1 Moyo wangu umefurika kwa neno jema, Mimi nasema niliyomfanyizia mfalme; Ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi mstadi.
2 Samuel 23.2  Job 33.3  Cantique 1.12  Esdras 7.6  Psaumes 49.3  
 2 Wewe u mzuri sana kuliko wanadamu; Neema imemiminiwa midomoni mwako, Kwa hiyo Mungu amekubariki hata milele.
Luc 4.22  Psaumes 21.6  Esaïe 50.4  Hébreux 1.3-1.4  Zacharie 9.17  
 3 Jifungie upanga wako pajani, wewe uliye hodari, Utukufu ni wako na fahari ni yako.
Apocalypse 1.16  Hébreux 4.12  Esaïe 49.2  Psaumes 21.5  Psaumes 96.6  
 4 Katika fahari yako usitawi uendelee Kwa ajili ya kweli na upole na haki Na mkono wako wa kuume Utakufundisha mambo ya kutisha.
Apocalypse 6.2  Psaumes 110.2-110.3  Psaumes 65.5  1 Thessaloniciens 2.13  1 Thessaloniciens 1.5  
 5 Mishale yako ni mikali, watu huanguka chini yako; Imo mioyoni mwa adui za mfalme.
Psaumes 38.2  Nombres 24.8  Psaumes 22.27  Psaumes 21.12  Actes 5.33  
 6 Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele, Fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili.
Psaumes 93.2  Luc 1.32-1.33  Psaumes 145.13  Apocalypse 19.11  Esaïe 9.6-9.7  
 7 Umeipenda haki; Umeichukia dhuluma. Kwa hiyo MUNGU, Mungu wako, amekupaka mafuta, Mafuta ya furaha kuliko wenzako.
Psaumes 33.5  Hébreux 1.9  Psaumes 21.6  Colossiens 1.18-1.19  Romains 8.29  
 8 Mavazi yako yote hunukia manemane Na udi na mdalasini. Katika majumba ya pembe Vinubi vimekufurahisha.
Cantique 1.3  2 Corinthiens 2.14-2.16  Jean 19.39  Cantique 4.6  Matthieu 2.11  
 9 Binti za wafalme wamo Miongoni mwa akina bibi wako wastahiki. Mkono wako wa kuume amesimama malkia Amevaa dhahabu ya Ofiri.1 Rois 2.19  Ephésiens 5.26-5.27  Cantique 4.8-4.11  Esaïe 60.10-60.11  Cantique 6.8-6.9  
 10 Sikia, binti, utazame, utege sikio lako, Uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako.
Cantique 2.10-2.13  Esaïe 55.1-55.3  2 Corinthiens 6.17-7.1  2 Corinthiens 5.16  Deutéronome 21.13  
 11 Naye mfalme atautamani uzuri wako, Maana ndiye bwana wako, nawe umsujudie.
Esaïe 54.5  Psaumes 95.6  Philippiens 3.8  Cantique 2.14  Ephésiens 5.26-5.27  
 12 Na binti Tiro analeta kipawa chake, Nao matajiri wa watu watajipendekeza kwako.
Psaumes 22.29  Psaumes 72.10  Esaïe 49.23  Esaïe 60.6-60.7  Matthieu 2.11  
 13 Binti mfalme yumo ndani ana fahari tupu, Mavazi yake ni ya nyuzi za dhahabu.
Esaïe 61.10  Apocalypse 19.7-19.8  Psaumes 45.9-45.10  Romains 3.22  2 Corinthiens 5.17  
 14 Atapelekwa kwa mfalme Na mavazi yaliyofumwa kwa uzuri. Wanawali wenzake wanaomfuata, Watapelekwa kwako.
Juges 5.30  Exode 28.39  Cantique 6.13  2 Corinthiens 11.2  Cantique 6.8  
 15 Watapelekwa kwa furaha na shangwe, Na kuingia katika nyumba ya mfalme.
Esaïe 56.5  Apocalypse 7.15-7.17  Esaïe 60.19-60.20  Jude 1.24  Esaïe 35.10  
 16 Badala ya baba zako watakuwapo watoto wako, Utawafanya kuwa wakuu katika nchi zote.
Apocalypse 5.10  1 Pierre 2.9  Apocalypse 1.6  Apocalypse 20.6  Philippiens 3.7-3.8  
 17 Jina lako nitalifanya kuwa kumbukumbu Katika vizazi vyote. Kwa hiyo mataifa watakushukuru Milele na milele.
Malachie 1.11  Psaumes 72.17-72.19  Esaïe 61.9  1 Corinthiens 11.26  Esaïe 62.3