Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Nombres 31.9
Bible en Swahili de l’est


Dernières responsabilités de Moïse

Victoire sur Madian

1 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
2 Walipize kisasi wana wa Israeli juu ya Wamidiani; kisha baadaye utakusanywa uwe pamoja na watu wako.
Nombres 27.13 Nombres 31.3 Esaïe 1.24 Nahum 1.2 Nombres 25.14-25.18
3 Basi Musa akanena na watu, na kuwaambia, Wavikeni silaha watu miongoni mwenu waende vitani, ili waende kupigana na Midiani, wapate kumlipiza kisasi Bwana, juu ya Midiani.
Lévitique 26.25 Jérémie 46.10 2 Rois 9.7 2 Rois 10.30 Nombres 25.11
4 Katika kila kabila mtatoa watu elfu, katika kabila zote za Israeli, nanyi mtawapeleka waende vitani.
Lévitique 26.8 1 Samuel 14.6 Juges 7.2
5 Basi walitolewa katika maelfu ya Israeli, elfu moja ya kila kabila, watu waume kumi na mbili elfu walioandaliwa kwa vita.
6 Basi Musa akawapeleka, watu elfu wa kila kabila waende vitani, wao na Finehasi mwana wa Eleazari kuhani, waende vitani, na vile vyombo vya mahali patakatifu, na hizo tarumbeta za kupiga sauti za kugutusha mkononi mwake.
Nombres 14.44 Nombres 10.8-10.9 Nombres 33.20-33.22 1 Samuel 4.17 1 Samuel 23.9
7 Nao wakapigana na Midiani kama Bwana alivyomwagiza Musa; nao wakamwua kila mume.
Juges 21.11 1 Rois 11.15-11.16 1 Samuel 27.9 Juges 6.33 Juges 6.1-6.2
8 Nao wafalme wa Midiani wakawaua pamoja na watu wengine waliouawa; Evi, na Rekemu, na Suri, na Huri, na Reba, hao wafalme watano wa Midiani; Balaamu mwana wa Beori naye wakamwua kwa upanga.
Nombres 25.15 Josué 13.21-13.22 Nombres 25.18 Nombres 22.4 Apocalypse 2.14
9 Wana wa Israeli wakawachukua mateka wanawake wa Midiani na watoto wao; na ng’ombe zao wote, na kondoo zao wote, na mali zao zote, wakachukua nyara.
2 Chroniques 28.8-28.10 2 Chroniques 28.5 Nombres 31.15-31.16 Deutéronome 20.14
10 Na miji yao yote, kila mahali walipokuwa wakikaa, na marago yao yote wakayateketeza kwa moto.
1 Rois 9.16 Esaïe 1.7 1 Samuel 30.1 Genèse 25.16 Apocalypse 18.8
11 Nao wakatwaa hizo nyara zote, na mateka yote, ya wanadamu na ya wanyama.
Deutéronome 20.14 Josué 8.2
12 Nao wakawaleta mateka ya wanadamu, na mateka ya wanyama, na hizo nyara, na kuyaweka mbele ya Musa, na mbele ya Eleazari kuhani, na mbele ya mkutano wa wana wa Israeli, hapo maragoni katika nchi tambarare za Moabu, zilizo karibu na Yordani hapo Yeriko.
Nombres 22.1
13 Basi Musa, na Eleazari kuhani, na wakuu wote wa huo mkutano, wakatoka nje kwenda kuwalaki nje ya marago.
Nombres 31.12 Nombres 5.2 Genèse 14.17 1 Samuel 30.21 Nombres 31.22-31.24
14 Musa akawakasirikia majemadari wa jeshi, na hao maakida wa elfu elfu, na wakuu wa mia mia, hao waliorudi kutoka katika kupiga vita.
Exode 32.19 Exode 32.22 Nombres 12.3 Ephésiens 4.26 Lévitique 10.16
15 Musa akawauliza, Je! Mmewaponya wanawake wote hai?
1 Samuel 15.3 Deutéronome 20.13 Josué 10.40 Josué 8.25 Jérémie 48.10
16 Tazama, hawa ndio waliowakosesha wana wa Israeli, kwa shauri la Balaamu, wamfanyie Bwana dhambi katika hilo jambo la Peori, na kwa hivyo pigo lilikuwa katika mkutano wa Bwana.
2 Pierre 2.15 Nombres 25.1-25.9 Apocalypse 2.14 Deutéronome 4.3 Josué 22.17
17 Basi kwa ajili hiyo mwueni kila mume katika hao watoto, na kila mwanamke aliyemjua mume kwa kulala pamoja naye.
Deutéronome 7.2 Deutéronome 20.16-20.18 Juges 21.11-21.12
18 Lakini hao watoto wote wa kike ambao hawakumjua mume kwa kulala pamoja naye, mtawaweka hai kwa ajili yenu.
Deutéronome 21.10-21.14 Lévitique 25.44 2 Chroniques 28.8-28.10 Esaïe 14.2 Deutéronome 20.14
19 Nanyi fanyeni matuo yenu nje ya marago muda wa siku saba; mtu awaye yote aliyemwua mtu, na awaye yote aliyemgusa mtu aliyeuawa, jitakaseni nafsi zenu siku ya tatu, na siku ya saba, ninyi na mateka yenu.
Nombres 19.11-19.22 Nombres 5.2 1 Chroniques 22.8
20 Na katika habari ya kila nguo, na kila kitu kilichofanywa cha ngozi, na kazi yote ya singa za mbuzi, na vyombo vyote vilivyofanywa vya mti, mtajitakasa wenyewe;
Genèse 35.2 Nombres 19.14-19.16 Nombres 19.22 Exode 19.10
21 Kisha Eleazari kuhani akawaambia waume wa vita wote waliokwenda vitani, Hii ndiyo amri ya sheria Bwana aliyomwagiza Musa;
Nombres 30.16
22 lakini dhahabu, na fedha, na shaba, na chuma, na bati, na risasi,
23 kila kitu kiwezacho kuuhimili moto, mtakipitisha katika moto, nacho kitakuwa safi, pamoja na haya kitatakaswa kwa hayo maji ya farakano; na kila kitu kisichouhimili moto mtakipitisha katika hayo maji.
Nombres 19.9 Nombres 19.17 1 Corinthiens 3.13 Esaïe 43.2 Matthieu 3.11
24 Nanyi mtazifua nguo zenu siku ya saba, nanyi mtakuwa safi, kisha baadaye mtaingia maragoni.
Lévitique 11.25 Lévitique 14.9 Lévitique 15.13 Nombres 19.19
25 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
26 Fanya jumla ya hayo mateka ya wanadamu, na ya wanyama pia, wewe, na Eleazari kuhani, na wakuu wa nyumba za baba za mkutano;
27 ukagawanye nyara mafungu mawili; kati ya watu waliozoea vita, waliotoka nje waende vitani, na huo mkutano wote;
Josué 22.8 1 Samuel 30.24-30.25 1 Samuel 30.4 Psaumes 68.12
28 kisha uwatoze hao watu wa vita waliotoka kwenda vitani sehemu kwa ajili ya Bwana; mmoja katika mia tano, katika wanadamu, na katika ng’ombe, na katika punda, na katika kondoo;
Nombres 18.26 Nombres 31.47 Nombres 31.30 1 Chroniques 18.11 Josué 6.19
29 twaa katika nusu yao, ukampe Eleazari kuhani, kuwa sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
Deutéronome 12.12 Exode 29.27 Deutéronome 12.19 Nombres 18.26
30 Na katika hiyo nusu ya wana wa Israeli utatwaa mmoja atakayetolewa katika kila hamsini, katika wanadamu, na katika ng’ombe, na katika punda, na katika kondoo, maana, katika wanyama wote, ukawape Walawi, hao walindao ulinzi wa maskani ya Bwana.
Nombres 3.31 Nombres 3.7-3.8 Nombres 3.25 1 Chroniques 26.20-26.27 1 Corinthiens 9.13-9.14
31 Musa na Eleazari kuhani wakafanya kama Bwana alivyomwagiza Musa.
32 Basi masazo ya hizo nyara walizotwaa watu wa vita, zilikuwa ni kondoo mia sita na sabini na tano elfu,
33 na ng’ombe sabini na mbili elfu,
34 na punda sitini na moja elfu,
35 tena wanadamu jumla yao ilikuwa thelathini na mbili elfu, katika hao wanawake ambao hawakumjua mume kwa kulala pamoja naye.
36 Na hiyo nusu ambayo ilikuwa ni sehemu ya hao waliotoka kwenda vitani, hesabu yake ilikuwa kondoo mia tatu na thelathini na saba elfu na mia tano;
37 na kodi ya Bwana katika hao kondoo ilikuwa kondoo mia sita na sabini na watano.
38 Tena, ng’ombe walikuwa thelathini na sita elfu; na katika hao kodi ya Bwana ilikuwa ng’ombe sabini na wawili.
39 Na punda walikuwa thelathini elfuna mia tano, katika hao kodi ya Bwana ilikuwa punda sitini na mmoja.
40 Na wanadamu walikuwa watu kumi na sita elfu; katika hao sehemu ya Bwana ilikuwa ni watu thelathini na wawili.
41 Basi Musa akampa Eleazari kuhani hiyo sehemu, iliyokuwa sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana, kama Bwana alivyomwagiza Musa.
Nombres 18.8 Nombres 18.19 Hébreux 7.9-7.12 Nombres 31.29-31.31 Hébreux 7.4-7.6
42 Tena katika hiyo nusu iliyokuwa ya wana wa Israeli, ambayo Musa aliitenga na watu waliokwenda vitani,
43 (basi hiyo nusu ya mkutano ilikuwa ni kondoo mia tatu na thelathini na saba elfu na mia tano,
44 na ng’ombe thelathini na sita elfu,
45 na punda thelathini elfu, na mia tano,
46 na wanadamu kumi na sita elfu;)
47 na katika hiyo nusu iliyokuwa ya wana wa Israeli, Musa akatwaa mmoja aliyetolewa katika kila hamsini, wa binadamu na wa wanyama, akawapa Walawi, waliolinda ulinzi wa maskani ya Bwana; kama Bwana alivyomwagiza Musa.
Nombres 31.30 1 Thessaloniciens 5.12-5.13 Nombres 18.21-18.24 Luc 10.1-10.8 Deutéronome 12.17-12.19
48 Na majemadari waliokuwa juu ya elfu elfu za hiyo jeshi, na maakida wa elfu elfu, na maakida wa mia mia, wakamkaribia Musa;
49 wakamwambia Musa wakisema, Sisi watumishi wako tumefanya jumla ya hesabu ya watu wa vita walio chini ya mikono yetu, na hapana hata mmoja aliyetupungukia.
Jean 18.9 1 Samuel 30.18-30.19 Psaumes 72.14
50 Nasi tumeleta matoleo ya Bwana, aliyopata kila mtu, ya vyombo vya dhahabu, na mitali, na timbi, na pete za muhuri, na vipini, na vikuku, ili kuzifanyia upatanisho nafsi zetu mbele ya Bwana.
Exode 30.12 Exode 30.15-30.16 Lévitique 17.11 Psaumes 116.12 Psaumes 116.17
51 Musa na Eleazari kuhani wakapokea kwao hiyo dhahabu, maana, vile vyombo vyote vilivyofanyizwa.
Nombres 7.2-7.6
52 Na dhahabu yote ya sadaka ya kuinuliwa waliyosongeza kwa Bwana, ya maakida wa elfu elfu, na maakida wa mia mia, ilikuwa shekeli kumi na sita elfu na mia saba na hamsini.
53 (Kwa kuwa hao watu wa vita walikuwa wametwaa nyara, kila mtu nafsi yake.)
Deutéronome 20.14 Nombres 31.32
54 Basi Musa na Eleazari kuhani wakapokea hiyo dhahabu mikononi mwa hao maakida wa elfu elfu na wa mia mia, na kuileta ndani ya hema ya kukutania, ili iwe ukumbusho kwa ajili ya wana wa Israeli mbele za Bwana.
Exode 30.16 Josué 4.7 Actes 10.4 Zacharie 6.14 Psaumes 103.1-103.2

Cette Bible est dans le domaine public.