Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Proverbes 12.7
Bible en Swahili de l’est


1 Kila apendaye mafundisho hupenda maarifa; Bali yeye achukiaye kulaumiwa ni kama mnyama.
Proverbes 15.10 Psaumes 119.97-119.100 2 Thessaloniciens 2.10 Psaumes 32.9 Proverbes 9.7-9.8
2 Mtu mwema atapata upendeleo kwa Bwana; Bali mtu wa hila atahukumiwa naye.
Proverbes 8.35 Ecclésiaste 8.8 Actes 11.24 Proverbes 6.18 Esaïe 32.5-32.7
3 Mtu hatathibitika kwa njia ya uovu; Shina la mwenye haki halitaondolewa kamwe.
Proverbes 10.25 Colossiens 2.7 Psaumes 15.5 1 Samuel 25.33 Job 5.3-5.5
4 Mwanamke mwema ni taji ya mumewe; Bali aaibishaye ni kama kuoza mifupani mwake.
Proverbes 14.30 Proverbes 14.1 Habakuk 3.16 Proverbes 21.9 Proverbes 27.15-27.16
5 Mawazo ya mwenye haki ni adili; Bali mashauri ya mtu mwovu ni hadaa.
Psaumes 139.23 1 Corinthiens 4.5 Proverbes 11.23 2 Corinthiens 4.2 Matthieu 2.3-2.8
6 Maneno ya waovu huotea damu; Bali kinywa cha wanyofu kitawaokoa.
Proverbes 14.3 2 Samuel 17.1-17.4 Jérémie 5.26 Esther 7.4-7.6 Esther 4.7-4.14
7 Waovu huangamia, hata hawako tena; Bali nyumba ya mwenye haki itasimama.
Proverbes 10.25 Matthieu 7.24-7.27 Proverbes 11.21 Proverbes 14.11 Job 27.18-27.23
8 Mtu atasifiwa kwa kadiri ya akili zake; Bali mwenye moyo wa ukaidi atadharauliwa.
1 Samuel 13.13 Luc 16.8 Proverbes 1.26 Luc 12.42-12.44 2 Corinthiens 10.18
9 Afadhali mtu anayedharauliwa, ikiwa ana mtumwa, Kuliko ajisifuye, ikiwa anahitaji chakula.
Luc 14.11 Proverbes 13.7
10 Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake; Bali huruma za mtu mwovu ni ukatili.
Deutéronome 25.4 1 Jean 3.17 Jean 4.11 Jacques 2.13-2.16 Jean 19.31-19.32
11 Alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele; Bali afuataye mambo ya upuzi hana ufahamu.
Proverbes 28.19 1 Thessaloniciens 4.11-4.12 Proverbes 14.23 2 Thessaloniciens 3.8 Proverbes 14.4
12 Asiye haki hutamani nyavu za wabaya; Bali shina lao wenye haki huleta matunda.
Psaumes 10.9 Proverbes 10.15 Michée 7.2 Jean 15.5 Habakuk 1.15-1.17
13 Katika kosa la midomo kuna mtego kwa mbaya; Bali mwenye haki atatoka katika taabu.
2 Pierre 2.9 Proverbes 11.8 Psaumes 64.8 Proverbes 21.23 Psaumes 5.6
14 Mtu atashiba mema kwa matunda ya kinywa chake; Na atarudishiwa matendo ya mikono yake.
Esaïe 3.10-3.11 Proverbes 13.2 Hébreux 2.2 2 Thessaloniciens 1.6-1.7 Psaumes 63.5

Le fou et le sage

15 Njia ya mpumbavu imenyoka machoni pake mwenyewe; Bali yeye aliye na hekima husikiliza shauri.
Proverbes 3.7 Proverbes 19.20 Proverbes 16.2 Proverbes 14.12 Proverbes 1.5
16 Ghadhabu ya mpumbavu hujulika mara; Bali mtu mwerevu husitiri aibu.
Proverbes 29.11 Jacques 1.19 Proverbes 10.12 Proverbes 17.9 Proverbes 25.28
17 Atamkaye maneno ya kweli hufunua haki; Bali shahidi wa uongo hutamka hila.
Proverbes 14.5 Proverbes 14.25 Proverbes 6.19 1 Samuel 22.14-22.15 Matthieu 26.59
18 Kuna anenaye bila kufikiri, kama kuchoma kwa upanga; Bali ulimi wa mwenye haki ni afya.
Proverbes 16.24 Psaumes 57.4 Proverbes 4.22 Proverbes 15.4 Jacques 3.6-3.8
19 Mdomo wa kweli utathibitishwa milele; Bali ulimi wa uongo ni wa kitambo tu.
Proverbes 19.9 Actes 5.3-5.10 Matthieu 24.35 Zacharie 1.4-1.6 Job 20.5
20 Hila imo mioyoni mwao wafikirio uovu; Bali wafanyao mashauri ya amani, kwao kuna furaha.
Romains 1.29 Zacharie 6.13 Marc 12.14-12.17 Hébreux 12.14 Esaïe 9.6-9.7
21 Mwenye haki hatapatikana na msiba wo wote; Bali wasio haki watajazwa mabaya.
1 Pierre 3.13 Apocalypse 18.6 Psaumes 91.10 Jérémie 13.12-13.14 Habakuk 2.16
22 Midomo ya uongo ni chukizo kwa Bwana; Bali watendao uaminifu ndio furaha yake.
Apocalypse 22.15 Proverbes 11.20 Proverbes 6.16-6.17 Psaumes 5.6 Proverbes 11.1
23 Mwanadamu mwenye busara husitiri maarifa; Bali moyo wa wapumbavu hutangaza upumbavu.
Proverbes 13.16 Proverbes 15.2 Proverbes 11.13 Ecclésiaste 10.12-10.14 Proverbes 10.19
24 Mkono wa mwenye bidii utatawala; Bali mvivu atalipishwa kodi.
Proverbes 21.25-21.26 Proverbes 10.4 Proverbes 12.27 Genèse 49.15 Proverbes 17.2
25 Uzito katika moyo wa mtu huuinamisha; Bali neno jema huufurahisha.
Proverbes 15.13 Proverbes 15.23 Esaïe 50.4 Proverbes 16.24 Proverbes 17.22
26 Mwenye haki ni kiongozi cha mwenzake; Bali njia ya wasio haki huwakosesha.
Jacques 1.13-1.14 1 Jean 2.26 1 Pierre 2.18-2.21 Apocalypse 13.14 Luc 6.32-6.36
27 Mtu mvivu hapiki mawindo yake; Bali mwenye bidii anazo mali za thamani.
Proverbes 13.4 Proverbes 23.2 Proverbes 15.16 Psaumes 37.16 Proverbes 26.15
28 Katika njia ya haki kuna uhai; Wala hakuna mauti katika mapito yake.
3 Jean 1.11 Romains 6.22-6.23 Tite 2.11-2.12 1 Jean 3.7 Proverbes 8.35

Cette Bible est dans le domaine public.