Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 4.10
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 1 d’Éliphaz

1 Ndipo huyo Elifazi, Mtemani, akajibu na kusema,
Job 3.1-3.2 Job 42.9 Job 22.1 Job 6.1 Job 8.1
2 Mtu akijaribu kuzungumza nawe, je! Utaona ni vibaya? Lakini ni nani awezaye kujizuia asinene?
Job 32.18-32.20 Actes 4.20 Jérémie 6.11 2 Corinthiens 7.8-7.10 2 Corinthiens 2.4-2.6
3 Tazama, wewe umewafunza watu wengi, Nawe umeitia nguvu mikono iliyokuwa minyonge.
Esaïe 35.3 Hébreux 12.12 Colossiens 4.6 Ezéchiel 13.22 Job 16.5
4 Maneno yako yamemtegemeza huyo aliyekuwa anaanguka, Nawe umeyaimarisha magoti manyonge.
Hébreux 12.12 2 Corinthiens 7.6 Daniel 5.6 2 Corinthiens 2.7 Esaïe 35.3-35.4
5 Lakini sasa haya yamekufikilia wewe, nawe wafa moyo; Yamekugusa, nawe wafadhaika.
Job 19.21 Job 2.5 Job 3.25-3.26 Job 6.14 Hébreux 12.3
6 Je! Dini yako siyo mataraja yako, Na matumaini yako si huo uelekevu wa njia zako?
Proverbes 3.26 Job 1.1 Job 16.17 1 Pierre 1.13 Job 29.12-29.17
7 Kumbuka, tafadhali, ni nani aliyeangamia akiwa hana hatia? Au hao waelekevu, walikatiliwa mbali wapi?
Psaumes 37.25 2 Pierre 2.9 Job 8.20 Ecclésiaste 7.15 Ecclésiaste 9.1-9.2
8 Kama mimi nilivyoona, hao walimao maovu, Na kupanda madhara, huvuna yayo hayo.
Proverbes 22.8 Galates 6.7-6.8 Osée 8.7 Psaumes 7.14-7.16 Job 15.35
9 Kwa pumzi za Mungu huangamia. Na kwa kuvuma kwa hasira zake humalizika.
Esaïe 30.33 Job 15.30 Esaïe 11.4 2 Thessaloniciens 2.8 Exode 15.8
10 Kunguruma kwake simba, na sauti ya simba mkali, Na meno ya simba wachanga, yamevunjika.
Psaumes 58.6 Psaumes 3.7 Job 29.17 Psaumes 57.4 Job 5.15
11 Simba mzee huangamia kwa kukosa mawindo, Nao watoto wa simba mke wametawanyika mbalimbali.
Psaumes 34.10 Genèse 49.9 Job 1.19 Job 8.3-8.4 Nombres 24.9
12 Basi, nililetewa neno kwa siri, Sikio langu likasikia manong’ono yake.
Job 26.14 1 Corinthiens 13.12 Psaumes 62.11
13 Katika mawazo yaliyotoka katika maono ya usiku, Hapo usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu.
Genèse 2.21 Genèse 15.12 Job 33.14-33.16 Daniel 2.19 Genèse 46.2
14 Hofu iliniangukia na kutetema, Iliyoitetemesha mifupa yangu yote.
Habakuk 3.16 Apocalypse 1.17 Psaumes 119.120 Job 33.19 Luc 1.12
15 Ndipo pepo ilipita mbele ya uso wangu; Na nywele za mwili wangu zilisimama.
Matthieu 14.26 Daniel 5.6 Esaïe 21.3-21.4 Psaumes 104.4 Esaïe 13.8
16 Hiyo pepo ilisimama kimya, nisiweze kutambua sura zake, Mfano ulikuwa mbele ya macho yangu; Kulikuwa kimya, nami nilisikia sauti, ikinena,
1 Rois 19.12
17 Je! Binadamu atakuwa na haki kuliko Mungu? Je! Mtu atakuwa safi kuliko Muumba wake?
Job 9.2 Job 25.4 Psaumes 143.2 Jérémie 12.1 Romains 9.20
18 Tazama, yeye hawategemei watumishi wake; Na malaika zake huwahesabia upuzi;
2 Pierre 2.4 Job 25.5-25.6 Jude 1.6 Job 15.15-15.16 Psaumes 103.20-103.21
19 Je! Si zaidi sana hao wakaao katika nyumba za udongo, Ambazo misingi yao i katika mchanga, Hao waliosetwa mbele ya nondo!
Job 10.9 Genèse 2.7 Genèse 3.19 Job 33.6 Genèse 18.27
20 Kati ya asubuhi na jioni huvunjwa-vunjwa; Waangamia milele wala hapana atiaye moyoni.
Job 20.7 Proverbes 10.7 Job 14.20 2 Chroniques 15.6 2 Chroniques 21.20
21 Je! Kamba ya hema yao haikung’olewa ndani yao? Wafa, kisha hali hawana akili.
Job 36.12 Job 8.22 Luc 16.22-16.23 Psaumes 49.20 Jacques 1.11

Cette Bible est dans le domaine public.