Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 65.10
Bible en Swahili de l’est


Louange à Dieu pour ses bienfaits

1 Ee Mungu, sifa zakulaiki katika Sayuni, Na kwako Wewe itaondolewa nadhiri.
Psaumes 62.1 Psaumes 76.11 Psaumes 116.17-116.18 1 Chroniques 11.7 1 Chroniques 16.41-16.42
2 Wewe usikiaye kuomba, Wote wenye mwili watakujia.
Esaïe 66.23 Psaumes 86.9 Jérémie 29.12-29.13 Psaumes 66.4 Daniel 9.17-9.19
3 Ingawa maovu mengi yanamshinda, Wewe utayafunika maasi yetu.
Psaumes 38.4 Psaumes 79.9 Esaïe 6.7 Hébreux 9.14 Psaumes 40.12
4 Heri mtu yule umchaguaye, Na kumkaribisha akae nyuani mwako. Na tushibe wema wa nyumba yako, Patakatifu pa hekalu lako.
Psaumes 36.8 Psaumes 33.12 Psaumes 84.4 Psaumes 63.5 Psaumes 4.3
5 Kwa mambo ya kutisha utatujibu, Katika haki, Ee Mungu wa wokovu wetu. Wewe uliye tumaini la miisho yote ya dunia, Na la bahari iliyo mbali sana,
Psaumes 45.4 Psaumes 22.27 Psaumes 66.3 Deutéronome 10.21 Zacharie 9.10
6 Milima waiweka imara kwa nguvu zako, Huku ukijifunga uweza kama mshipi.
Psaumes 93.1 Michée 6.2 1 Samuel 2.4 Psaumes 119.90 Esaïe 51.9
7 Wautuliza uvumi wa bahari, Uvumi wa mawimbi yake, Na ghasia ya mataifa;
Esaïe 17.12-17.13 Psaumes 89.9 Psaumes 107.29 Psaumes 93.3-93.4 Jean 18.6
8 Kwa hiyo wakaao mbali kabisa huogopa ishara zako; Milango ya asubuhi na jioni waifurahisha.
Psaumes 2.8 Psaumes 19.5 Psaumes 104.20-104.23 Apocalypse 11.13 Josué 2.9-2.11
9 Umeijilia nchi na kuisitawisha, Umeitajirisha sana; Mto wa Mungu umejaa maji; Wawaruzuku watu nafaka Maana ndiwe uitengenezaye ardhi.
Psaumes 46.4 Psaumes 104.13-104.15 Psaumes 68.9-68.10 Jérémie 5.24 Lévitique 26.4
10 Matuta yake wayajaza maji; Wapasawazisha palipoinuka, Wailainisha nchi kwa manyunyu; Waibariki mimea yake.
Psaumes 147.8 1 Corinthiens 3.6-3.7 Deutéronome 32.2
11 Umeuvika mwaka taji ya wema wako; Mapito yako yadondoza unono.
Joël 2.21-2.26 Job 36.28 Psaumes 104.3 Aggée 2.19 Psaumes 103.4
12 Huyadondokea malisho ya nyikani, Na vilima vyajifunga furaha.
Job 38.26-38.27 Psaumes 104.10-104.13 Joël 2.22 Esaïe 55.9-55.13 Psaumes 65.6
13 Na malisho yamevikwa kondoo, Na mabonde yamepambwa nafaka, Yanashangilia, naam, yanaimba.
Esaïe 55.12 Esaïe 44.23 Esaïe 35.1-35.2 Psaumes 144.13 Jérémie 48.33

Cette Bible est dans le domaine public.