Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 16.18
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 5 de Job

1 Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
2 Nimesikia maneno mengi mfano wa hayo; Ninyi nyote ni wafariji wenye kutaabisha.
Job 13.4-13.5 Psaumes 69.26 Philippiens 1.16 Job 26.2-26.3 Job 6.6
3 Je! Maneno yasiyo faida yatakuwa na mwisho? Au, kuna nini kinachokukasirisha, hata ukajibu?
Job 6.26 Job 15.2 Tite 2.8 Matthieu 22.46 Job 20.3
4 Mimi nami ningeweza kunena kama ninyi; Kama roho zenu zingekuwa mahali pa roho yangu, Ningeweza kutunga maneno juu yenu, Na kuwatikisia ninyi kichwa changu.
Psaumes 109.25 Psaumes 22.7 Lamentations 2.15 2 Rois 19.21 Jérémie 18.16
5 Lakini ningewatia nguvu kwa kinywa changu, Na utuzo wa midomo yangu ungetuliza.
Proverbes 27.17 Job 4.3-4.4 Esaïe 35.3-35.4 Job 29.25 Galates 6.1
6 Nijapokuwa nanena, huzuni yangu haitulizwi; Nijapokuwa najizuia, nimepunguziwa kitu gani?
Psaumes 88.15-88.18 Job 10.1 Psaumes 77.1-77.9
7 Lakini sasa amenichokesha; Jamii yangu yote umeifanya ukiwa.
Job 7.3 Job 1.15-1.19 Esaïe 50.4 Job 7.16 Job 29.5-29.25
8 Umenishika sana, ni ushahidi juu yangu; Na kukonda kwangu kwaniinukia, kwanishuhudia usoni pangu.
Job 10.17 Ruth 1.21 Job 19.20 Psaumes 106.15 Ephésiens 5.27
9 Amenirarua katika ghadhabu zake, na kunionea; Amesaga-saga meno juu yangu; Mtesi wangu hunikazia macho makali.
Psaumes 35.16 Lamentations 2.16 Job 13.24 Actes 7.54 Job 18.4
10 Wamenifumbulia vinywa vyao; Wamenipiga shavuni kwa kunitukana; Hujikutanisha pamoja juu yangu.
Psaumes 22.13 Psaumes 35.15 Lamentations 3.30 Esaïe 50.6 Actes 23.2
11 Mungu amenitia kwa hao wapotovu, Na kunitupa mikononi mwao waovu.
Psaumes 31.8 Psaumes 27.12 1 Samuel 24.18 Psaumes 7.14 Jean 19.16
12 Nilikuwa katika raha, naye akanivunja-vunja; Naam, amenishika shingo, na kuniponda; Tena amenisimamisha niwe shabaha yake.
Job 7.20 Lamentations 3.4 Lamentations 3.11-3.12 Psaumes 44.19 Job 7.12
13 Wapigaji wake wa mishale hunizingira kotekote, Hunipasua viuno vyangu, asinihurumie; Nyonga zangu amezimwaga juu ya nchi.
Job 6.4 Job 20.25 Lamentations 2.11 Job 6.10 Psaumes 7.12-7.13
14 Hunivunja kwa uvunjifu juu ya uvunjifu; Hunishambulia mfano wa jitu shujaa.
Psaumes 42.7 Lamentations 3.3-3.5 Juges 15.8 Joël 2.7 Job 9.17
15 Nimeshona nguo ya magunia juu ya mwili wangu, Na pembe yangu nimeidhili uvumbini.
Genèse 37.34 Psaumes 7.5 1 Rois 21.27 Esaïe 22.12 Psaumes 75.5
16 Uso wangu umeharibika kwa kutoa machozi, Na giza tupu li katika kope zangu;
Esaïe 52.14 Psaumes 116.3 Jonas 2.1-2.10 Psaumes 102.3-102.5 Psaumes 6.6-6.7
17 Ijapokuwa hapana jeuri mikononi mwangu, Na kuomba kwangu ni safi.
Job 22.5-22.9 Job 31.1-31.40 Proverbes 15.8 1 Timothée 2.8 Job 29.12-29.17
18 Ee nchi, usiifunike damu yangu, Na kilio changu kisipate mahali pa kupumzika.
Esaïe 26.21 Ezéchiel 24.7 Genèse 4.11 Psaumes 66.18-66.19 Job 27.9
19 Hata sasa, tazama, shahidi wangu yuko mbinguni. Na huyo atakayenidhamini yuko juu.
Romains 1.9 2 Corinthiens 11.31 Job 25.2 2 Corinthiens 1.23 1 Thessaloniciens 2.10
20 Rafiki zangu hunidharau; Lakini jicho langu humwagia Mungu machozi;
Hébreux 5.7 Psaumes 142.2 Osée 12.4-12.5 Job 17.2 Psaumes 109.4
21 Laiti angemtolea mtu hoja mbele ya Mungu, Amtetee na mwanadamu mbele ya jirani yake.
Job 31.35 Job 13.22 Job 40.1-40.5 Ecclésiaste 6.10 Job 23.3-23.7
22 Kwani ikiisha pita miaka michache, Nitakwenda njia hiyo ambayo sitarudi tena.
Job 14.10 Job 14.14 Job 7.9-7.10 Job 14.5 Ecclésiaste 12.5

Cette Bible est dans le domaine public.