Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Exode 23.22
Bible en Swahili de l’est


Règles morales

1 Usivumishe habari za uongo; usitie mkono wako pamoja na mwovu, kuwa shahidi wa udhalimu.
Psaumes 101.5 Exode 20.16 Psaumes 35.11 Proverbes 19.5 Lévitique 19.11
2 Usiandamane na mkutano kutenda uovu; wala usitie ushahidi wako katika neno lo lote kwa kugeukia kando na kuandamana na mkutano ili kupotoa hukumu;
Exode 32.1-32.5 Proverbes 1.15 Proverbes 1.10-1.11 Lévitique 19.15 Josué 24.15
3 wala usimpendelee mtu mnyonge katika neno lake.
Psaumes 82.2-82.3 Jacques 3.17 Deutéronome 1.17 Lévitique 19.15
4 Ukimwona ng’ombe wa adui wako, au punda wake, amepotea, sharti umrudishie mwenyewe tena.
Deutéronome 22.1-22.4 Matthieu 5.44 1 Thessaloniciens 5.15 Proverbes 25.21 Luc 6.27-6.28
5 Ukimwona punda wake huyo akuchukiaye hali ameanguka chini ya mzigo wake, nawe ungejizuia usimsaidie, lazima umsaidie.
Deutéronome 22.4
6 Usipotoe hukumu ya mtu maskini katika neno lake.
Esaïe 10.1-10.2 Malachie 3.5 Exode 23.2-23.3 Deutéronome 16.19 Jérémie 5.28
7 Jitenge mbali na neno uongo; wala wasio hatia na wenye haki usiwaue; kwa kuwa mimi sitamhesabia haki yeye aliye mwovu.
Exode 34.7 Exode 23.1 Ephésiens 4.25 Deutéronome 27.25 Lévitique 19.11
8 Nawe usipokee rushwa; kwani hiyo rushwa huwapofusha macho hao waonao, na kuyapotoa maneno ya wenye haki.
Deutéronome 16.19 Proverbes 17.23 Proverbes 15.27 Esaïe 5.23 1 Samuel 8.3
9 Usimwonee mgeni; maana, ninyi mwajua moyo wa mgeni ulivyo, kwa kuwa ninyi mlikuwa wageni katika nchi ya Misri.
Deutéronome 27.19 Exode 22.21 Deutéronome 10.19 Hébreux 2.17-2.18 Matthieu 18.33

Les fêtes et le sabbat

10 Utapanda mbegu katika nchi yako muda wa miaka sita na kuyavuna maongeo yake;
Lévitique 25.3-25.4
11 lakini mwaka wa saba utaiacha nchi ipumzike na kutulia; hao maskini miongoni mwa watu wako wapate kula; na hicho watakachosaza wao, wapate kula wanyama wa kondeni. Utafanya vivyo katika shamba lako la mizabibu, na katika shamba lako la mizeituni.
Lévitique 25.11-25.12 Lévitique 25.22 Lévitique 26.34-26.35 Lévitique 25.2-25.7 Lévitique 25.20
12 Siku sita utafanya kazi yako, na siku ya saba utapumzika; ili kwamba ng’ombe wako na punda wako wapate kupumzika, kisha mwana wa mjakazi wako na mgeni wapate kuburudika.
Exode 20.8-20.11 Luc 13.14 Deutéronome 5.13-5.15 Exode 31.15-31.16 Exode 35.3
13 Yaangalieni hayo yote niliyowaambia; wala msitaje kabisa majina ya miungu mingine, wala yasisikizwe kutoka kinywani mwako.
1 Timothée 4.16 Deutéronome 4.9 Osée 2.17 Josué 23.7 Psaumes 16.4
14 Mara tatu kila mwaka utaniwekea sikukuu.
Deutéronome 16.16 Lévitique 23.16 Lévitique 23.5 Exode 34.22-34.24 Lévitique 23.34
15 Utaiweka sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu; utakula mikate isiyochachwa muda wa siku saba kama nilivyokuagiza, kwa wakati uliowekwa, mwezi wa Abibu (kwa maana ndio mwezi uliotoka Misri); wala hapana mtu atakayeonekana mbele yangu na mikono mitupu;
Exode 34.20 Nombres 28.16-28.25 Deutéronome 16.16 Lévitique 23.10 Exode 34.18
16 tena, sikukuu ya mavuno, hayo malimbuko ya kazi zako za kupanda mashambani; tena, sikukuu ya kukusanya, mwisho wa mwaka, hapo utakapokusanya hayo uliyoyataabikia shambani.
Exode 34.22 Lévitique 23.34-23.44 Lévitique 23.9-23.21 Zacharie 14.16-14.19 Actes 2.1
17 Mara tatu katika mwaka watu waume wako wote watahudhuria mbele ya Bwana MUNGU.
Deutéronome 16.16 Exode 34.23 Exode 23.14 Deutéronome 12.5 Luc 2.42
18 Usisongeze damu ya dhabihu zangu pamoja na mkate uliotiwa chachu, wala mafuta ya sikukuu yangu usiyaache kusalia hata asubuhi.
Exode 34.25 Lévitique 2.11 Deutéronome 16.4 Exode 12.8 Exode 12.10
19 Ya kwanza ya malimbuko ya nchi yako utayaleta na kuyatia ndani ya nyumba ya Bwana, Mungu wako. Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.
Exode 34.26 Deutéronome 14.21 Deutéronome 26.10 Exode 22.29 Néhémie 10.35

Instructions et promesses pour la conquête

20 Tazama, mimi namtuma malaika aende mbele yako, ili akulinde njiani na kukupeleka mpaka mahali pale nilipokutengezea.
Exode 14.19 Exode 32.34 Exode 33.14 Exode 33.2 Esaïe 63.9
21 Jitunzeni mbele yake, mwisikize sauti yake; wala msimtie kasirani; maana, hatawasamehe makosa yenu; kwa kuwa jina langu limo ndani yake.
Psaumes 78.40 Psaumes 78.56 Exode 3.14 Hébreux 12.25 Josué 24.19
22 Lakini ukiisikiza sauti yake kweli, na kuyatenda yote ninenayo mimi; ndipo mimi nitakuwa ni adui wa adui zako, na mtesi wa hao wakutesao.
Genèse 12.3 Deutéronome 30.7 Nombres 24.9 Jérémie 30.20 Actes 9.4-9.5
23 Kwa kuwa malaika wangu atatangulia mbele yako, na kukufikisha kwenye Mwamori, na Mhiti, na Mperizi, na Mkanaani, na Mhivi, na Myebusi; nami nitawakatilia mbali.
Exode 23.20 Josué 24.8-24.11 Exode 32.2 Genèse 34.2 Esaïe 5.13
24 Usiisujudie miungu yao, wala kuitumikia; wala usitende mfano wa matendo yao; bali utaiangamiza kabisa, na nguzo zao utazivunja vipande vipande.
Exode 20.5 Nombres 33.52 Deutéronome 12.3 Deutéronome 7.5 Deutéronome 12.30-12.31
25 Nanyi mtamtumikia Bwana, Mungu wenu, naye atakibarikia chakula chako, na maji yako; nami nitakuondolea ugonjwa kati yako.
Deutéronome 7.15 Deutéronome 6.13 Deutéronome 7.13 Deutéronome 10.12 Josué 22.5
26 Hapatakuwa na mwenye kuharibu mimba, wala aliye tasa, katika nchi yako; na hesabu ya siku zako nitaitimiza.
Deutéronome 7.14 Job 5.26 Psaumes 55.23 Psaumes 107.38 Psaumes 90.10
27 Nitatuma utisho wangu utangulie mbele yako, nami nitawafadhaisha watu wote utakaowafikilia, nami nitawafanya hao adui zako wote wakuonyeshe maungo yao.
Deutéronome 2.25 Deutéronome 7.23 Genèse 35.5 Psaumes 18.40 Josué 2.9-2.11
28 Nami nitapeleka mavu mbele yako, watakaomfukuza Mhivi, na Mkanaani, na Mhiti, watoke mbele yako.
Deutéronome 7.20 Josué 24.11-24.12
29 Sitawafukuza mbele yako katika mwaka mmoja; nchi isiwe ukiwa, na wanyama wa bara wakaongezeka kukusumbua.
Deutéronome 7.22 Juges 3.1-3.4 Josué 15.63 Josué 17.12-17.13 Josué 16.10
30 Nitawafukuza kidogo kidogo mbele yako, hata utakapoongezeka wewe, na kuirithi hiyo nchi.
31 Nami nitakuwekea mpaka wako tangu Bahari ya Shamu hata bahari ya Wafilisti, tena tangu jangwani hata huo Mto; kwa kuwa nitawatia wenyeji wa nchi mkononi mwako; nawe utawafukuza mbele yako.
Genèse 15.18 Josué 21.44 Deutéronome 11.24 Josué 1.4 Nombres 34.3-34.15
32 Usifanye maagano pamoja nao, wala pamoja na miungu yao.
Exode 34.12 Deutéronome 7.2 Exode 34.15 Deutéronome 7.16 2 Corinthiens 6.15
33 Wasikae katika nchi yako, wasije wakakufanya kunitendea mimi dhambi; kwa sababu ukiitumikia miungu yao, jambo hili halikosi litakuwa ni tanzi kwako.
Deutéronome 7.16 Psaumes 106.36 Exode 34.12 Juges 2.3 Josué 23.13

Cette Bible est dans le domaine public.