Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 12.19
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 4 de Job

1 Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
2 Hapana shaka ninyi ndinyi watu halisi, Nanyi mtakapokufa, ndipo na hekima itakoma.
Job 11.6 Job 6.24-6.25 Job 15.2 Job 32.7-32.13 Job 17.10
3 Lakini mimi pia, nina fahamu kama ninyi; Mimi si duni yenu ninyi; Naam, ni nani asiyejua mambo kama hayo?
Job 13.2-13.5 Job 6.6-6.7 2 Corinthiens 11.21-11.23 Job 26.2-26.3 2 Corinthiens 11.5
4 Mimi ni mtu wa kuchekwa na jirani yake, Ni mtu niliyemwita Mungu, naye akanijibu; Huyo mwenye haki, aliye mtimilifu, amekuwa ni kicheko.
Job 21.3 Job 17.6 Job 30.1 Psaumes 91.15 Job 16.10
5 Katika mawazo yake huyo aliye na raha mna kudharau mashaka; Tayari kwa ajili ya wenye kuteleza miguu.
Jérémie 13.16 Luc 12.19 Matthieu 25.8 Proverbes 20.20 Job 18.5
6 Hema za wapokonyi hufanikiwa, Na hao wamkasirishao Mungu hukaa salama; Mikononi mwao Mungu huleta vitu vingi.
Job 9.24 Job 21.7-21.15 Psaumes 73.11-73.12 Psaumes 17.14 Psaumes 37.1
7 Lakini sasa waulize hao wanyama, nao watakufundisha; Na nyuni wa angani, nao watakuambia;
Proverbes 6.6 Job 21.29-21.30 Esaïe 1.3 Jérémie 8.7
8 Au nena na nchi, nayo itakufundisha; Nao samaki wa baharini watakutangazia.
9 Katika hawa wote ni yupi asiyejua, Kwamba ni mkono wa Bwana uliofanya haya?
Esaïe 41.20 Daniel 5.18 Jacques 2.5-2.7 Romains 11.36 Deutéronome 8.17-8.18
10 Ambaye nafsi ya kila kilicho hai i mkononi mwake, Na pumzi zao wanadamu wote.
Actes 17.28 Job 27.3 Nombres 16.22 Psaumes 146.3-146.4 Job 34.14-34.15
11 Je! Sikio silo lijaribulo maneno, Kama vile kaakaa lionjavyo chakula?
Job 34.3 Hébreux 5.14 1 Corinthiens 10.15 1 Pierre 2.3 Job 6.30
12 Wazee ndio walio na hekima, Na katika kuishi siku nyingi iko fahamu.
Job 32.7 Job 15.10 Job 8.8
13 Hekima na amri zina yeye [Mungu]; Yeye anayo mashauri na fahamu.
Job 9.4 Job 36.5 Proverbes 8.14 Job 11.6 1 Corinthiens 1.24
14 Tazama, yuavunja, wala haiwezekani kujenga tena; Humfunga mtu, wala haiwezekani kumfungua.
Apocalypse 3.7 Esaïe 22.22 Job 19.10 Malachie 1.4 Job 11.10
15 Tazama, yuayazuia maji, nayo yakatika; Tena, huyapeleka, nayo yaipindua dunia.
1 Rois 17.1 Amos 5.8 Deutéronome 11.17 Jacques 5.17-5.18 Genèse 6.17
16 Kwake yeye ziko nguvu, na makusudi kufanikiwa; Huyo adanganywaye, na mdanganyi pia ni wake.
Ezéchiel 14.9 Matthieu 6.13 Job 13.7 Job 12.13 1 Rois 22.22-22.23
17 Yeye huwaondoa washauri hali wametekwa nyara, Naye huwafanya waamuzi kuwa ni wapumbavu.
2 Samuel 17.23 Esaïe 29.14 1 Corinthiens 1.19-1.20 Esaïe 19.12-19.14 Job 9.24
18 Yeye hulegeza kifungo cha wafalme, Na kuwafunga viuno vyao kwa mshipi.
Daniel 2.21 Psaumes 116.16 2 Chroniques 33.11-33.14 Jérémie 52.31-52.34 Apocalypse 19.16
19 Yeye huwaondoa makuhani hali wametekwa nyara. Na kuwapindua mashujaa.
Josué 10.42 Job 35.9 Job 24.22 Apocalypse 17.14 1 Samuel 17.45-17.46
20 Huondoa matamko ya hao walioaminiwa, Na kuondoa fahamu za wazee.
Job 32.9 Job 17.4 Job 39.17 Job 12.24 Proverbes 12.22
21 Humwaga aibu juu ya hao wakuu, Na kulegeza mshipi wa wenye nguvu.
Psaumes 107.40 Esaïe 24.21-24.22 1 Rois 21.23-21.24 Actes 12.23 Esaïe 11.5
22 Huvumbua mambo ya siri tokea gizani, Na hicho kilicho giza tupu huleta mwangani.
Daniel 2.22 1 Corinthiens 4.5 Job 3.5 1 Corinthiens 2.10 Amos 5.8
23 Huyaongeza mataifa, na kuyaangamiza; Huyaeneza mataifa mbali, na kuyaacha.
Esaïe 26.15 Esaïe 9.3 Esaïe 60.22 Psaumes 107.38 Exode 1.7
24 Huwaondolea moyo wakuu wa watu wa nchi, Na kuwapoteza nyikani pasipokuwa na njia.
Psaumes 107.40 Job 12.20 Esaïe 6.9-6.10 Job 17.4 Esaïe 19.1
25 Wao hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga, Naye huwafanya kupepesuka kama vile mlevi.
Psaumes 107.27 Job 5.14 Esaïe 24.20 Esaïe 19.14 1 Jean 2.11

Cette Bible est dans le domaine public.