Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 46.7
Bible en Swahili de l’est


Prophéties sur les nations

Prophétie sur l’Égypte

1 Neno la Bwana lililomjia Yeremia, nabii, katika habari za mataifa.
Jérémie 1.10 Nombres 23.9 Jérémie 4.7 Zacharie 2.8 Romains 3.29
2 Katika habari za Misri; habari za jeshi la Farao Neko, mfalme wa Misri, lililokuwa karibu na mto Frati katika Karkemishi, ambalo Nebukadreza, mfalme wa Babeli, alilipiga katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda.
2 Rois 23.29 Jérémie 45.1 Jérémie 46.14 Jérémie 25.1 Ezéchiel 29.1-29.21
3 Tengenezeni kigao na ngao, mkakaribie ili kupigana.
Esaïe 21.5 Nahum 3.14 Joël 3.9 Nahum 2.1 Jérémie 51.11-51.12
4 Watandikeni farasi; pandeni, enyi mpandao farasi; simameni na chapeo zenu, isugueni mikuki; zivaeni dirii.
Ezéchiel 21.9-21.11 Jérémie 51.3 Ezéchiel 21.28 1 Samuel 17.38 Néhémie 4.16
5 Nimeyaona haya kwa sababu gani? Wamefadhaika, wamerudi nyuma; mashujaa wao wamevunjika-vunjika; wanakimbia upesi sana, hawatazami nyuma; hofu ziko pande zote; asema Bwana.
Jérémie 6.25 Jérémie 49.29 Jérémie 46.21 Jérémie 20.3-20.4 Apocalypse 6.15-6.17
6 Mtu mwepesi asikimbie, wala shujaa asiokoke; pande za kaskazini karibu na mto Frati wamejikwaa na kuanguka.
Daniel 11.19 Jérémie 46.12 Psaumes 33.16-33.17 Jérémie 46.10 Jérémie 4.6
7 Nani huyu ajiinuaye kama mto Nile, Ambaye maji yake yanajirusha kama mito?
Jérémie 47.2 Daniel 11.22 Esaïe 8.7-8.8 Cantique 3.6 Apocalypse 12.15
8 Misri anajiinua kama mto Nile, Na maji yake yanajirusha kama mito; Asema, Nitajiinua, nitaifunikiza nchi; Nitauharibu mji na hao wakaao ndani yake.
Esaïe 10.13-10.16 Ezéchiel 32.2 Esaïe 37.24-37.26 Ezéchiel 29.3 Exode 15.9-15.10
9 Haya! Pandeni, enyi farasi; Jihimizeni, enyi magari ya vita; Mashujaa nao na watoke nje Kushi na Puti, watumiao ngao; Nao Waludi, washikao uta na kuupeta.
Esaïe 66.19 Ezéchiel 27.10 Nahum 3.9 Genèse 10.13 1 Chroniques 1.11
10 Maana hiyo ni siku ya Bwana, Bwana wa majeshi, Siku ya kisasi, ili ajilipize kisasi juu ya adui zake; Nao upanga utakula na kushiba, Utakunywa damu yao hata kukinai; Maana Bwana, Bwana wa majeshi, ana sadaka yake Katika nchi ya kaskazini karibu na mto Frati.
Joël 1.15 Deutéronome 32.42 Jérémie 46.2 Jérémie 46.6 Apocalypse 19.17-19.21
11 Panda uende Gileadi, ukatwae zeri, Ee binti, bikira wa Misri; unatumia dawa nyingi bure tu; hupati kupona kamwe.
Jérémie 8.22 Esaïe 47.1 Michée 1.9 Nahum 3.19 Ezéchiel 27.17
12 Mataifa wamesikia habari za aibu yako, nayo dunia imejaa kilio chako; maana shujaa amejikwaa juu ya shujaa mwenzake, wameanguka wote wawili pamoja.
Nahum 3.8-3.10 Jérémie 46.6 Esaïe 19.2 Jérémie 14.2 Jérémie 49.21
13 Neno hili ndilo ambalo Bwana alimwambia Yeremia, nabii, kueleza jinsi Nebukadreza, mfalme wa Babeli, atakavyokuja na kuipiga nchi ya Misri.
Jérémie 44.30 Jérémie 43.10-43.13 Esaïe 19.1-19.25 Esaïe 29.1-29.24
14 Tangazeni habari hii katika Misri, mkaihubiri katika Migdoli, na kuihubiri katika Nofu, na Tahpanesi; semeni, Simama, ujifanye tayari kwa maana upanga umekula pande zako zote.
Jérémie 44.1 Jérémie 46.10 Jérémie 43.8-43.9 Jérémie 2.30 Esaïe 1.20
15 Mbona mashujaa wako wamechukuliwa mbali? Hawakusimama kwa sababu Bwana aliwafukuza.
Esaïe 66.15-66.16 Psaumes 18.14 Jérémie 46.5 Psaumes 18.39 Psaumes 68.2
16 Aliwakwaza wengi, naam, wakaangukiana wao kwa wao; wakasema, Haya! Na tuondoke, tukarudi kwa watu wetu wenyewe, hata nchi tuliyozaliwa, tuukimbie upanga unaotuonea.
Jérémie 51.9 Lévitique 26.36-26.37 Jérémie 50.16 Jérémie 46.21 Jérémie 46.6
17 Wakalia huko, Farao, mfalme wa Misri, ni kishindo tu; muhula alioandikiwa ameuacha upite.
Esaïe 19.11-19.16 1 Rois 20.10 Exode 15.9 1 Rois 20.18 Ezéchiel 31.18
18 Kama mimi niishivyo, asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana wa majeshi, hakika yake, kama Tabori katika milima, na kama Karmeli karibu na bahari, ndivyo atakavyokuja.
Jérémie 48.15 Josué 19.22 Juges 4.6 Esaïe 48.2 Malachie 1.14
19 Ee binti ukaaye katika Misri, Ujiweke tayari kwenda zako hali ya kufungwa; Kwa maana Nofu utakuwa ukiwa, Utateketezwa, usikaliwe na watu.
Esaïe 20.4 Jérémie 48.18 Ezéchiel 30.13 Jérémie 44.1 Jérémie 26.9
20 Misri ni mtamba mzuri sana, lakini uharibifu umekuja, Umekuja utokao pande za kaskazini.
Jérémie 47.2 Osée 10.11 Jérémie 46.6 Jérémie 46.10 Jérémie 1.14
21 Na watu wake waliojiwa, walio kati yake, Ni kama ndama waliowanda malishoni; Maana wao nao wamerudi nyuma, Wamekimbia wote pamoja, wasisimame; Maana siku ya msiba wao imewafikilia, Wakati wa kujiliwa kwao.
Jérémie 46.5 2 Rois 7.6 Abdias 1.13 Esaïe 34.7 Psaumes 37.13
22 Sauti yake ni kama nyoka, wajapo kwa nguvu, Watamjia na mashoka, kama wachanja kuni.
Esaïe 29.4 Esaïe 14.8 Michée 1.8 Esaïe 37.24 Zacharie 11.2
23 Wataukata msitu wake, asema Bwana, ingawa haupenyeki; Kwa maana ni wengi kuliko nzige, hawahesabiki.
Juges 7.12 Juges 6.5 Joël 2.25 Esaïe 10.18 Ezéchiel 20.46
24 Binti ya Misri ataaibishwa; Atatiwa mikononi mwa watu wa kaskazini.
Jérémie 1.15 Jérémie 46.11 Psaumes 137.8 Jérémie 46.19-46.20 Ezéchiel 29.1-29.21
25 Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Tazama, nitamwadhibu Amoni wa No, na Farao, na Misri, pamoja na miungu yake, na wafalme wake, naam, Farao, na hao wanaomtumainia;
Esaïe 20.5-20.6 Exode 12.12 Sophonie 2.11 Jérémie 43.12-43.13 Ezéchiel 32.9-32.12
26 nami nitawatia katika mikono ya hao wanaowatafuta roho zao, na katika mikono ya Nebukadreza, mfalme wa Babeli, na katika mikono ya watumishi wake; na baada ya hayo itakaliwa na watu, kama katika siku za kale, asema Bwana.
Ezéchiel 32.11 Jérémie 44.30 Ezéchiel 29.8-29.14 Jérémie 48.47 Jérémie 49.39
27 Lakini usiogope wewe, Ee Yakobo, mtumishi wangu; wala usifadhaike, Ee Israeli; kwa maana, tazama, nitakuokoa toka mbali, na wazao wako toka nchi ya uhamisho wao; na Yakobo atarudi, naye atatulia na kustarehe, wala hapana mtu atakayemtia hofu.
Jérémie 30.10-30.11 Jérémie 50.19 Esaïe 43.5 Esaïe 41.13-41.14 Jérémie 23.3-23.4
28 Usiogope wewe, Ee Yakobo, mtumishi wangu, asema Bwana; kwa maana mimi ni pamoja nawe; maana nitawakomesha kabisa mataifa yote huko nilikokufukuza, bali sitakukomesha wewe kabisa; lakini nitakurudi kwa hukumu, wala sitakuacha bila adhabu.
Jérémie 4.27 Jérémie 10.24 Jérémie 30.11 Hébreux 12.5-12.10 1 Corinthiens 11.32

Cette Bible est dans le domaine public.