Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 16.5
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 5 de Job

1 Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
2 Nimesikia maneno mengi mfano wa hayo; Ninyi nyote ni wafariji wenye kutaabisha.
Job 13.4-13.5 Job 6.6 Job 6.25 Job 11.2-11.3 Job 19.2-19.3
3 Je! Maneno yasiyo faida yatakuwa na mwisho? Au, kuna nini kinachokukasirisha, hata ukajibu?
Job 6.26 Job 15.2 Job 32.3-32.6 Job 8.2 Tite 1.11
4 Mimi nami ningeweza kunena kama ninyi; Kama roho zenu zingekuwa mahali pa roho yangu, Ningeweza kutunga maneno juu yenu, Na kuwatikisia ninyi kichwa changu.
Psaumes 22.7 Psaumes 109.25 Lamentations 2.15 2 Rois 19.21 Jérémie 18.16
5 Lakini ningewatia nguvu kwa kinywa changu, Na utuzo wa midomo yangu ungetuliza.
Job 29.25 Galates 6.1 Job 6.14 Proverbes 27.9 Psaumes 27.14
6 Nijapokuwa nanena, huzuni yangu haitulizwi; Nijapokuwa najizuia, nimepunguziwa kitu gani?
Psaumes 88.15-88.18 Job 10.1 Psaumes 77.1-77.9
7 Lakini sasa amenichokesha; Jamii yangu yote umeifanya ukiwa.
Job 7.3 Job 1.15-1.19 Job 10.1 Michée 6.13 Psaumes 6.6-6.7
8 Umenishika sana, ni ushahidi juu yangu; Na kukonda kwangu kwaniinukia, kwanishuhudia usoni pangu.
Job 10.17 Job 19.20 Ruth 1.21 Esaïe 24.16 Psaumes 109.24
9 Amenirarua katika ghadhabu zake, na kunionea; Amesaga-saga meno juu yangu; Mtesi wangu hunikazia macho makali.
Lamentations 2.16 Psaumes 35.16 Job 13.24 Psaumes 37.12 Osée 6.1
10 Wamenifumbulia vinywa vyao; Wamenipiga shavuni kwa kunitukana; Hujikutanisha pamoja juu yangu.
Psaumes 22.13 Psaumes 35.15 Esaïe 50.6 Actes 23.2 Michée 5.1
11 Mungu amenitia kwa hao wapotovu, Na kunitupa mikononi mwao waovu.
Psaumes 31.8 Psaumes 27.12 Jean 19.16 Romains 11.32 Job 1.13-1.19
12 Nilikuwa katika raha, naye akanivunja-vunja; Naam, amenishika shingo, na kuniponda; Tena amenisimamisha niwe shabaha yake.
Job 7.20 Lamentations 3.4 Lamentations 3.11-3.12 Matthieu 21.44 Job 4.10
13 Wapigaji wake wa mishale hunizingira kotekote, Hunipasua viuno vyangu, asinihurumie; Nyonga zangu amezimwaga juu ya nchi.
Job 6.4 Job 20.25 Lamentations 2.11 2 Pierre 2.5 Romains 8.32
14 Hunivunja kwa uvunjifu juu ya uvunjifu; Hunishambulia mfano wa jitu shujaa.
Psaumes 42.7 Lamentations 3.3-3.5 Juges 15.8 Joël 2.7 Job 9.17
15 Nimeshona nguo ya magunia juu ya mwili wangu, Na pembe yangu nimeidhili uvumbini.
Genèse 37.34 Psaumes 7.5 Esaïe 22.12 Psaumes 75.5 1 Rois 21.27
16 Uso wangu umeharibika kwa kutoa machozi, Na giza tupu li katika kope zangu;
Psaumes 32.3 Psaumes 102.9 Psaumes 31.9 Marc 14.34 Job 17.7
17 Ijapokuwa hapana jeuri mikononi mwangu, Na kuomba kwangu ni safi.
Job 27.6-27.7 Jonas 3.8 Job 21.27-21.28 Psaumes 44.17-44.21 Job 15.34
18 Ee nchi, usiifunike damu yangu, Na kilio changu kisipate mahali pa kupumzika.
Esaïe 26.21 Ezéchiel 24.7 Genèse 4.11 Psaumes 66.18-66.19 Néhémie 4.5
19 Hata sasa, tazama, shahidi wangu yuko mbinguni. Na huyo atakayenidhamini yuko juu.
Romains 1.9 Psaumes 113.5 Genèse 31.50 1 Samuel 12.5 1 Thessaloniciens 2.5
20 Rafiki zangu hunidharau; Lakini jicho langu humwagia Mungu machozi;
Job 17.2 Psaumes 109.4 Luc 6.11-6.12 Job 16.4 Job 12.4-12.5
21 Laiti angemtolea mtu hoja mbele ya Mungu, Amtetee na mwanadamu mbele ya jirani yake.
Job 31.35 Job 23.3-23.7 Romains 9.20 Job 9.34-9.35 Job 13.3
22 Kwani ikiisha pita miaka michache, Nitakwenda njia hiyo ambayo sitarudi tena.
Job 14.10 Job 14.14 Job 7.9-7.10 Job 14.5 Ecclésiaste 12.5

Cette Bible est dans le domaine public.