Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 9.9
Bible en Swahili de l’est


Le jugement de Dieu sur les nations

1 Nitamshukuru Bwana kwa moyo wangu wote; Nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu;
Psaumes 86.12 Psaumes 145.1-145.3 Psaumes 111.1 Psaumes 138.1 Psaumes 146.1-146.2
2 Nitafurahi na kukushangilia Wewe; Nitaliimbia jina lako, Wewe Uliye juu.
Psaumes 5.11 Psaumes 83.18 Psaumes 92.1 Psaumes 7.17 Psaumes 43.4
3 Kwa sababu adui zangu hurudi nyuma; Hujikwaa na kuangamia mbele zako.
Psaumes 68.1-68.2 2 Thessaloniciens 1.9 Psaumes 76.7 Psaumes 80.16 Esaïe 64.3
4 Kwa maana umenifanyia hukumu na haki Umeketi kitini pa enzi ukihukumu kwa haki.
Psaumes 140.12 1 Pierre 2.23 Esaïe 11.4 Psaumes 98.9 Psaumes 47.8
5 Umewakemea mataifa; Na kumwangamiza mdhalimu; Umelifuta jina lao milele na milele;
Proverbes 10.7 Deutéronome 9.14 1 Samuel 17.45-17.51 2 Samuel 22.44-22.46 Apocalypse 19.15
6 Adui wamekoma na kuachwa ukiwa milele. Nayo miji yao uliing’oa; Hata kumbukumbu lao limepotea.
Exode 14.13 1 Samuel 30.1 1 Samuel 31.7 Esaïe 37.26 Esaïe 14.17
7 Bali Bwana atakaa milele, Ameweka kiti chake tayari kwa hukumu.
Apocalypse 20.11 Hébreux 13.8 2 Pierre 3.8 Psaumes 89.14 Psaumes 103.19
8 Naye atauhukumu ulimwengu kwa haki; Atawaamua watu kwa adili.
Psaumes 96.13 Psaumes 98.9 Apocalypse 20.12-20.13 Actes 17.31 Psaumes 50.6
9 Bwana atakuwa ngome kwake aliyeonewa, Naam, ngome kwa nyakati za shida.
Proverbes 18.10 Psaumes 32.7 Psaumes 91.1-91.2 Hébreux 6.18 Esaïe 32.2
10 Nao wakujuao jina lako wakutumaini Wewe, Maana Wewe, Bwana hukuwaacha wakutafutao.
Psaumes 91.14 2 Corinthiens 1.9-1.10 2 Timothée 1.12 1 Jean 5.20 Proverbes 18.10
11 Mwimbieni Bwana akaaye Sayuni, Yatangazeni kati ya watu matendo yake.
Psaumes 107.22 Psaumes 76.2 Psaumes 66.2 Psaumes 105.1-105.2 Psaumes 148.1-148.5
12 Maana mlipiza kisasi cha damu awakumbuka, Hakukisahau kilio cha wanyonge.
Genèse 9.5 Exode 3.7 Psaumes 34.6 Psaumes 22.24 Psaumes 10.14
13 Wewe, Bwana, unifadhili, Tazama mateso niteswayo na wanaonichukia; Wewe uniinuaye katika malango ya mauti,
Psaumes 30.3 Psaumes 86.13 Jean 2.6 Psaumes 38.19 Psaumes 116.3-116.4
14 Ili nizisimulie sifa zako zote; Katika malango ya binti Sayuni Nitaufurahia wokovu wako.
Psaumes 13.5 Psaumes 35.9 Psaumes 106.2 Psaumes 51.12 Psaumes 20.5
15 Mataifa wamezama katika shimo walilolifanya; Kwa wavu waliouficha imenaswa miguu yao.
Psaumes 57.6 Psaumes 7.15-7.16 Psaumes 35.8 Proverbes 5.22 Psaumes 37.15
16 Bwana amejidhihirisha na kutekeleza hukumu; Amemnasa mdhalimu kwa kazi ya mikono yake.
Exode 7.5 Exode 14.4 Proverbes 12.13 2 Rois 19.34-19.35 Deutéronome 29.22-29.28
17 Wadhalimu watarejea kuzimu, Naam, mataifa yote wanaomsahau Mungu.
Psaumes 50.22 Job 8.13 2 Thessaloniciens 1.7-1.9 Romains 2.8-2.9 Esaïe 5.14
18 Kwa maana mhitaji hatasahauliwa daima; Matumaini ya wanyonge hayatapotea milele.
Proverbes 23.18 Psaumes 12.5 Psaumes 9.12 Proverbes 24.14 Psaumes 72.4
19 Bwana, usimame, mwanadamu asipate nguvu, Mataifa wahukumiwe mbele zako.
Psaumes 3.7 Esaïe 51.9 Joël 3.12 Jérémie 10.25 Zacharie 14.18
20 Bwana, uwawekee kitisho, Mataifa na wajijue kuwa ni binadamu.
Esaïe 31.3 Psaumes 76.12 Ezéchiel 30.13 Ezéchiel 28.2 Exode 15.16

Cette Bible est dans le domaine public.