Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 109.4
Bible en Swahili de l’est


Imprécation contre le méchant

1 Ee Mungu wa sifa zangu, usinyamaze,
Psaumes 83.1 Deutéronome 10.21 Psaumes 28.1 Jérémie 17.14 Esaïe 42.14
2 Kwa maana wamenifumbulia kinywa; Kinywa cha mtu asiye haki, cha hila, Wamesema nami kwa ulimi wa uongo.
Psaumes 52.4 Jérémie 9.3 Jérémie 9.5 Matthieu 26.59-26.62 2 Samuel 15.3-15.8
3 Naam, kwa maneno ya chuki wamenizunguka, Wamepigana nami bure.
Psaumes 69.4 Psaumes 35.7 Psaumes 22.12 Jean 15.24-15.25 1 Samuel 26.18
4 Badala ya upendo wangu wao hunishitaki, Ijapokuwa naliwaombea.
Psaumes 38.20 Luc 23.34 2 Samuel 13.39 Psaumes 35.12 Psaumes 69.12-69.13
5 Wamenichukuza mabaya badala ya mema, Na chuki badala ya upendo wangu.
Proverbes 17.13 Psaumes 38.20 Marc 14.44-14.45 2 Samuel 15.12 Luc 22.47-22.48
6 Uweke mtu mkorofi juu yake, Mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
Zacharie 3.1 Matthieu 5.25 Jean 13.2 Matthieu 27.4 Jean 13.27
7 Katika kuhukumiwa ataonekana hana haki, Na sala yake itadhaniwa kuwa ni dhambi.
Proverbes 28.9 Proverbes 15.8 Proverbes 21.27 Galates 3.10 Romains 3.19
8 Siku zake na ziwe chache, Usimamizi wake na atwae mtu mwingine.
Psaumes 55.23 Actes 1.16-1.26 Matthieu 27.5
9 Wanawe na wawe yatima, Na mkewe na awe mjane.
Exode 22.24 Jérémie 18.21 Lamentations 5.3
10 Kutanga na watange wanawe na kuomba, Watafute chakula mbali na mahame yao.
Psaumes 37.25 Job 30.3-30.9 Job 24.8-24.12 Genèse 4.12-4.14 Esaïe 16.2
11 Mdai na anase vitu vyote alivyo navyo, Wageni na wateke mapato ya kazi yake.
Job 5.5 Job 20.18 Deutéronome 28.33-28.34 Deutéronome 28.50-28.51 Deutéronome 28.29
12 Asiwe na mtu wa kumfanyia fadhili, Wala mtu wa kuwahurumia yatima wake.
Esaïe 13.18 Luc 6.38 Esaïe 9.17 Psaumes 137.8-137.9 Job 5.4
13 Wazao wake waangamizwe, Jina lao likafutwe katika kizazi cha pili.
Proverbes 10.7 Psaumes 37.28 Job 18.19 1 Samuel 2.31-2.33 Psaumes 21.10
14 Uovu wa baba zake ukumbukwe mbele za Bwana, Na dhambi ya mamaye isifutwe.
Jérémie 18.23 Exode 20.5 Néhémie 4.5 2 Samuel 21.1 Lévitique 26.39
15 Ziwe mbele za Bwana daima, Aliondoe kumbukumbu lao duniani.
Psaumes 34.16 Psaumes 90.8 Job 18.17 Esaïe 65.15 Deutéronome 32.34
16 Kwa kuwa hakukumbuka kutenda fadhili, Bali alimfukuza mnyonge na mhitaji, Hata akamfisha mtu aliyevunjika moyo,
Psaumes 34.18 Psaumes 37.14 Matthieu 18.33-18.35 Psaumes 10.2 2 Samuel 17.1-17.2
17 Naye alipenda kulaani, nako kukampata. Hakupendezwa na kubariki, kukawa mbali naye,
Proverbes 14.14 Ezéchiel 35.6 Matthieu 7.2 Apocalypse 16.6 Psaumes 59.12-59.13
18 Alijivika laana kana kwamba ni vazi lake. Ikamwingilia moyoni kama maji, Na kama mafuta mifupani mwake.
Nombres 5.22 Psaumes 73.6 1 Pierre 5.5 Actes 1.18 Actes 1.25
19 Na iwe kwake kama vazi ajivikalo, Na kama mshipi ajifungao daima.
Psaumes 109.29 Psaumes 109.18 Psaumes 35.26 Psaumes 132.18
20 Ndiyo malipo ya washitaki wangu toka kwa Bwana, Na ya hao wanaoisingizia nafsi yangu mabaya.
1 Corinthiens 12.3 Marc 9.39 Psaumes 110.5-110.6 Matthieu 26.66-26.67 2 Samuel 18.32
21 Na Wewe, MUNGU, Bwana, unitendee kwa ajili ya jina lako, Kwa kuwa fadhili zako ni njema uniokoe.
Psaumes 25.11 Psaumes 63.3 Psaumes 79.9-79.10 Psaumes 31.3 Psaumes 69.16
22 Kwa maana mimi ni mnyonge na mhitaji, Na moyo wangu umejeruhi ndani yangu.
Psaumes 40.17 Psaumes 86.1 2 Corinthiens 8.9 2 Rois 4.27 Psaumes 88.15-88.16
23 Ninapita kama kivuli kianzacho kutoweka, Ninapeperushwa kama nzige.
Exode 10.19 Ecclésiaste 8.13 Ecclésiaste 6.12 Psaumes 144.4 Jacques 4.14
24 Magoti yangu yamedhoofu kwa kufunga, Na mwili wangu umekonda kwa kukosa mafuta.
Hébreux 12.12 Psaumes 32.3-32.4 Psaumes 69.10 Matthieu 4.2 Psaumes 35.13-35.14
25 Nami nalikuwa laumu kwao, Wanionapo hutikisa vichwa vyao.
Psaumes 22.6-22.7 Psaumes 69.19-69.20 Romains 15.3 Marc 15.29 Job 16.4
26 Ee Bwana, Mungu wangu, unisaidie, Uniokoe sawasawa na fadhili zako.
Psaumes 119.86 Psaumes 69.16 Psaumes 57.1 Psaumes 69.13 Hébreux 5.7
27 Nao wakajue ya kuwa ndio mkono wako; Wewe, Bwana, umeyafanya hayo.
Job 37.7 1 Samuel 17.46-17.47 Nombres 16.28-16.30 1 Rois 18.36-18.37 Psaumes 64.8-64.9
28 Wao walaani, bali Wewe utabariki, Wameondoka wao wakaaibishwa, Bali mtumishi wako atafurahi.
Hébreux 12.2 Nombres 23.23 2 Samuel 16.10-16.13 Nombres 22.12 Esaïe 65.13-65.16
29 Washitaki wangu watavikwa fedheha, Watajivika aibu yao kama joho.
Psaumes 35.26 Psaumes 132.18 Job 8.22 Daniel 12.2 Jérémie 20.11
30 Nitamshukuru Bwana kwa kinywa changu, Naam, nitamsifu katikati ya mkutano.
Psaumes 35.18 Psaumes 111.1 Psaumes 22.22-22.25 Psaumes 108.1-108.3 Psaumes 9.1
31 Maana atasimama mkono wa kuume wa mhitaji Amwokoe na wanaoihukumu nafsi yake.
Psaumes 16.8 Psaumes 121.5 Psaumes 73.23 Psaumes 110.5 Psaumes 72.4

Cette Bible est dans le domaine public.