Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 3.21
Bible en Swahili de l’est


1 Watu husema, Mtu akimwacha mkewe, naye akienda zake, akawa mke wa mtu mwingine, je! Mtu huyo atamrudia tena? Je! Nchi hiyo haitatiwa unajisi? Lakini wewe umefanya mambo ya ukahaba na wapenzi wengi; nawe, je! Utanirudia mimi? Asema Bwana.
Deutéronome 24.1-24.4 Jérémie 2.20 Jérémie 4.1 Ezéchiel 16.26 Osée 2.5-2.7
2 Inua macho yako, ukavitazame vilele vya milima, ukaone; pa wapi mahali ambapo hawakulala nawe? Kando ya njia umeketi ili kuwangojea, kama vile Mwarabu jangwani; nawe umeitia nchi unajisi kwa ukahaba wako na uovu wako.
Genèse 38.14 Jérémie 2.7 Ezéchiel 16.24-16.25 Deutéronome 12.2 Jérémie 3.1
3 Kwa sababu hiyo manyunyu yamezuiliwa, wala hapakuwa na mvua ya vuli; hata hivyo ulikuwa na kipaji cha uso cha kahaba, ulikataa kutahayarika.
Jérémie 14.4 Lévitique 26.19 Deutéronome 28.23 Jérémie 14.22 Esaïe 5.6
4 Je, tokea wakati huu hutanililia, Ee Baba yangu, wewe u kiongozi wa ujana wangu?
Jérémie 3.19 Jérémie 2.2 Osée 2.15 Jérémie 31.9 Proverbes 2.17
5 Je! Ataishika hasira yake hata milele? Ataishika hata mwisho? Tazama, umesema hivyo, bali umetenda mambo mabaya, umefuata njia yako mwenyewe.
Esaïe 57.16 Jérémie 3.12 Esaïe 64.9 Ezéchiel 22.6 Michée 2.1

Appel à revenir à Dieu

6 Tena, Bwana akaniambia siku za mfalme Yosia, Je! Umeyaona aliyotenda Israeli mwenye kuasi? Amepanda juu ya kila mlima mrefu, akafanya huko mambo ya ukahaba, tena, chini ya kila mti wenye majani mabichi.
Ezéchiel 16.31 2 Rois 17.7-17.17 1 Rois 14.23 Ezéchiel 16.24-16.25 Jérémie 7.24
7 Nami nalisema baada ya yeye kuyatenda hayo yote, Atanirudia mimi, lakini hakurudi; na dada yake, Yuda mwenye hiana, akayaona hayo.
Ezéchiel 16.46 Osée 14.1 Jérémie 3.8-3.11 2 Chroniques 30.6-30.12 Osée 6.1-6.4
8 Nami nikaona, wakati nilipokuwa nimemwacha Israeli mwenye kuasi, nikampa hati ya talaka kwa sababu hiyo ya kuzini, dada yake, Yuda mwenye hiana, hakufanya hofu; bali yeye naye akaenda akafanya mambo ya ukahaba.
Deutéronome 24.1 Jérémie 3.1 Esaïe 50.1 2 Rois 18.9-18.11 Ezéchiel 23.9
9 Hata ikawa, kwa sababu alikuwa mwepesi wa kufanya ukahaba, nchi ikatiwa unajisi, naye akazini na mawe na miti.
Jérémie 2.27 Jérémie 3.2 Esaïe 57.6 Jérémie 10.8 Jérémie 2.7
10 Na pamoja na hayo yote dada yake, Yuda mwenye hiana, hajanirudia mimi kwa moyo wake wote, bali kwa unafiki, asema Bwana.
Osée 7.14 Psaumes 18.44 2 Chroniques 34.33-35.18 Psaumes 78.36-78.37 Esaïe 10.6
11 Bwana, akaniambia, Israeli mwenye kuasi amejionyesha kuwa mwenye haki kuliko Yuda mwenye hiana.
Ezéchiel 16.51-16.52 Ezéchiel 23.11 Osée 11.7 Osée 4.16 Ezéchiel 16.47
12 Enenda, ukatangaze maneno haya kuelekea upande wa kaskazini, ukaseme, Rudi, Ee Israeli mwenye kuasi, asema Bwana; sitakutazama kwa hasira; maana mimi ni mwenye rehema, asema Bwana, sitashika hasira hata milele.
Psaumes 86.15 Ezéchiel 33.11 Jérémie 33.26 2 Rois 17.6 Jérémie 3.18
13 Ungama uovu wako tu; ya kwamba umemwasi Bwana, Mungu wako, na njia zako zimekuwa nyingi kuwaendea wageni chini ya kila mti wenye majani mabichi, wala hamkuitii sauti yangu, asema Bwana.
Deutéronome 30.1-30.3 Jérémie 2.25 Jérémie 3.25 Deutéronome 12.2 Jérémie 3.6
14 Rudini, enyi watoto wenye kuasi, asema Bwana; maana mimi ni mume wenu; nami nitatwaa mtu mmoja wa mji mmoja, na wawili wa jamaa moja, nami nitawaleta hata Sayuni;
Osée 2.19-2.20 Esaïe 54.5 Jérémie 31.32 Jérémie 31.8-31.10 Jérémie 23.3
15 nami nitawapa ninyi wachungaji wanipendezao moyo wangu, watakaowalisha kwa maarifa na fahamu.
Jérémie 23.4 Actes 20.28 Ezéchiel 34.23 Ephésiens 4.11-4.12 Jean 21.15-21.17
16 Kisha itakuwa, mtakapoongezeka na kuwa wengi katika nchi hiyo, asema Bwana, siku zile hawatasema tena, Sanduku la agano la Bwana; wala halitaingia moyoni; wala hawatalikumbuka, wala hawatalizuru, wala hayatafanyika hayo tena.
Esaïe 65.17 Jérémie 31.27 Osée 1.10-1.11 Esaïe 66.1-66.2 Esaïe 60.22
17 Wakati ule watauita Yerusalemu kiti cha enzi cha Bwana; na mataifa yote watakusanyika huko Yerusalemu, kwa ajili ya jina la Bwana; wala hawatakwenda tena kwa ukaidi wa moyo wao mbaya.
Jérémie 11.8 Jérémie 17.12 Ezéchiel 43.7 Jérémie 31.23 Psaumes 87.3
18 Siku zile nyumba ya Yuda watakwenda pamoja na nyumba ya Israeli, nao watakuja pamoja, kutoka nchi ya kaskazini, mpaka nchi ile niliyowapa baba zenu iwe urithi wao.
Jérémie 31.8 Jérémie 50.4 Osée 1.11 Amos 9.15 Jérémie 16.15
19 Lakini mimi nalisema, Nitawezaje kukuweka pamoja na watoto, na kukupa nchi ipendezayo, urithi ulio mwema wa mataifa? Nami nikasema, Mtaniita, Baba yangu, wala hamtageuka na kuacha kunifuata.
Jérémie 3.4 Esaïe 63.16 Jérémie 12.10 Jérémie 32.39-32.40 2 Corinthiens 6.17-6.18
20 Hakika kama vile mke amwachavyo mumewe kwa hiana, ndivyo mlivyonitenda mimi kwa hiana, Ee nyumba ya Israeli, asema Bwana.
Jérémie 5.11 Esaïe 48.8 Jérémie 3.8-3.10 Osée 6.7 Osée 5.7
21 Sauti inasikiwa juu ya vilele vya milima, ni kulia kwao na maombi yao wana wa Israeli; kwa kuwa wameipotosha njia yao, wamemsahau Bwana, Mungu wao.
Jérémie 31.9 Jérémie 2.32 2 Corinthiens 7.10 Esaïe 15.2 Esaïe 17.10
22 Rudini, enyi watoto waasi, mimi nitaponya maasi yenu. Tazama, tumekuja kwako; maana wewe u Bwana, Mungu wetu.
Osée 14.4 Osée 14.8 Esaïe 27.8 Zacharie 13.9 Cantique 1.4
23 Ni kweli, msaada haufai unaotazamiwa kutoka milimani, makutano yenye mshindo juu ya milima; ni kweli, wokovu wa Israeli ni katika Bwana, Mungu wetu.
Psaumes 3.8 Psaumes 121.1-121.2 Jérémie 17.14 Esaïe 12.2 Esaïe 45.17
24 Lakini kitu cha aibu kimeila kazi ya baba zetu tokea ujana wetu; makundi yao ya kondoo na ng’ombe, wana wao na binti zao.
Osée 9.10 Ezéchiel 16.63 Osée 10.6 Osée 2.8 Jérémie 11.13
25 Na tulale kwa aibu yetu, haya yetu na itufunike; kwa maana tumemwasi Bwana, Mungu wetu, sisi na baba zetu, tangu ujana wetu hata leo; wala hatukuitii sauti ya Bwana, Mungu wetu.
Jérémie 22.21 Ezéchiel 7.18 Psaumes 109.29 Jérémie 2.26 Jérémie 6.26

Cette Bible est dans le domaine public.