Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 45.13
Bible en Swahili de l’est


Les noces du roi

1 Moyo wangu umefurika kwa neno jema, Mimi nasema niliyomfanyizia mfalme; Ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi mstadi.
2 Samuel 23.2 Esdras 7.6 Psaumes 49.3 Job 33.3 Cantique 1.12
2 Wewe u mzuri sana kuliko wanadamu; Neema imemiminiwa midomoni mwako, Kwa hiyo Mungu amekubariki hata milele.
Luc 4.22 Psaumes 21.6 Zacharie 9.17 Hébreux 7.26 Jean 1.14
3 Jifungie upanga wako pajani, wewe uliye hodari, Utukufu ni wako na fahari ni yako.
Hébreux 4.12 Apocalypse 1.16 Psaumes 96.6 Apocalypse 19.15 Esaïe 49.2
4 Katika fahari yako usitawi uendelee Kwa ajili ya kweli na upole na haki Na mkono wako wa kuume Utakufundisha mambo ya kutisha.
Psaumes 65.5 Apocalypse 6.2 Psaumes 110.2-110.3 Esaïe 63.1-63.6 Matthieu 11.29
5 Mishale yako ni mikali, watu huanguka chini yako; Imo mioyoni mwa adui za mfalme.
Psaumes 21.12 Psaumes 38.2 Nombres 24.8 Psaumes 22.27 Actes 4.4
6 Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele, Fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili.
Psaumes 93.2 Esaïe 9.6-9.7 Hébreux 1.8-1.9 Daniel 2.44 Jérémie 23.5-23.6
7 Umeipenda haki; Umeichukia dhuluma. Kwa hiyo MUNGU, Mungu wako, amekupaka mafuta, Mafuta ya furaha kuliko wenzako.
Hébreux 1.9 Psaumes 33.5 Psaumes 21.6 Colossiens 1.18-1.19 Esaïe 61.1-61.3
8 Mavazi yako yote hunukia manemane Na udi na mdalasini. Katika majumba ya pembe Vinubi vimekufurahisha.
Cantique 1.3 Jean 19.39 Cantique 4.6 2 Corinthiens 2.14-2.16 Matthieu 2.11
9 Binti za wafalme wamo Miongoni mwa akina bibi wako wastahiki. Mkono wako wa kuume amesimama malkia Amevaa dhahabu ya Ofiri.
1 Rois 2.19 Cantique 7.1 Job 22.24 Esaïe 49.23 Jean 3.29
10 Sikia, binti, utazame, utege sikio lako, Uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako.
Cantique 2.10-2.13 Genèse 12.1 Esaïe 55.1-55.3 2 Corinthiens 6.17-7.1 2 Corinthiens 5.16
11 Naye mfalme atautamani uzuri wako, Maana ndiye bwana wako, nawe umsujudie.
Esaïe 54.5 Psaumes 95.6 Luc 24.52 Cantique 4.9-4.10 Jean 4.21-4.22
12 Na binti Tiro analeta kipawa chake, Nao matajiri wa watu watajipendekeza kwako.
Psaumes 22.29 Esaïe 49.23 Psaumes 72.10 Esaïe 23.17-23.18 Psaumes 68.29
13 Binti mfalme yumo ndani ana fahari tupu, Mavazi yake ni ya nyuzi za dhahabu.
Esaïe 61.10 Apocalypse 19.7-19.8 1 Pierre 3.3-3.4 1 Samuel 16.7 Apocalypse 3.18
14 Atapelekwa kwa mfalme Na mavazi yaliyofumwa kwa uzuri. Wanawali wenzake wanaomfuata, Watapelekwa kwako.
Juges 5.30 Cantique 6.1 Jean 17.24 Cantique 2.7 Cantique 1.3-1.5
15 Watapelekwa kwa furaha na shangwe, Na kuingia katika nyumba ya mfalme.
Apocalypse 3.21 Esaïe 55.12-55.13 Esaïe 61.10 Esaïe 56.5 Apocalypse 7.15-7.17
16 Badala ya baba zako watakuwapo watoto wako, Utawafanya kuwa wakuu katika nchi zote.
Apocalypse 5.10 Apocalypse 1.6 1 Pierre 2.9 Apocalypse 20.6 Philippiens 3.7-3.8
17 Jina lako nitalifanya kuwa kumbukumbu Katika vizazi vyote. Kwa hiyo mataifa watakushukuru Milele na milele.
Malachie 1.11 1 Corinthiens 11.26 Esaïe 62.3 Psaumes 72.17-72.19 Esaïe 61.9

Cette Bible est dans le domaine public.