Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 9.12
Bible en Swahili de l’est


Le jugement de Dieu sur les nations

1 Nitamshukuru Bwana kwa moyo wangu wote; Nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu;
Psaumes 86.12 Psaumes 145.1-145.3 Psaumes 111.1 Psaumes 138.1 Psaumes 146.1-146.2
2 Nitafurahi na kukushangilia Wewe; Nitaliimbia jina lako, Wewe Uliye juu.
Psaumes 83.18 Psaumes 5.11 Psaumes 92.1 Psaumes 7.17 Habakuk 3.17-3.18
3 Kwa sababu adui zangu hurudi nyuma; Hujikwaa na kuangamia mbele zako.
Psaumes 80.16 Esaïe 64.3 Apocalypse 6.12-6.17 Apocalypse 20.11 Psaumes 68.1-68.2
4 Kwa maana umenifanyia hukumu na haki Umeketi kitini pa enzi ukihukumu kwa haki.
Psaumes 140.12 1 Pierre 2.23 Psaumes 98.9 Psaumes 47.8 Psaumes 45.6-45.7
5 Umewakemea mataifa; Na kumwangamiza mdhalimu; Umelifuta jina lao milele na milele;
Proverbes 10.7 Deutéronome 9.14 Psaumes 5.6 Malachie 4.3 2 Samuel 8.1-8.15
6 Adui wamekoma na kuachwa ukiwa milele. Nayo miji yao uliing’oa; Hata kumbukumbu lao limepotea.
Esaïe 10.13-10.14 Psaumes 7.5 Exode 15.16 1 Corinthiens 15.54-15.57 Michée 7.10
7 Bali Bwana atakaa milele, Ameweka kiti chake tayari kwa hukumu.
Psaumes 89.14 Psaumes 103.19 Psaumes 90.2 Psaumes 102.12 Hébreux 1.11-1.12
8 Naye atauhukumu ulimwengu kwa haki; Atawaamua watu kwa adili.
Psaumes 96.13 Psaumes 98.9 Psaumes 50.6 Romains 2.16 Romains 2.5-2.6
9 Bwana atakuwa ngome kwake aliyeonewa, Naam, ngome kwa nyakati za shida.
Psaumes 32.7 Proverbes 18.10 Psaumes 91.1-91.2 Hébreux 6.18 Esaïe 4.5-4.6
10 Nao wakujuao jina lako wakutumaini Wewe, Maana Wewe, Bwana hukuwaacha wakutafutao.
Psaumes 91.14 2 Corinthiens 1.9-1.10 2 Timothée 1.12 Proverbes 18.10 Esaïe 26.3-26.4
11 Mwimbieni Bwana akaaye Sayuni, Yatangazeni kati ya watu matendo yake.
Psaumes 107.22 Psaumes 76.2 Apocalypse 14.1 Jean 17.26 Psaumes 96.10
12 Maana mlipiza kisasi cha damu awakumbuka, Hakukisahau kilio cha wanyonge.
Genèse 9.5 Psaumes 34.6 Exode 3.7 Psaumes 102.17 Apocalypse 16.6
13 Wewe, Bwana, unifadhili, Tazama mateso niteswayo na wanaonichukia; Wewe uniinuaye katika malango ya mauti,
Psaumes 30.3 Psaumes 86.13 Psaumes 107.18 Psaumes 142.6 Esaïe 38.10
14 Ili nizisimulie sifa zako zote; Katika malango ya binti Sayuni Nitaufurahia wokovu wako.
Psaumes 13.5 Psaumes 106.2 Psaumes 51.12 Psaumes 20.5 Psaumes 35.9
15 Mataifa wamezama katika shimo walilolifanya; Kwa wavu waliouficha imenaswa miguu yao.
Psaumes 57.6 Psaumes 7.15-7.16 Psaumes 35.8 Proverbes 5.22 Psaumes 37.15
16 Bwana amejidhihirisha na kutekeleza hukumu; Amemnasa mdhalimu kwa kazi ya mikono yake.
Exode 7.5 Proverbes 12.13 Exode 14.4 Juges 1.7 Psaumes 19.14
17 Wadhalimu watarejea kuzimu, Naam, mataifa yote wanaomsahau Mungu.
Job 8.13 Psaumes 50.22 2 Thessaloniciens 1.7-1.9 Romains 2.8-2.9 Esaïe 5.14
18 Kwa maana mhitaji hatasahauliwa daima; Matumaini ya wanyonge hayatapotea milele.
Proverbes 23.18 Psaumes 12.5 Psaumes 9.12 Proverbes 24.14 Jacques 2.5
19 Bwana, usimame, mwanadamu asipate nguvu, Mataifa wahukumiwe mbele zako.
Psaumes 3.7 Genèse 32.28 Psaumes 44.23 2 Chroniques 14.11 Psaumes 44.26
20 Bwana, uwawekee kitisho, Mataifa na wajijue kuwa ni binadamu.
Esaïe 31.3 Ezéchiel 28.2 Exode 15.16 Exode 23.27 Deutéronome 2.25

Cette Bible est dans le domaine public.