Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 74.11
Bible en Swahili de l’est


Supplication après la destruction du temple

1 Ee Mungu, mbona umetutupa milele? Kwa nini hasira yako inatoka moshi Juu ya kondoo wa malisho yako?
Psaumes 79.13 Psaumes 100.3 Deutéronome 29.20 Psaumes 95.7 Psaumes 44.9
2 Ulikumbuke kusanyiko lako, Ulilolinunua zamani. Ulilolikomboa liwe kabila ya urithi wako, Mlima Sayuni ulioufanya maskani yako.
Exode 15.16 Jérémie 10.16 Deutéronome 32.9 Esaïe 51.11 Psaumes 33.12
3 Upainulie miguu yako palipoharibika milele; Adui ameufanya kila ubaya katika patakatifu.
Psaumes 79.1 Michée 3.12 Josué 10.24 Esaïe 61.4 Daniel 9.27
4 Watesi wako wamenguruma kati ya kusanyiko lako; Wameweka bendera zao ziwe alama.
Lamentations 2.7 Nombres 2.2 Matthieu 24.15 Luc 13.1 Jérémie 6.1-6.5
5 Wanaonekana kama watu wainuao mashoka, Waikate miti ya msituni.
Jérémie 46.22-46.23 2 Chroniques 2.14 1 Rois 5.6
6 Na sasa nakishi yake yote pia Wanaivunja-vunja kwa mashoka na nyundo.
1 Rois 6.18 1 Rois 6.32 1 Rois 6.35 1 Rois 6.29
7 Wamepatia moto patakatifu pako; Wamelinajisi kao la jina lako hata chini.
2 Rois 25.9 Psaumes 89.39 Esaïe 64.11 Lamentations 2.2 1 Rois 8.20
8 Walisema mioyoni mwao, Na tuwaangamize kabisa; Mahali penye mikutano ya Mungu Wamepachoma moto katika nchi pia.
Psaumes 83.4 Esther 3.8-3.9 2 Rois 4.23 Matthieu 4.23 2 Rois 2.3
9 Hatuzioni ishara zetu, wala sasa hakuna nabii, Wala kwetu hakuna ajuaye, hata lini?
1 Samuel 3.1 Amos 8.11 Exode 13.9-13.10 Ezéchiel 20.12 Lamentations 2.9
10 Ee Mungu, mtesi atalaumu hata lini? Adui alidharau jina lako hata milele?
Psaumes 79.4-79.5 Psaumes 79.12 Psaumes 44.16 Psaumes 13.1-13.2 Daniel 12.6
11 Mbona unaurudisha mkono wako, Naam, mkono wako wa kuume, Uutoe kifuani mwako, Ukawaangamize kabisa.
Lamentations 2.3 Psaumes 78.65-78.66 Psaumes 44.23 Esaïe 64.12
12 Lakini Mungu ni mfalme wangu tokea zamani, Afanyaye mambo ya wokovu katikati ya nchi.
Psaumes 44.4 Exode 15.2-15.15 Exode 19.5-19.6 Habakuk 3.12-3.14 Juges 4.23-4.24
13 Wewe umeipasua bahari kwa nguvu zako, Umevivunja vichwa vya nyangumi juu ya maji.
Exode 14.21 Ezéchiel 29.3 Psaumes 78.13 Esaïe 51.9-51.10 Psaumes 66.6
14 Wewe uliviseta vichwa vya lewiathani, Awe chakula cha watu wa jangwani.
Esaïe 27.1 Job 41.1-41.34 Psaumes 104.25-104.26 Exode 14.30 Exode 12.35-12.36
15 Wewe ulitokeza chemchemi na kijito; Wewe ulikausha mito yenye maji sikuzote.
Nombres 20.11 Esaïe 48.21 Exode 17.5-17.6 Psaumes 105.41 Josué 2.10
16 Mchana ni wako, usiku nao ni wako, Ndiwe uliyeufanya mwanga na jua.
Psaumes 136.7-136.9 Genèse 1.14-1.18 Psaumes 19.1-19.6 Psaumes 104.19 Genèse 1.3-1.5
17 Wewe uliiweka mipaka yote ya dunia, Kaskazi na kusi Wewe ulizitengeneza.
Deutéronome 32.8 Actes 17.26 Genèse 8.22 Psaumes 24.1-24.2 Actes 14.17
18 Ee Bwana, uyakumbuke hayo, adui amelaumu, Na watu wapumbavu wamelidharau jina lako.
Psaumes 39.8 Apocalypse 16.19 Deutéronome 32.6 Psaumes 94.2-94.8 Esaïe 37.23-37.24
19 Usimpe mnyama mkali nafsi ya hua wako; Usiusahau milele uhai wa watu wako walioonewa.
Cantique 2.14 Psaumes 68.10 Psaumes 9.18 Psaumes 72.2 Psaumes 68.13
20 Ulitafakari agano; Maana mahali penye giza katika nchi Pamejaa makao ya ukatili.
Psaumes 106.45 Genèse 17.7-17.8 Hébreux 8.10 Deutéronome 9.27 Luc 1.72-1.75
21 Aliyeonewa asirejee ametiwa haya, Mnyonge na mhitaji na walisifu jina lako.
Jérémie 33.11 Psaumes 12.5 Esaïe 45.17 Psaumes 109.22 Psaumes 35.10
22 Ee Mungu, usimame, ujitetee mwenyewe, Ukumbuke unavyotukanwa na mpumbavu mchana kutwa.
Psaumes 74.18 Psaumes 53.1 Psaumes 75.4-75.5 Psaumes 79.9-79.10 Psaumes 89.50-89.51
23 Usiisahau sauti ya watesi wako, Ghasia yao wanaokuondokea inapaa daima.
Psaumes 65.7 Esaïe 37.29 Psaumes 13.1 Lamentations 2.16 Psaumes 10.11-10.12

Cette Bible est dans le domaine public.