Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 23.4
Bible en Swahili de l’est


1 Ole wao wachungaji, wanaoharibu kondoo za malisho yangu na kuwatawanya! Asema Bwana.
Jérémie 10.21 Zacharie 11.15-11.17 Ezéchiel 34.2-34.10 Matthieu 9.36 Ezéchiel 13.3
2 Kwa sababu hiyo Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, juu ya wachungaji wanaowalisha watu wangu, Mmetawanya kundi langu, na kuwafukuza, wala hamkwenda kuwatazama; angalieni, nitawapatiliza uovu wa matendo yenu, asema Bwana.
Exode 32.34 Michée 7.4 Jérémie 21.12 Jérémie 5.29 Matthieu 25.43
3 Nami nitakusanya mabaki ya kundi langu, katika nchi zile zote nilizowafukuza, nami nitawaleta tena mazizini mwao; nao watazaa na kuongezeka.
Jérémie 32.37 Jérémie 31.8 Esaïe 43.5-43.6 Jérémie 29.14 Jérémie 30.3
4 Nami nitaweka juu yao wachungaji watakaowalisha; wala hawataona hofu tena, wala kufadhaika, wala hatapotea hata mmoja wao, asema Bwana.
Michée 5.4-5.5 1 Pierre 1.5 Jérémie 3.14-3.15 Jean 21.15-21.17 Ezéchiel 34.23-34.31
5 Tazama siku zinakuja, asema Bwana, nitakapomchipushia Daudi Chipukizi la haki; naye atamiliki mfalme, atatenda kwa hekima, naye atafanya hukumu na haki katika nchi.
Esaïe 4.2 Esaïe 52.13 Luc 1.32-1.33 Esaïe 53.2 Esaïe 9.7
6 Katika siku zake Yuda ataokolewa, na Israeli atakaa salama, na jina lake atakaloitwa ni hili, Bwana ni haki yetu.
1 Corinthiens 1.30 Romains 3.22 Jérémie 33.16 Matthieu 1.21-1.23 Philippiens 3.9
7 Kwa hiyo, angalia, siku zinakuja, asema Bwana, ambapo hawatasema tena, Aishivyo Bwana, aliyewatoa wana wa Israeli katika nchi ya Misri;
Jérémie 16.14-16.15 Jérémie 23.3 Esaïe 43.18-43.19 Jérémie 31.31-31.34
8 lakini, Aishivyo Bwana, aliyewapandisha na kuwaongoza wazao wa nyumba ya Israeli kutoka nchi ya kaskazini, na kutoka nchi zote nilikowafukuza; nao watakaa katika nchi yao wenyewe.
Esaïe 43.5-43.6 Amos 9.14-9.15 Ezéchiel 34.13 Esaïe 14.1 Esaïe 65.8-65.10

Les prétendus prophètes

9 Katika habari za manabii. Moyo wangu ndani yangu umevunjika, Mifupa yangu yote inatikisika. Nimekuwa kama mtu aliye mlevi, Na kama mtu aliyeshindwa na divai;kwa ajili ya Bwana,na kwa ajili ya maneno yake matakatifu.
Habakuk 3.16 Ezéchiel 9.6 Jérémie 25.15-25.18 Esaïe 51.21 Jérémie 14.17-14.18
10 Maana nchi imejaa wazinzi; kwa sababu ya kuapa nchi inaomboleza; malisho ya nyikani yamekauka; mwenendo wao ni mbaya, na nguvu zao si za haki.
Psaumes 107.34 Jérémie 9.10 Jérémie 9.2 Osée 4.2-4.3 Malachie 3.5
11 Maana nabii, na kuhani, wote wawili wanakufuru; naam, katika nyumba yangu nimeuona uovu wao, asema Bwana.
Jérémie 6.13 Sophonie 3.4 Ezéchiel 23.39 Jérémie 7.30 Ezéchiel 8.16
12 Kwa ajili ya hayo njia yao itakuwa kwao kama mahali pa kuteleza gizani; watatelemshwa na kuanguka hapo; kwa maana nitaleta uovu juu yao, naam, mwaka wa kujiliwa kwao, asema Bwana.
Psaumes 35.6 Jérémie 11.23 Jérémie 13.16 Proverbes 4.19 Psaumes 73.18
13 Nami nimeona upumbavu katika manabii wa Samaria; walitabiri kwa Baali, wakawakosesha watu wangu Israeli.
Jérémie 2.8 Esaïe 9.16 1 Rois 18.18-18.21 Osée 9.7-9.8 2 Chroniques 33.9
14 Katika manabii wa Yerusalemu nimeona neno linalochukiza sana; hufanya zinaa; huenenda katika maneno ya uongo, hutia nguvu mikono ya watendao maovu, hata ikawa hapana mtu arejeaye na kuuacha uovu wake; wote pia wamekuwa kama Sodoma kwangu, na wenyeji wake kama Gomora.
Jérémie 29.23 Esaïe 1.9-1.10 Ezéchiel 22.25 Jérémie 14.14 Jérémie 23.32
15 Basi Bwana wa majeshi asema hivi, katika habari ya manabii, Tazama, nitawalisha pakanga, nitawanywesha maji ya uchungu; kwa kuwa kutoka kwa manabii hao wa Yerusalemu kukufuru kumeingia katika nchi yote.
Jérémie 8.14 Jérémie 9.15 Matthieu 27.34 Lamentations 3.19 Lamentations 3.15
16 Bwana wa majeshi asema hivi, Msisikilize maneno ya manabii wakiwatabiria; huwafundisha ubatili; hunena maono ya mioyo yao wenyewe; hayakutoka katika kinywa cha Bwana.
Jérémie 27.9-27.10 Matthieu 7.15 Jérémie 14.14 2 Corinthiens 11.13-11.15 Jérémie 23.21
17 Daima huwaambia wao wanaonidharau, Bwana amesema, Mtakuwa na amani; nao humwambia kila mtu aendaye kwa ukaidi wa moyo wake, Hamtapatwa na ubaya wo wote.
Michée 3.11 Jérémie 13.10 Amos 9.10 Jérémie 8.11 Zacharie 10.2
18 Maana, ni nani aliyesimama katika baraza la Bwana, hata akalifahamu neno lake na kulisikia? Ni nani aliyelitia moyoni neno langu, na kulisikia?
Jérémie 23.22 1 Corinthiens 2.16 2 Chroniques 18.23 Psaumes 25.14 Jean 15.15
19 Tazama, tufani ya Bwana, yaani, ghadhabu yake, imetokea; ni dhoruba ya kisulisuli; itapasuka, na kuwaangukia waovu vichwani.
Jérémie 30.23 Jérémie 25.32 Amos 1.14 Psaumes 58.9 Proverbes 1.27
20 Hasira ya Bwana haitarudi, hata atakapokwisha kuyatimiza makusudi ya moyo wake; katika siku za mwisho mtalifahamu neno hili kabisa.
Jérémie 30.24 Genèse 49.1 Zacharie 1.6 Esaïe 14.24 Esaïe 55.11
21 Mimi sikuwatuma manabii hao, lakini walikwenda mbio; sikusema nao, lakini walitabiri.
Jérémie 14.14 Jérémie 27.15 Jérémie 23.32 Jérémie 29.31 Jean 20.21
22 Lakini kama wangalisimama katika baraza yangu, ndipo wangaliwasikizisha watu wangu maneno yangu, na kuwageuza waziache njia zao mbaya, na uovu wa matendo yao.
Zacharie 1.4 Jérémie 25.5 Jérémie 23.18 Jérémie 35.15 Ezéchiel 3.17
23 Mimi ni Mungu aliye karibu, asema Bwana, mimi si Mungu aliye mbali.
Psaumes 139.1-139.10 Jonas 1.3-1.4 Psaumes 113.5 Ezéchiel 20.32-20.35 1 Rois 20.23
24 Je, mtu ye yote aweza kujificha mahali pa siri, nisimwone? Asema Bwana. Je! Mbingu na nchi hazikujawa nami? Asema Bwana.
Proverbes 15.3 1 Rois 8.27 Esaïe 29.15 Psaumes 139.7 Psaumes 90.8
25 Nimesikia waliyoyasema manabii wanaotabiri uongo kwa jina langu, wakisema, Nimeota ndoto; nimeota ndoto.
Joël 2.28 Jérémie 29.8 Jérémie 23.28 Jérémie 23.32 1 Corinthiens 4.5
26 Je! Mambo hayo yatakuwa katika mioyo ya manabii wanaotabiri uongo hata lini, manabii hao wenye udanganyifu katika mioyo yao wenyewe?
1 Timothée 4.1-4.2 Jérémie 14.14 2 Pierre 2.13-2.16 Osée 8.5 2 Timothée 4.3
27 Wanaodhania ya kuwa watawasahaulisha watu wangu jina langu kwa ndoto zao, wanazomhadithia kila mtu jirani yake, kama vile baba zao walivyolisahau jina langu, kwa ajili ya Baali.
Juges 3.7 Juges 8.33-8.34 Actes 13.8 2 Rois 21.3 Jérémie 29.8
28 Nabii aliye na ndoto, na aseme ndoto yake; na yeye aliye na neno langu, na aseme neno langu kwa uaminifu. Makapi ni kitu gani kuliko ngano? Asema Bwana.
1 Corinthiens 3.12-3.13 Proverbes 14.5 Matthieu 24.45 1 Timothée 1.12 Luc 12.42
29 Je! Neno langu si kama moto? Asema Bwana; na kama nyundo ivunjayo mawe vipande vipande?
Jérémie 5.14 Hébreux 4.12 2 Corinthiens 10.4-10.5 Jérémie 20.9 Luc 24.32
30 Basi kwa sababu hiyo mimi ni juu ya manabii hao, asema Bwana, wanaompokonya kila mtu jirani yake maneno yangu.
Deutéronome 18.20 Ezéchiel 13.8 Jérémie 14.14-14.15 Psaumes 34.16 Ezéchiel 13.20
31 Tazama, mimi ni juu ya manabii, asema Bwana, wanaotumia ndimi zao na kusema, Yeye asema,
Jérémie 23.17 Michée 2.11 2 Chroniques 18.19-18.21 2 Chroniques 18.10-18.12 Esaïe 30.10
32 Tazama, mimi ni juu ya hao wanaotabiri ndoto za uongo, asema Bwana, na kuzisema, na kuwakosesha watu wangu kwa uongo wao, na kwa majivuno yao ya upuzi, lakini mimi sikuwatuma, wala sikuwapa amri; wala hawatawafaidia watu hawa hata kidogo, asema Bwana.
Jérémie 7.8 Lamentations 2.14 Sophonie 3.4 Jérémie 23.16 Jérémie 27.14-27.22
33 Na watu hawa, au nabii au kuhani, atakapokuuliza, akisema, Mzigo wa Bwana ni nini? Ndipo utawaambia, Mzigo gani? Bwana asema, Nitawatupilia mbali.
Malachie 1.1 Nahum 1.1 Habakuk 1.1 Jérémie 12.7 Esaïe 13.1
34 Na katika habari ya nabii, na kuhani, na watu, watakaosema, Mzigo wa Bwana, mimi nitamwadhibu mtu yule, na nyumba yake.
Zacharie 13.3 Lamentations 2.14
35 Mtasema hivi kila mtu na jirani yake, na kila mtu na ndugu yake, Bwana amejibu mtu? Na, Bwana amesemaje?
Jérémie 42.4 Hébreux 8.11 Jérémie 31.34 Jérémie 33.3
36 Na mzigo wa Bwana hamtautaja tena; maana neno la kila mtu ndilo litakalokuwa mzigo wake; maana ninyi mmeyapotosha maneno ya Mungu aliye hai, ya Bwana wa majeshi, Mungu wetu.
2 Pierre 3.16 Jérémie 10.10 2 Rois 19.4 Galates 1.7-1.9 Psaumes 149.9
37 Nawe utamwambia nabii hivi, Bwana amekujibu nini? Na, Bwana amesemaje?
38 Lakini mkisema, Mzigo wa Bwana, basi, Bwana asema hivi, Kwa sababu mwasema neno hili, (Mzigo wa Bwana); nami nimemtuma mtu kwenu kusema, Msiseme, (Mzigo wa Bwana);
2 Chroniques 11.13-11.14
39 basi, kwa hiyo angalieni, nitawasahau ninyi kabisa, nami nitawatupilia mbali, pamoja na mji huu niliowapa ninyi na baba zenu, mtoke mbele za uso wangu;
Jérémie 23.33 Ezéchiel 8.18 Genèse 6.17 Lévitique 26.28 Jérémie 52.3
40 nami nitaleta juu yenu aibu ya milele, na fedheha ya daima, ambayo haitasahauliwa.
Jérémie 20.11 Ezéchiel 5.14-5.15 Jérémie 42.18 Daniel 12.2 Daniel 9.16

Cette Bible est dans le domaine public.