Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Accueil  /  Bible  /  Bible en Swahili de l’est  / Job 4     

Job 4
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 1 d’Éliphaz

1 Ndipo huyo Elifazi, Mtemani, akajibu na kusema,
Job 2.11 Job 15.1 Job 3.1-3.2 Job 42.9 Job 22.1
2 Mtu akijaribu kuzungumza nawe, je! Utaona ni vibaya? Lakini ni nani awezaye kujizuia asinene?
Job 32.18-32.20 Actes 4.20 Jérémie 6.11 2 Corinthiens 7.8-7.10 2 Corinthiens 2.4-2.6
3 Tazama, wewe umewafunza watu wengi, Nawe umeitia nguvu mikono iliyokuwa minyonge.
Esaïe 35.3 Hébreux 12.12 Esdras 6.22 Genèse 18.19 Colossiens 4.6
4 Maneno yako yamemtegemeza huyo aliyekuwa anaanguka, Nawe umeyaimarisha magoti manyonge.
Hébreux 12.12 Proverbes 12.18 Proverbes 16.23-16.24 2 Corinthiens 7.6 Daniel 5.6
5 Lakini sasa haya yamekufikilia wewe, nawe wafa moyo; Yamekugusa, nawe wafadhaika.
Job 19.21 Proverbes 24.10 Job 2.5 Job 3.25-3.26 Job 6.14
6 Je! Dini yako siyo mataraja yako, Na matumaini yako si huo uelekevu wa njia zako?
Proverbes 3.26 Job 1.1 Job 27.5-27.6 Job 17.15 Job 16.17
7 Kumbuka, tafadhali, ni nani aliyeangamia akiwa hana hatia? Au hao waelekevu, walikatiliwa mbali wapi?
Psaumes 37.25 2 Pierre 2.9 Actes 28.4 Job 36.7 Job 8.20
8 Kama mimi nilivyoona, hao walimao maovu, Na kupanda madhara, huvuna yayo hayo.
Proverbes 22.8 Galates 6.7-6.8 Osée 8.7 2 Corinthiens 9.6 Psaumes 7.14-7.16
9 Kwa pumzi za Mungu huangamia. Na kwa kuvuma kwa hasira zake humalizika.
Job 15.30 Esaïe 30.33 Esaïe 11.4 2 Thessaloniciens 2.8 Exode 15.8
10 Kunguruma kwake simba, na sauti ya simba mkali, Na meno ya simba wachanga, yamevunjika.
Psaumes 58.6 Job 29.17 Psaumes 3.7 Psaumes 57.4 Job 5.15
11 Simba mzee huangamia kwa kukosa mawindo, Nao watoto wa simba mke wametawanyika mbalimbali.
Psaumes 34.10 Nombres 23.24 Psaumes 7.2 Genèse 49.9 Job 1.19
12 Basi, nililetewa neno kwa siri, Sikio langu likasikia manong’ono yake.
Job 26.14 1 Corinthiens 13.12 Psaumes 62.11
13 Katika mawazo yaliyotoka katika maono ya usiku, Hapo usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu.
Job 33.14-33.16 Genèse 2.21 Genèse 15.12 Daniel 10.9 Daniel 2.19
14 Hofu iliniangukia na kutetema, Iliyoitetemesha mifupa yangu yote.
Habakuk 3.16 Daniel 10.11 Apocalypse 1.17 Psaumes 119.120 Job 33.19
15 Ndipo pepo ilipita mbele ya uso wangu; Na nywele za mwili wangu zilisimama.
Hébreux 1.7 Luc 24.37-24.39 Matthieu 14.26 Daniel 5.6 Esaïe 21.3-21.4
16 Hiyo pepo ilisimama kimya, nisiweze kutambua sura zake, Mfano ulikuwa mbele ya macho yangu; Kulikuwa kimya, nami nilisikia sauti, ikinena,
1 Rois 19.12
17 Je! Binadamu atakuwa na haki kuliko Mungu? Je! Mtu atakuwa safi kuliko Muumba wake?
Job 9.2 Job 25.4 Psaumes 143.2 Genèse 18.25 Job 35.2
18 Tazama, yeye hawategemei watumishi wake; Na malaika zake huwahesabia upuzi;
Jude 1.6 2 Pierre 2.4 Job 25.5-25.6 Job 15.15-15.16 Esaïe 6.2-6.3
19 Je! Si zaidi sana hao wakaao katika nyumba za udongo, Ambazo misingi yao i katika mchanga, Hao waliosetwa mbele ya nondo!
Job 10.9 Genèse 2.7 Genèse 3.19 Job 33.6 Job 13.12
20 Kati ya asubuhi na jioni huvunjwa-vunjwa; Waangamia milele wala hapana atiaye moyoni.
Job 20.7 Psaumes 90.5-90.6 Psaumes 39.13 Proverbes 10.7 Job 14.20
21 Je! Kamba ya hema yao haikung’olewa ndani yao? Wafa, kisha hali hawana akili.
Job 36.12 Luc 16.22-16.23 Job 8.22 Job 18.21 Psaumes 49.20

Cette Bible est dans le domaine public.