Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 21.1
Bible en Swahili de l’est


Reconnaissance du roi

1 Ee Bwana, mfalme atazifurahia nguvu zako, Na wokovu wako ataufanyia shangwe nyingi sana.
Psaumes 28.7 Matthieu 2.2 Psaumes 99.4 Hébreux 12.2 Psaumes 118.14-118.15
2 Umempa haja ya moyo wake, Wala hukumzuilia matakwa ya midomo yake.
Psaumes 20.4-20.5 Psaumes 92.11 Psaumes 37.4 Hébreux 7.25 Psaumes 2.8-2.9
3 Maana umemsogezea baraka za heri, Umemvika taji ya dhahabu safi kichwani pake.
2 Samuel 12.30 1 Chroniques 20.2 Job 41.11 Hébreux 2.9 Romains 2.4
4 Alikuomba uhai, ukampa, Muda mrefu wa siku nyingi, milele na milele.
Psaumes 91.16 Psaumes 61.5-61.6 Psaumes 72.17 Psaumes 89.29 Psaumes 119.175
5 Utukufu wake ni mkuu kwa wokovu wako, Heshima na adhama waweka juu yake.
Jean 13.31-13.32 Psaumes 96.6 2 Samuel 7.19 Apocalypse 5.8-5.13 Psaumes 3.3
6 Maana umemfanya kuwa baraka za milele, Wamfurahisha kwa furaha ya uso wako.
Psaumes 45.7 Psaumes 16.11 Actes 2.28 Ephésiens 1.3 Psaumes 43.4
7 Kwa kuwa mfalme humtumaini Bwana, Na kwa fadhili zake Aliye juu hataondoshwa.
Psaumes 16.8 Psaumes 91.9-91.10 Psaumes 9.2 1 Samuel 30.6 Matthieu 27.43
8 Mkono wako utawapata adui zako wote, Mkono wako wa kuume utawapata wanaokuchukia.
Esaïe 10.10 Psaumes 72.9 Luc 19.14 Psaumes 89.22-89.23 Psaumes 18.1
9 Utawafanya kuwa kama tanuru ya moto, Wakati wa ghadhabu yako. Bwana atawameza kwa ghadhabu yake, Na moto utawala.
Malachie 4.1 Lamentations 2.2 Psaumes 18.8 Psaumes 50.3 Psaumes 2.5
10 Matunda yao utayaharibu na kuyaondoa katika nchi, Na wazao wao katika wanadamu.
Psaumes 37.28 Esaïe 14.20 Psaumes 109.13 1 Rois 13.34 Job 18.16-18.19
11 Madhali walinuia kukutenda mabaya, Waliwaza hila wasipate kuitimiza.
Psaumes 2.1 Psaumes 10.2 Matthieu 2.8 Actes 4.17-4.18 Ezéchiel 11.2
12 Kwa maana utawafanya kukupa kisogo, Kwa upote wa uta wako ukiwaelekezea mishale.
Psaumes 7.12-7.13 Psaumes 18.40 Psaumes 9.3 Job 16.12-16.13 Psaumes 44.10
13 Ee Bwana, utukuzwe kwa nguvu zako, Nasi tutaimba na kuuhimidi uweza wako.
Apocalypse 19.1-19.6 Psaumes 113.5 Apocalypse 11.17 1 Chroniques 29.11 Psaumes 57.5

Cette Bible est dans le domaine public.