Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 45.8
Bible en Swahili de l’est


Les noces du roi

1 Moyo wangu umefurika kwa neno jema, Mimi nasema niliyomfanyizia mfalme; Ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi mstadi.
2 Samuel 23.2 Esdras 7.6 Psaumes 49.3 Job 33.3 Cantique 1.12
2 Wewe u mzuri sana kuliko wanadamu; Neema imemiminiwa midomoni mwako, Kwa hiyo Mungu amekubariki hata milele.
Luc 4.22 Psaumes 21.6 Hébreux 1.3-1.4 Zacharie 9.17 Hébreux 7.26
3 Jifungie upanga wako pajani, wewe uliye hodari, Utukufu ni wako na fahari ni yako.
Hébreux 4.12 Apocalypse 1.16 Psaumes 21.5 Psaumes 96.6 Apocalypse 19.15
4 Katika fahari yako usitawi uendelee Kwa ajili ya kweli na upole na haki Na mkono wako wa kuume Utakufundisha mambo ya kutisha.
Psaumes 110.2-110.3 Psaumes 65.5 Apocalypse 6.2 Apocalypse 11.18 2 Thessaloniciens 3.1
5 Mishale yako ni mikali, watu huanguka chini yako; Imo mioyoni mwa adui za mfalme.
Psaumes 22.27 Psaumes 21.12 Psaumes 38.2 Nombres 24.8 Actes 7.54
6 Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele, Fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili.
Psaumes 93.2 Apocalypse 19.11 Esaïe 9.6-9.7 Hébreux 1.8-1.9 Daniel 2.44
7 Umeipenda haki; Umeichukia dhuluma. Kwa hiyo MUNGU, Mungu wako, amekupaka mafuta, Mafuta ya furaha kuliko wenzako.
Hébreux 1.9 Psaumes 33.5 Psaumes 21.6 Colossiens 1.18-1.19 Esaïe 61.1-61.3
8 Mavazi yako yote hunukia manemane Na udi na mdalasini. Katika majumba ya pembe Vinubi vimekufurahisha.
Cantique 1.3 Jean 19.39 Cantique 4.6 2 Corinthiens 2.14-2.16 Matthieu 2.11
9 Binti za wafalme wamo Miongoni mwa akina bibi wako wastahiki. Mkono wako wa kuume amesimama malkia Amevaa dhahabu ya Ofiri.
1 Rois 2.19 1 Rois 10.11 Apocalypse 21.24 Cantique 7.1 Job 22.24
10 Sikia, binti, utazame, utege sikio lako, Uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako.
Cantique 2.10-2.13 Deutéronome 21.13 Genèse 12.1 Esaïe 55.1-55.3 2 Corinthiens 6.17-7.1
11 Naye mfalme atautamani uzuri wako, Maana ndiye bwana wako, nawe umsujudie.
Esaïe 54.5 Psaumes 95.6 Sophonie 3.17 Romains 14.9 Psaumes 2.12
12 Na binti Tiro analeta kipawa chake, Nao matajiri wa watu watajipendekeza kwako.
Psaumes 22.29 Esaïe 49.23 Psaumes 72.10 Esaïe 60.10-60.11 Esaïe 60.3
13 Binti mfalme yumo ndani ana fahari tupu, Mavazi yake ni ya nyuzi za dhahabu.
Esaïe 61.10 Apocalypse 19.7-19.8 Luc 11.40 Matthieu 22.11-22.12 1 Pierre 3.3-3.4
14 Atapelekwa kwa mfalme Na mavazi yaliyofumwa kwa uzuri. Wanawali wenzake wanaomfuata, Watapelekwa kwako.
Juges 5.30 Cantique 5.8-5.9 Cantique 6.1 Jean 17.24 Cantique 2.7
15 Watapelekwa kwa furaha na shangwe, Na kuingia katika nyumba ya mfalme.
Esaïe 35.10 Apocalypse 3.12 Apocalypse 3.21 Esaïe 55.12-55.13 Esaïe 61.10
16 Badala ya baba zako watakuwapo watoto wako, Utawafanya kuwa wakuu katika nchi zote.
Apocalypse 5.10 Apocalypse 1.6 1 Pierre 2.9 Philippiens 3.7-3.8 Apocalypse 20.6
17 Jina lako nitalifanya kuwa kumbukumbu Katika vizazi vyote. Kwa hiyo mataifa watakushukuru Milele na milele.
Malachie 1.11 1 Corinthiens 11.26 Esaïe 62.3 Psaumes 72.17-72.19 Esaïe 61.9

Cette Bible est dans le domaine public.