Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 38.21
Bible en Swahili de l’est


Demande de grâce

1 Ee Bwana, usinilaumu katika ghadhabu yako, Wala usiniadhibu kwa ukali wa hasira yako.
Psaumes 6.1 Hébreux 12.5-12.11 Psaumes 70.1 Esaïe 54.8 Esaïe 27.8
2 Kwa maana mishale yako imenichoma, Na mkono wako umenipata.
Job 6.4 Psaumes 32.4 Psaumes 64.7 1 Samuel 5.11 Psaumes 21.12
3 Hamna uzima katika mwili wangu Kwa sababu ya ghadhabu yako. Wala hamna amani mifupani mwangu Kwa sababu ya hatia zangu.
Psaumes 51.8 Psaumes 6.2 Psaumes 31.9-31.10 Esaïe 1.5-1.6 Job 33.19-33.22
4 Maana dhambi zangu zimenifunikiza kichwa, Kama mzigo mzito zimenilemea mno.
Esdras 9.6 Psaumes 40.12 Lévitique 7.18 Matthieu 11.28 Esaïe 53.11
5 Jeraha zangu zinanuka, zimeoza, Kwa sababu ya upumbavu wangu.
Psaumes 69.5 Psaumes 38.7 Esaïe 1.5-1.6 Jérémie 8.22 Psaumes 32.3
6 Nimepindika na kuinama sana, Mchana kutwa nimekwenda nikihuzunika.
Job 30.28 Psaumes 35.14 Psaumes 42.9 Psaumes 43.2 Psaumes 42.5
7 Maana viuno vyangu vimejaa homa, Wala hamna uzima katika mwili wangu.
Actes 12.23 Psaumes 41.8 2 Chroniques 21.18-21.19 Job 30.18 Job 7.5
8 Nimedhoofika na kuchubuka sana, Nimeugua kwa fadhaa ya moyo wangu.
Job 3.24 Psaumes 32.3 Psaumes 22.1-22.2 Esaïe 59.11 Job 30.28
9 Bwana, haja zangu zote ziko mbele zako, Kuugua kwangu hakukusitirika kwako.
Psaumes 6.6 Psaumes 102.5 Romains 8.26-8.27 Psaumes 10.17 Romains 8.22-8.23
10 Moyo wangu unapwita-pwita, Nguvu zangu zimeniacha; Nuru ya macho yangu nayo imeniondoka.
Psaumes 6.7 Psaumes 69.3 Psaumes 88.9 Psaumes 31.10 Psaumes 42.1
11 Wanipendao na rafiki zangu wanasimama mbali na pigo langu; Naam, karibu zangu wamesimama mbali.
Psaumes 31.11 Luc 23.49 Luc 10.31-10.32 Job 19.13-19.17 Esaïe 53.8
12 Nao wanaoutafuta uhai wangu hutega mitego; Nao wanaotaka kunidhuru hunena mabaya; Na kufikiri hila mchana kutwa.
Psaumes 35.20 Psaumes 140.5 Psaumes 64.2-64.5 2 Samuel 17.1-17.3 2 Samuel 16.7-16.8
13 Lakini kama kiziwi sisikii, Nami ni kama bubu asiyefumbua kinywa chake.
Psaumes 39.9 Psaumes 39.2 1 Pierre 2.23 Esaïe 53.7 2 Samuel 16.10-16.12
14 Naam, nimekuwa kama mtu asiyesikia, Ambaye hamna hoja kinywani mwake.
Marc 15.3-15.5 Michée 7.5 Jean 8.6 Amos 5.13
15 Kwa kuwa nakungoja Wewe, Bwana, Wewe utajibu, Ee Bwana, Mungu wangu.
Psaumes 39.7 Psaumes 123.1-123.3 Psaumes 17.6 Psaumes 138.3
16 Maana nalisema, Wasije wakanifurahia; Mguu wangu ukiteleza wajitukuza juu yangu.
Psaumes 94.18 Psaumes 13.3-13.4 Psaumes 35.24-35.26 Deutéronome 32.35
17 Kwa maana mimi ni karibu na kusita, Na maumivu yangu yako mbele yangu daima.
Psaumes 35.15 Psaumes 38.6 Psaumes 6.6 Psaumes 77.2-77.3 Esaïe 53.3-53.5
18 Kwa maana nitaungama uovu wangu, Na kusikitika kwa dhambi zangu.
Psaumes 32.5 Proverbes 28.13 Psaumes 51.3 2 Corinthiens 7.7-7.11 Job 33.27
19 Lakini adui zangu ni wazima wenye nguvu, Nao wanaonichukia bure wamekuwa wengi.
Psaumes 35.19 Jean 15.18-15.25 Psaumes 25.19 Psaumes 3.1 Psaumes 59.1-59.3
20 Naam, wakilipa mabaya kwa mema, Huwa adui zangu kwa kuwa nalifuata lililo jema.
Psaumes 35.12 1 Jean 3.12 1 Samuel 25.21 Jérémie 18.20 1 Samuel 23.12
21 Wewe, Bwana, usiniache, Mungu wangu, usijitenge nami.
Psaumes 22.19 Psaumes 22.1 Psaumes 35.21-35.22 Psaumes 22.11 Psaumes 22.24
22 Ufanye haraka kunisaidia, Ee Bwana, wokovu wangu.
Psaumes 40.13 Psaumes 27.1 Psaumes 40.17 Psaumes 62.2 Psaumes 141.1

Cette Bible est dans le domaine public.