Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 4.13
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 1 d’Éliphaz

1 Ndipo huyo Elifazi, Mtemani, akajibu na kusema,
Job 6.1 Job 8.1 Job 2.11 Job 15.1 Job 3.1-3.2
2 Mtu akijaribu kuzungumza nawe, je! Utaona ni vibaya? Lakini ni nani awezaye kujizuia asinene?
Job 32.18-32.20 Actes 4.20 2 Corinthiens 2.4-2.6 Jérémie 20.9 Jérémie 6.11
3 Tazama, wewe umewafunza watu wengi, Nawe umeitia nguvu mikono iliyokuwa minyonge.
Esaïe 35.3 Hébreux 12.12 Esaïe 50.4 Esdras 6.22 Genèse 18.19
4 Maneno yako yamemtegemeza huyo aliyekuwa anaanguka, Nawe umeyaimarisha magoti manyonge.
Hébreux 12.12 Psaumes 145.14 Proverbes 12.18 Proverbes 16.23-16.24 2 Corinthiens 7.6
5 Lakini sasa haya yamekufikilia wewe, nawe wafa moyo; Yamekugusa, nawe wafadhaika.
Job 19.21 2 Corinthiens 4.1 Job 1.11 Proverbes 24.10 Job 2.5
6 Je! Dini yako siyo mataraja yako, Na matumaini yako si huo uelekevu wa njia zako?
Proverbes 3.26 Job 1.1 Job 1.8-1.10 Job 13.15 Job 27.5-27.6
7 Kumbuka, tafadhali, ni nani aliyeangamia akiwa hana hatia? Au hao waelekevu, walikatiliwa mbali wapi?
Psaumes 37.25 2 Pierre 2.9 Job 9.22-9.23 Actes 28.4 Job 36.7
8 Kama mimi nilivyoona, hao walimao maovu, Na kupanda madhara, huvuna yayo hayo.
Proverbes 22.8 Galates 6.7-6.8 Osée 8.7 Osée 10.12-10.13 Jérémie 4.18
9 Kwa pumzi za Mungu huangamia. Na kwa kuvuma kwa hasira zake humalizika.
Esaïe 30.33 Job 15.30 2 Thessaloniciens 2.8 Esaïe 11.4 Exode 15.8
10 Kunguruma kwake simba, na sauti ya simba mkali, Na meno ya simba wachanga, yamevunjika.
Psaumes 58.6 Job 29.17 Psaumes 3.7 Job 5.15 Proverbes 30.14
11 Simba mzee huangamia kwa kukosa mawindo, Nao watoto wa simba mke wametawanyika mbalimbali.
Psaumes 34.10 Jérémie 4.7 2 Timothée 4.17 Nombres 23.24 Psaumes 7.2
12 Basi, nililetewa neno kwa siri, Sikio langu likasikia manong’ono yake.
Job 26.14 1 Corinthiens 13.12 Psaumes 62.11
13 Katika mawazo yaliyotoka katika maono ya usiku, Hapo usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu.
Job 33.14-33.16 Genèse 2.21 Genèse 15.12 Genèse 20.3 Genèse 31.24
14 Hofu iliniangukia na kutetema, Iliyoitetemesha mifupa yangu yote.
Habakuk 3.16 Job 7.14 Esaïe 6.5 Daniel 10.11 Apocalypse 1.17
15 Ndipo pepo ilipita mbele ya uso wangu; Na nywele za mwili wangu zilisimama.
Esaïe 13.8 Hébreux 1.14 Hébreux 1.7 Luc 24.37-24.39 Matthieu 14.26
16 Hiyo pepo ilisimama kimya, nisiweze kutambua sura zake, Mfano ulikuwa mbele ya macho yangu; Kulikuwa kimya, nami nilisikia sauti, ikinena,
1 Rois 19.12
17 Je! Binadamu atakuwa na haki kuliko Mungu? Je! Mtu atakuwa safi kuliko Muumba wake?
Job 9.2 Job 25.4 Psaumes 143.2 Job 8.3 Psaumes 145.17
18 Tazama, yeye hawategemei watumishi wake; Na malaika zake huwahesabia upuzi;
2 Pierre 2.4 Job 25.5-25.6 Jude 1.6 Job 15.15-15.16 Esaïe 6.2-6.3
19 Je! Si zaidi sana hao wakaao katika nyumba za udongo, Ambazo misingi yao i katika mchanga, Hao waliosetwa mbele ya nondo!
Job 10.9 Genèse 2.7 Genèse 3.19 Job 33.6 2 Corinthiens 4.7
20 Kati ya asubuhi na jioni huvunjwa-vunjwa; Waangamia milele wala hapana atiaye moyoni.
Job 20.7 Job 16.22 Psaumes 90.5-90.6 Psaumes 39.13 Proverbes 10.7
21 Je! Kamba ya hema yao haikung’olewa ndani yao? Wafa, kisha hali hawana akili.
Job 36.12 Luc 16.22-16.23 Job 8.22 Psaumes 39.5 Esaïe 2.22

Cette Bible est dans le domaine public.