkuu wa wana wa Gadi
Nombres 1.14 Nombres 2.14
43 matoleo yake yalikuwa sahani moja ya fedha, uzani wake ni shekeli mia na thelathini, na bakuli moja ya fedha, uzani wake shekeli sabini, kwa shekeli ya mahali patakatifu; vyombo hivyo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, kuwa sadaka ya unga;
Lévitique 14.10 Lévitique 2.5 Hébreux 1.9 1 Jean 2.27
44 na kijiko kimoja cha dhahabu, uzani wake shekeli kumi, kilichojaa uvumba;
45 na ng’ombe mmoja mume mchanga, na kondoo mume mmoja, na mwana-kondoo mume mmoja wa mwaka wa kwanza, kuwa sadaka ya kuteketezwa;
Esaïe 53.4 Psaumes 66.15 2 Corinthiens 5.21
46 na mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi;
47 tena kwa ajili ya dhabihu ya sadaka za amani, ng’ombe wawili waume, na kondoo waume watano, na mbuzi waume watano, na wana-kondoo watano waume wa mwaka wa kwanza; hayo ndiyo matoleo ya Eliasafu mwana wa Deueli.
48 Siku ya saba Elishama mwana wa Amihudi, mkuu wa wana wa Efraimu;
Nombres 1.10 Nombres 2.18
49 matoleo yake yalikuwa sahani moja ya fedha, uzani wake ni shekeli mia na thelathini, na bakuli moja ya fedha, uzani wake shekeli sabini, kwa shekeli ya mahali patakatifu; vyombo hivyo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, kuwa sadaka ya unga;
50 na kijiko kimoja cha dhahabu, uzani wake shekeli kumi, kilichojaa uvumba;
51 na ng’ombe mmoja mume mchanga, na kondoo mume mmoja, na mwana-kondoo mume mmoja wa mwaka wa kwanza, kuwa sadaka ya kuteketezwa;
52 na mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi;
53 tena kwa ajili ya dhabihu ya sadaka za amani, ng’ombe wawili waume, na kondoo waume watano, na mbuzi waume watano, na wana-kondoo watano waume wa mwaka wa kwanza; hayo ndiyo matoleo ya Elishama mwana wa Amihudi.
54 Siku ya nane Gamalieli mwana wa Pedasuri, mkuu wa wana wa Manase;
Nombres 1.10 Nombres 2.20
55 matoleo yake yalikuwa sahani moja ya fedha, uzani wake ni shekeli mia na thelathini, na bakuli moja ya fedha, uzani wake shekeli sabini, kwa shekeli ya mahali patakatifu; vyombo hivyo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, kuwa sadaka ya unga;
56 na kijiko kimoja cha dhahabu, uzani wake shekeli kumi, kilichojaa uvumba;
57 na ng’ombe mmoja mume mchanga, na kondoo mume mmoja, na mwana-kondoo mume mmoja wa mwaka wa kwanza, kuwa sadaka ya kuteketezwa;
58 na mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi;
59 tena kwa ajili ya dhabihu ya sadaka za amani, ng’ombe wawili waume, na kondoo waume watano, na mbuzi waume watano, na wana-kondoo watano waume wa mwaka wa kwanza; hayo ndiyo matoleo ya Gamalieli mwana wa Pedasuri.
60 Siku ya kenda Abidani mwana wa Gideoni, mkuu wa wana wa Benyamini;
Nombres 1.11 Nombres 2.22
61 matoleo yake yalikuwa sahani moja ya fedha, uzani wake ni shekeli mia na thelathini, na bakuli moja ya fedha, uzani wake shekeli sabini, kwa shekeli ya mahali patakatifu; vyombo hivyo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, kuwa sadaka ya unga;
62 na kijiko kimoja cha dhahabu, uzani wake shekeli kumi, kilichojaa uvumba;
Philippiens 4.18 Daniel 9.27 Hébreux 13.15 Esaïe 66.20 Psaumes 112.2
63 na ng’ombe mmoja mume mchanga, na kondoo mume mmoja, na mwana-kondoo mume mmoja wa mwaka wa kwanza, kuwa sadaka ya kuteketezwa;
64 na mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi;
65 tena kwa ajili ya dhabihu ya sadaka za amani, ng’ombe wawili waume, na kondoo waume watano, na mbuzi waume watano, na wana-kondoo watano waume wa mwaka wa kwanza; hayo ndiyo matoleo ya Abidani mwana wa Gideoni.
66 Siku ya kumi Ahiezeri mwana wa Amishadai, mkuu wa wana wa Dani;
Nombres 1.12 Nombres 2.25
67 matoleo yake yalikuwa sahani moja ya fedha, uzani wake ni shekeli mia na thelathini, na bakuli moja ya fedha, uzani wake shekeli sabini, kwa shekeli ya mahali patakatifu; vyombo hivyo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, kuwa sadaka ya unga;
68 na kijiko kimoja cha dhahabu, uzani wake shekeli kumi, kilichojaa uvumba;
69 na ng’ombe mmoja mume mchanga, na kondoo mume mmoja, na mwana-kondoo mume mmoja wa mwaka wa kwanza, kuwa sadaka ya kuteketezwa;
70 na mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi;
71 tena kwa ajili ya dhabihu ya sadaka za amani, ng’ombe wawili waume, na kondoo waume watano, na mbuzi waume watano, na wana-kondoo watano waume wa mwaka wa kwanza; hayo ndiyo matoleo ya Ahiezeri mwana wa Amishadai.
72 Na siku ya kumi na moja Pagieli mwana wa Okrani, mkuu wa wana wa Asheri;
Nombres 1.13 Nombres 2.27
73 matoleo yake yalikuwa sahani moja ya fedha, uzani wake ni shekeli mia na thelathini, na bakuli moja ya fedha, uzani wake shekeli sabini, kwa shekeli ya mahali patakatifu; vyombo hivyo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, kuwa sadaka ya unga;
Nombres 7.13-7.88
74 na kijiko kimoja cha dhahabu, uzani wake shekeli kumi, kilichojaa uvumba;
75 na ng’ombe mmoja mume mchanga, na kondoo mume mmoja, na mwana-kondoo mume mmoja wa mwaka wa kwanza, kuwa sadaka ya kuteketezwa;
76 na mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi;
77 tena kwa ajili ya dhabihu ya sadaka za amani, ng’ombe wawili waume, na kondoo waume watano, na mbuzi waume watano, na wana-kondoo watano waume wa mwaka wa kwanza; hayo ndiyo matoleo ya Pagieli mwana wa Okrani.
78 Na siku ya kumi na mbili Ahira mwana wa Enani, mkuu wa wana wa Naftali;
Nombres 1.15 Nombres 2.29
79 matoleo yake yalikuwa sahani moja ya fedha, uzani wake ni shekeli mia na thelathini, na bakuli moja ya fedha, uzani wake shekeli sabini, kwa shekeli ya mahali patakatifu; vyombo hivyo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, kuwa sadaka ya unga;
80 na kijiko kimoja cha dhahabu, uzani wake shekeli kumi, kilichojaa uvumba;
81 na ng’ombe mmoja mume mchanga, na kondoo mume mmoja, na mwana-kondoo mume mmoja wa mwaka wa kwanza, kuwa sadaka ya kuteketezwa;
82 na mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi;
83 tena kwa ajili ya dhabihu ya sadaka za amani, ng’ombe wawili waume, na kondoo waume watano, na mbuzi waume watano, na wana-kondoo watano waume wa mwaka wa kwanza; hayo ndiyo matoleo ya Ahira mwana wa Enani.
84 Hayo ndiyo matoleo yaliyotolewa na wakuu wa Israeli kwa ajili ya kuiweka wakfu madhabahu, siku hiyo ilipotiwa mafuta; sahani za fedha kumi na mbili, na bakuli za fedha kumi na mbili, na vijiko vya dhahabu kumi na viwili;
Nombres 7.10 Hébreux 13.10 Nombres 7.1 Apocalypse 21.14 Esdras 2.68-2.69
85 kila sahani ya fedha uzani wake ni shekeli mia na thelathini, na kila bakuli uzani wake ni shekeli sabini; fedha yote ya vile vyombo ilikuwa shekeli elfu mbili na mia nne, kwa shekeli ya mahali patakatifu;
Esdras 8.25-8.26 1 Chroniques 29.7 1 Chroniques 29.4 1 Chroniques 22.14
86 na vijiko vya dhahabu vilivyojaa uvumba kumi na viwili, uzani wake kila kijiko shekeli kumi, kwa shekeli ya mahali patakatifu; dhahabu yote ya vile vijiko ilikuwa shekeli mia na ishirini;
87 ng’ombe wote waliokuwa wa sadaka ya kuteketezwa walikuwa ng’ombe waume kumi na wawili, na hao kondoo waume walikuwa kumi na wawili, na wana-kondoo waume wa mwaka wa kwanza walikuwa kumi na wawili, pamoja na sadaka yao ya unga; na mbuzi waume wa sadaka ya dhambi ni kumi na wawili;
88 na ng’ombe wote waliokuwa wa dhabihu ya sadaka za amani ni ng’ombe waume ishirini na wanne, na hao kondoo waume walikuwa ni sitini, na hao mbuzi waume walikuwa ni sitini, na wana-kondoo waume wa mwaka wa kwanza walikuwa sitini. Hayo ndiyo matoleo yaliyotolewa kwa ajili ya kuiweka wakfu madhabahu, baada ya hiyo madhabahu kutiwa mafuta.
Nombres 7.10 Nombres 7.1 Nombres 7.84
89 Kisha, Musa alipoingia ndani ya hema ya kukutania ili kunena na Mungu ndipo alipoisikia Sauti ikinena naye kutoka hapo juu ya kiti cha rehema, kilichokuwa juu ya sanduku la ushahidi, ikitoka kati ya yale makerubi mawili; naye akanena naye.
Psaumes 80.1 Exode 33.9-33.11 Nombres 12.8 Hébreux 4.16 Nombres 1.1

Cette Bible est dans le domaine public.