Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 45.5
Bible en Swahili de l’est


Les noces du roi

1 Moyo wangu umefurika kwa neno jema, Mimi nasema niliyomfanyizia mfalme; Ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi mstadi.
2 Samuel 23.2 Job 33.3 Cantique 1.12 Esdras 7.6 Psaumes 49.3
2 Wewe u mzuri sana kuliko wanadamu; Neema imemiminiwa midomoni mwako, Kwa hiyo Mungu amekubariki hata milele.
Luc 4.22 Psaumes 21.6 Esaïe 50.4 Hébreux 1.3-1.4 Zacharie 9.17
3 Jifungie upanga wako pajani, wewe uliye hodari, Utukufu ni wako na fahari ni yako.
Apocalypse 1.16 Hébreux 4.12 Esaïe 49.2 Psaumes 21.5 Psaumes 96.6
4 Katika fahari yako usitawi uendelee Kwa ajili ya kweli na upole na haki Na mkono wako wa kuume Utakufundisha mambo ya kutisha.
Apocalypse 6.2 Psaumes 110.2-110.3 Psaumes 65.5 1 Thessaloniciens 2.13 1 Thessaloniciens 1.5
5 Mishale yako ni mikali, watu huanguka chini yako; Imo mioyoni mwa adui za mfalme.
Psaumes 38.2 Nombres 24.8 Psaumes 22.27 Psaumes 21.12 Actes 5.33
6 Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele, Fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili.
Psaumes 93.2 Luc 1.32-1.33 Psaumes 145.13 Apocalypse 19.11 Esaïe 9.6-9.7
7 Umeipenda haki; Umeichukia dhuluma. Kwa hiyo MUNGU, Mungu wako, amekupaka mafuta, Mafuta ya furaha kuliko wenzako.
Psaumes 33.5 Hébreux 1.9 Psaumes 21.6 Colossiens 1.18-1.19 Romains 8.29
8 Mavazi yako yote hunukia manemane Na udi na mdalasini. Katika majumba ya pembe Vinubi vimekufurahisha.
Cantique 1.3 2 Corinthiens 2.14-2.16 Jean 19.39 Cantique 4.6 Matthieu 2.11
9 Binti za wafalme wamo Miongoni mwa akina bibi wako wastahiki. Mkono wako wa kuume amesimama malkia Amevaa dhahabu ya Ofiri.
1 Rois 2.19 Ephésiens 5.26-5.27 Cantique 4.8-4.11 Esaïe 60.10-60.11 Cantique 6.8-6.9
10 Sikia, binti, utazame, utege sikio lako, Uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako.
Cantique 2.10-2.13 Esaïe 55.1-55.3 2 Corinthiens 6.17-7.1 2 Corinthiens 5.16 Deutéronome 21.13
11 Naye mfalme atautamani uzuri wako, Maana ndiye bwana wako, nawe umsujudie.
Esaïe 54.5 Psaumes 95.6 Philippiens 3.8 Cantique 2.14 Ephésiens 5.26-5.27
12 Na binti Tiro analeta kipawa chake, Nao matajiri wa watu watajipendekeza kwako.
Psaumes 22.29 Psaumes 72.10 Esaïe 49.23 Esaïe 60.6-60.7 Matthieu 2.11
13 Binti mfalme yumo ndani ana fahari tupu, Mavazi yake ni ya nyuzi za dhahabu.
Esaïe 61.10 Apocalypse 19.7-19.8 Psaumes 45.9-45.10 Romains 3.22 2 Corinthiens 5.17
14 Atapelekwa kwa mfalme Na mavazi yaliyofumwa kwa uzuri. Wanawali wenzake wanaomfuata, Watapelekwa kwako.
Juges 5.30 Exode 28.39 Cantique 6.13 2 Corinthiens 11.2 Cantique 6.8
15 Watapelekwa kwa furaha na shangwe, Na kuingia katika nyumba ya mfalme.
Esaïe 56.5 Apocalypse 7.15-7.17 Esaïe 60.19-60.20 Jude 1.24 Esaïe 35.10
16 Badala ya baba zako watakuwapo watoto wako, Utawafanya kuwa wakuu katika nchi zote.
Apocalypse 5.10 1 Pierre 2.9 Apocalypse 1.6 Apocalypse 20.6 Philippiens 3.7-3.8
17 Jina lako nitalifanya kuwa kumbukumbu Katika vizazi vyote. Kwa hiyo mataifa watakushukuru Milele na milele.
Malachie 1.11 Psaumes 72.17-72.19 Esaïe 61.9 1 Corinthiens 11.26 Esaïe 62.3

Cette Bible est dans le domaine public.