Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 38
Bible en Swahili de l’est


Demande de grâce

1 Ee Bwana, usinilaumu katika ghadhabu yako, Wala usiniadhibu kwa ukali wa hasira yako.
Psaumes 6.1 Hébreux 12.5-12.11 Psaumes 70.1 Esaïe 54.8 Jérémie 30.11
2 Kwa maana mishale yako imenichoma, Na mkono wako umenipata.
Job 6.4 Psaumes 32.4 1 Samuel 5.6 Lamentations 3.12 Psaumes 64.7
3 Hamna uzima katika mwili wangu Kwa sababu ya ghadhabu yako. Wala hamna amani mifupani mwangu Kwa sababu ya hatia zangu.
Psaumes 51.8 Psaumes 6.2 Job 2.7-2.8 Psaumes 102.3 Psaumes 31.9-31.10
4 Maana dhambi zangu zimenifunikiza kichwa, Kama mzigo mzito zimenilemea mno.
Esdras 9.6 Psaumes 40.12 1 Pierre 2.24 Lévitique 7.18 Matthieu 11.28
5 Jeraha zangu zinanuka, zimeoza, Kwa sababu ya upumbavu wangu.
Jérémie 8.22 Psaumes 32.3 Psaumes 69.5 Psaumes 38.7 Esaïe 1.5-1.6
6 Nimepindika na kuinama sana, Mchana kutwa nimekwenda nikihuzunika.
Job 30.28 Psaumes 35.14 Psaumes 42.9 Psaumes 43.2 Psaumes 42.5
7 Maana viuno vyangu vimejaa homa, Wala hamna uzima katika mwili wangu.
Job 7.5 Psaumes 102.3 Actes 12.23 Psaumes 41.8 2 Chroniques 21.18-21.19
8 Nimedhoofika na kuchubuka sana, Nimeugua kwa fadhaa ya moyo wangu.
Psaumes 32.3 Job 3.24 Job 30.28 Psaumes 22.1-22.2 Esaïe 59.11
9 Bwana, haja zangu zote ziko mbele zako, Kuugua kwangu hakukusitirika kwako.
Psaumes 6.6 Psaumes 102.5 2 Corinthiens 5.2 Jean 1.48 Romains 8.26-8.27
10 Moyo wangu unapwita-pwita, Nguvu zangu zimeniacha; Nuru ya macho yangu nayo imeniondoka.
Psaumes 6.7 Psaumes 69.3 Psaumes 88.9 Lamentations 5.16-5.17 Psaumes 143.4-143.7
11 Wanipendao na rafiki zangu wanasimama mbali na pigo langu; Naam, karibu zangu wamesimama mbali.
Psaumes 31.11 Luc 23.49 Luc 10.31-10.32 Job 19.13-19.17 Esaïe 53.8
12 Nao wanaoutafuta uhai wangu hutega mitego; Nao wanaotaka kunidhuru hunena mabaya; Na kufikiri hila mchana kutwa.
Psaumes 35.20 Psaumes 140.5 Psaumes 35.4 Psaumes 64.2-64.5 2 Samuel 17.1-17.3
13 Lakini kama kiziwi sisikii, Nami ni kama bubu asiyefumbua kinywa chake.
Psaumes 39.2 Psaumes 39.9 1 Pierre 2.23 Esaïe 53.7 2 Samuel 16.10-16.12
14 Naam, nimekuwa kama mtu asiyesikia, Ambaye hamna hoja kinywani mwake.
Jean 8.6 Amos 5.13 Marc 15.3-15.5 Michée 7.5
15 Kwa kuwa nakungoja Wewe, Bwana, Wewe utajibu, Ee Bwana, Mungu wangu.
Psaumes 39.7 Psaumes 138.3 Psaumes 123.1-123.3 Psaumes 17.6
16 Maana nalisema, Wasije wakanifurahia; Mguu wangu ukiteleza wajitukuza juu yangu.
Psaumes 94.18 Deutéronome 32.35 Psaumes 13.3-13.4 Psaumes 35.24-35.26
17 Kwa maana mimi ni karibu na kusita, Na maumivu yangu yako mbele yangu daima.
Psaumes 35.15 Psaumes 38.6 Michée 4.6-4.7 Psaumes 6.6 Psaumes 77.2-77.3
18 Kwa maana nitaungama uovu wangu, Na kusikitika kwa dhambi zangu.
Psaumes 32.5 Proverbes 28.13 Job 31.33 Psaumes 51.3 2 Corinthiens 7.7-7.11
19 Lakini adui zangu ni wazima wenye nguvu, Nao wanaonichukia bure wamekuwa wengi.
Psaumes 35.19 Psaumes 56.1-56.2 Jean 15.18-15.25 Psaumes 25.19 Psaumes 3.1
20 Naam, wakilipa mabaya kwa mema, Huwa adui zangu kwa kuwa nalifuata lililo jema.
Psaumes 35.12 1 Jean 3.12 Psaumes 109.3-109.5 1 Samuel 25.21 Jérémie 18.20
21 Wewe, Bwana, usiniache, Mungu wangu, usijitenge nami.
Psaumes 22.19 Psaumes 22.11 Psaumes 22.24 Psaumes 22.1 Psaumes 35.21-35.22
22 Ufanye haraka kunisaidia, Ee Bwana, wokovu wangu.
Psaumes 40.13 Psaumes 27.1 Psaumes 40.17 Psaumes 70.1 Psaumes 62.2

Cette Bible est dans le domaine public.